Zaburi
Nafsi yangu yote imusifu Yehova.+
2 Nitamusifu Yehova maisha yangu yote.
Nitamuimbia Mungu wangu sifa* wakati wote wenye nitakuwa muzima.
5 Mwenye furaha ni ule mwenye Mungu wa Yakobo ni musaidizi wake,+
Mwenye anamutumainia Yehova Mungu wake,+
6 Mutengenezaji wa mbingu na dunia,
Wa bahari, na vyote vyenye kuwa ndani,+
Yeye mwenye kuwa muaminifu sikuzote,+
7 Yeye mwenye kutenda haki kwa ajili ya wale wenye walipunjwa,
Yeye mwenye kupatia wenye njaa mukate.+
Yehova anaachilia huru wafungwa.+
8 Yehova anafungua macho ya vipofu;+
Yehova anasimamisha wale wenye kuinama chini;+
Yehova anapenda wenye haki.
9 Yehova analinda wakaaji wageni;
Anamutegemeza mutoto mwenye hana baba na mujane,+
10 Yehova atakuwa Mufalme milele,+
Mungu wako, Ee Sayuni, kizazi kwa kizazi.
Mumusifu Yah!*