Cha Pili cha Mambo ya Nyakati
10 Rehoboamu alienda Shekemu,+ kwa maana Israeli wote walikuwa wamekuja Shekemu ili kumufanya kuwa mufalme.+ 2 Wakati tu Yeroboamu+ mwana wa Nebati alisikia habari hiyo (alikuwa angali Misri kwa sababu alikuwa amemukimbia Mufalme Sulemani),+ Yeroboamu akarudia kutoka Misri. 3 Basi wakatuma watu wamuite, na Yeroboamu na Israeli wote wakakuja kwa Rehoboamu na kusema: 4 “Baba yako alifanya nira yetu ikuwe nguvu.+ Lakini kama unafanya utumishi mugumu wa baba yako kuwa mwepesi zaidi na unapunguza uzito wa nira nzito* yenye aliweka juu yetu, tutakutumikia.”
5 Halafu akawaambia: “Murudie kwangu kisha siku tatu (3).” Basi watu wakaenda.+ 6 Kisha Mufalme Rehoboamu akafanya shauri pamoja na wanaume wazee* wenye walikuwa wamemutumikia Sulemani baba yake wakati alikuwa muzima, na kusema: “Munaweza kutoa shauri gani juu ya namna ya kujibu watu hawa?” 7 Wakamujibu: “Kama unakuwa mwema kwa watu hawa na unawafurahisha na kuwapatia jibu lenye kufaa, watakuwa watumishi wako sikuzote.”
8 Lakini, akakataa shauri lenye wanaume wazee* walimupatia, na akafanya shauri pamoja na vijana wenye walikomaa pamoja naye na wenye sasa walikuwa watumishi wake.+ 9 Akawauliza: “Munatoa shauri gani juu ya namna tunapaswa kujibu watu hawa wenye wameniambia, ‘Fanya nira yenye baba yako aliweka juu yetu kuwa mwepesi zaidi?” 10 Vijana hao wenye walikomaa pamoja naye wakamuambia: “Ni hivi unapaswa kuambia watu wenye wamekuambia, ‘Baba yako alifanya nira yetu kuwa nzito, lakini wewe unapaswa kuifanya kuwa mwepesi zaidi kwa ajili yetu’; ni hivi unapaswa kuwaambia: ‘Kidole changu kidogo kitakuwa kinene kuliko kiuno cha baba yangu. 11 Baba yangu aliweka nira nzito juu yenu, lakini mimi nitaongeza kwenye nira yenu. Baba yangu aliwapatia ninyi azabu kwa fimbo, lakini mimi nitawapatia azabu kwa mijeledi.’”
12 Yeroboamu na watu wote wakakuja kwa Rehoboamu siku ya tatu (3), kama vile mufalme alikuwa amesema: “Murudie kwangu siku ya tatu.”+ 13 Lakini mufalme akawajibu kwa ukali. Kwa hiyo Mufalme Rehoboamu akakataa shauri la wanaume wazee.* 14 Akawajibu kulingana na shauri la vijana, na kusema: “Nitafanya nira yenu kuwa nzito zaidi, na nitaongeza juu yake. Baba yangu aliwapatia ninyi azabu kwa fimbo, lakini mimi nitawapatia azabu kwa mijeledi.” 15 Basi mufalme hakusikiliza watu, kwa maana Mungu wa kweli ndiye alitokeza badiliko hilo la mambo,+ ili kutimiza neno lenye Yehova alikuwa amesema kupitia Ahiya+ Mushilo kwa Yeroboamu mwana wa Nebati.
16 Na kuhusu Israeli wote, kwa sababu mufalme alikataa kuwasikiliza, watu wakamujibu mufalme: “Tuko na fungu gani katika Daudi? Hatuna uriti wowote katika mwana wa Yese. Kila mutu aende kwa miungu yake, Ee Israeli! Sasa hangaikia nyumba yako mwenyewe, Ee Daudi.”+ Kwa hiyo Israeli wote wakarudia kwenye nyumba zao.*+
17 Lakini Rehoboamu akaendelea kutawala juu ya Waisraeli wenye walikuwa wanaishi katika miji ya Yuda.+
18 Kisha Mufalme Rehoboamu akamutuma Hadoramu,+ mwenye alikuwa musimamizi wa watu wenye waliandikishwa kwa ajili ya kazi ya kulazimishwa, lakini Waisraeli wakamupiga majiwe na kumuua. Mufalme Rehoboamu akaweza kupanda gari lake ili kukimbilia Yerusalemu.+ 19 Na Waisraeli wamekuwa wakiasi nyumba ya Daudi mupaka leo.