147 Mumusifu Yah!
Ni muzuri kumuimbia Mungu wetu sifa;
Inapendeza sana na inafaa sana kumusifu yeye!+
2 Yehova anajenga Yerusalemu;+
Anakusanya pamoja watu wa Israeli wenye walisambazwa.+
3 Anaponyesha wenye kuvunjika moyo;
Anafunga vidonda vyao.
4 Anahesabia jumla ya nyota;
Zote anaziita kwa majina.+
5 Bwana wetu ni mukubwa na mwenye nguvu nyingi sana;+
Uelewaji wake hauwezi kupimwa.+
6 Yehova anainua wapole,+
Lakini anatupa chini waovu.
7 Mumuimbie Yehova kwa shukrani;
Mumuimbie Mungu wetu sifa kwa kinubi,
8 Yeye mwenye kufunika mbingu kwa mawingu,
Yeye mwenye kupatia dunia mvua,+
Yeye mwenye kuchipusha majani+ juu ya milima.
9 Anapatia wanyama chakula,+
Kunguru wadogo wenye wanalia ili wakipate.+
10 Hafurahie nguvu za farasi;+
Wala hashangazwe na miguu yenye nguvu ya mutu.+
11 Yehova anafurahia wale wenye kumuogopa,+
Wale wenye kungojea upendo wake mushikamanifu.+
12 Umutukuze Yehova, Ee Yerusalemu.
Umusifu Mungu wako, Ee Sayuni.
13 Anafanya mapingo ya milango mikubwa ya muji wako yakuwe yenye nguvu;
Anabariki wana wako wenye kuwa ndani yako.
14 Analeta amani katika eneo lako;+
Anakushibisha kwa ngano ya muzuri kabisa.+
15 Anatuma amri yake katika dunia;
Neno lake linakimbia haraka sana.
16 Anatuma teluji kama manyoya ya kondoo;+
Anasambaza barafu nyembamba kama vile majivu.+
17 Anatupa chini majiwe yake ya mvua kama vipande vya mukate.+
Ni nani anaweza kuvumilia baridi yake?+
18 Anatuma neno lake, na inayeyuka.
Anafanya upepo wake uvume,+ na maji yanatiririka.
19 Anamutangazia Yakobo neno lake,
Na Israeli masharti yake na hukumu zake.+
20 Hajafanyia vile taifa lingine lolote;+
Hawajue kitu chochote kuhusu hukumu zake.
Mumusifu Yah!+