Siku ya Pili, 29 Mwezi wa 7
Nimekukubali.—Lu. 3:22.
Inatia moyo sana kujua kama Yehova anakubali watu wake wakiwa kikundi! Biblia inasema: “Yehova anafurahia watu wake.” (Zb. 149:4) Lakini, wakati fulani kuko Wakristo wenye wanaweza kuvunjika moyo na kujiuliza hivi: ‘Yehova ananikubali na miye?’ Watumishi fulani waaminifu wa Yehova wa zamani walijiuliza pia vile wakati fulani. (1 Sa. 1:6-10; Yob. 29:2, 4; Zb. 51:11) Biblia inaonyesha wazi kama wanadamu wenye hawakamilike wanaweza kukubaliwa na Yehova. Namna gani? Tunapaswa kukubali Yesu Kristo na kubatizwa. (Yoh. 3:16) Kwa kufanya vile tunaonyesha waziwazi kama tumetubu zambi zetu na tumemuahidi Mungu kama tutafanya mapenzi yake. (Mdo. 2:38; 3:19) Yehova anafurahi sana wakati tunafanya ile mambo ili kuwa marafiki wake wa karibu. Wakati tunaendelea kufanya yetu yote ili kuheshimia naziri yetu ya kujitoa kwake, Yehova anatukubali na kutuona kuwa marafiki wake.—Zb. 25:14. w24.03 26 fu. 1-2
Siku ya Tatu, 30 Mwezi wa 7
Hatuwezi kuacha kusema juu ya mambo yenye tumeona na kusikia.—Mdo. 4:20.
Tunaweza pia kuiga wanafunzi wa Yesu kwa kuendelea kuhubiri hata kama wenye mamlaka wanatukataza kufanya vile.Tuko hakika kama Yehova atatusaidia kutimiza utumishi wetu. Kwa hiyo, umuombe Yehova uhodari na hekima na akusaidie ili uvumilie magumu. Wengi kati yetu wako napambana na magumu ya kimwili ao ya kihisia, magumu ya kupoteza mupendwa wao, magumu fulani mu familia, mateso, ao magumu ingine. Na mambo sawa vile, magonjwa ya kuambukiza na vita imefanya ikuwe nguvu kuvumilia magumu mingi kati ya ile. Umufungulie Yehova moyo wako. Umuambie hali yako sawa vile tu unaweza kumuambia rafiki yako wa karibu sana. Ukuwe hakika kama Yehova “atatenda kwa ajili yako. (Zb. 37:3, 5) Kuendelea kusali kutakusaidia “uvumilie chini ya taabu.” (Ro. 12:12) Yehova anajua mambo yenye watumishi wake wako napambana nayo. “Anasikia kilio chao cha kuomba musaada.”—Zb. 145:18, 19. w23.05 5-6 fu. 12-15
Siku ya Ine, 31 Mwezi wa 7
Muendelee kuhakikisha ni nini yenye kukubaliwa kwa Bwana.—Efe. 5:10.
Wakati tunataka kukamata maamuzi ya maana, ni muzuri tutafute kujua “mapenzi ya Yehova” na kisha tutende kulingana nayo. (Efe. 5: 17) Wakati tunapata kanuni ya Biblia yenye inahusu hali yetu, ni sawa vile tuko natafuta mawazo ya Yehova kuhusu ile jambo. Na wakati tunatumikisha ile kanuni, tutaweza kukamata maamuzi ya muzuri. “Ule muovu,” adui yetu Shetani, anapenda tutumie wakati wetu wote ili kufuatilia mambo ya huu ulimwengu na tukose wakati wa kumutumikia Mungu. (1 Yo. 5:19) Inaweza kuwa mwepesi kwa Mukristo kutia pa nafasi ya kwanza vitu vya kimwili, elimu ya huu ulimwengu, ao kazi kuliko kutia utumishi wake kwa Yehova pa nafasi ya kwanza. Kama ile inatokea, inaweza kuonyesha kama ule Mukristo iko nachochewa na mawazo ya ulimwengu. Kusema kweli, ile mambo haiko ya mubaya, lakini haipaswe kuwa pa nafasi ya kwanza mu maisha yetu. w24.03 24 fu. 16-17