Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Yeremia 13
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika Yeremia

      • Mushipi wa kitani wenye uliharibika (1-11)

      • Mitungi ya divai itavunjwa-vunjwa (12-14)

      • Yuda mwenye hawezi kubadilika atapelekwa katika uhamisho (15-27)

        • “Je, Mukushi anaweza kubadilisha ngozi yake?” (23)

Yeremia 13:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mushipi.”

Yeremia 13:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mushipi.”

Yeremia 13:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mushipi.”

Yeremia 13:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mushipi.”

Yeremia 13:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mushipi.”

  • *

    Ao “mushipi.”

Yeremia 13:9

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 26:19; Sef 3:11

Yeremia 13:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mushipi.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2Nya 36:15, 16
  • +Yer 6:28

Yeremia 13:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mushipi.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 19:5; Kum 26:18; Zab 135:4
  • +Yer 33:9
  • +Yer 6:17

Yeremia 13:12

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Amuka!,

    9/2015, uku. 7

Yeremia 13:13

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 29:9; 51:17; Yer 25:27

Yeremia 13:14

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 6:21; Eze 5:10
  • +Eze 7:4; 24:14

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Mkaribie Yehova, uku. 257-258

Yeremia 13:16

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 59:9

Yeremia 13:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “Nafsi yangu italia.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 9:1
  • +Zab 100:3

Yeremia 13:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mwanamuke muheshimiwa.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Fal. 24:12; Yer 22:24, 26

Yeremia 13:19

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “imezungukwa kwa ajili ya vita.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 28:64

Yeremia 13:20

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 6:22
  • +Eze 34:8

Yeremia 13:21

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 39:1, 2
  • +Yer 6:24; Mik 4:9

Yeremia 13:22

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 5:19; 16:10, 11
  • +Eze 16:37

Yeremia 13:23

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “Mwetiopia.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mez. 27:22

Yeremia 13:24

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 26:33; Kum 28:64

Yeremia 13:25

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 2:32
  • +Kum 32:37, 38; Isa 28:15; Yer 10:14

Yeremia 13:26

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Omb 1:8; Eze 16:37; 23:29

Yeremia 13:27

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “wa haya.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 2:20; Eze 16:15
  • +Isa 65:7; Eze 6:13
  • +Eze 24:13

Maandiko ingine

Yer. 13:9Law. 26:19; Sef 3:11
Yer. 13:102Nya 36:15, 16
Yer. 13:10Yer 6:28
Yer. 13:11Kut 19:5; Kum 26:18; Zab 135:4
Yer. 13:11Yer 33:9
Yer. 13:11Yer 6:17
Yer. 13:13Isa 29:9; 51:17; Yer 25:27
Yer. 13:14Yer 6:21; Eze 5:10
Yer. 13:14Eze 7:4; 24:14
Yer. 13:16Isa 59:9
Yer. 13:17Yer 9:1
Yer. 13:17Zab 100:3
Yer. 13:182 Fal. 24:12; Yer 22:24, 26
Yer. 13:19Kum 28:64
Yer. 13:20Yer 6:22
Yer. 13:20Eze 34:8
Yer. 13:21Isa 39:1, 2
Yer. 13:21Yer 6:24; Mik 4:9
Yer. 13:22Yer 5:19; 16:10, 11
Yer. 13:22Eze 16:37
Yer. 13:23Mez. 27:22
Yer. 13:24Law. 26:33; Kum 28:64
Yer. 13:25Yer 2:32
Yer. 13:25Kum 32:37, 38; Isa 28:15; Yer 10:14
Yer. 13:26Omb 1:8; Eze 16:37; 23:29
Yer. 13:27Yer 2:20; Eze 16:15
Yer. 13:27Isa 65:7; Eze 6:13
Yer. 13:27Eze 24:13
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Yeremia 13:1-27

Yeremia

13 Yehova aliniambia hivi: “Uende na ujinunulie mukaba* wa kitani na uuvae kuzunguka kiuno chako, lakini usiutie ndani ya maji.” 2 Basi nikanunua mukaba* kulingana na neno la Yehova na nikauvaa kuzunguka kiuno changu. 3 Na neno la Yehova likakuja kwangu mara ya pili: 4 “Kamata mukaba* wenye ulinunua na wenye umevaa na usimame, uende kwenye Efrati, na uufiche pale katika mupasuko wa mwamba.” 5 Basi nikaenda na nikauficha pembeni ya Efrati, kama vile Yehova alikuwa ameniamuru.

6 Lakini kisha siku nyingi Yehova akaniambia: “Simama, uende kwenye Efrati, na ukamate kutoka kule ule mukaba* wenye nilikuamuru uufiche kule.” 7 Basi nikaenda kwenye Efrati na nikachimba na kukamata ule mukaba* kutoka mahali kwenye nilikuwa nimeuficha, na nikaona kwamba mukaba* huo ulikuwa umeharibika; haukukuwa na mafaa kabisa.

8 Kisha neno la Yehova likakuja kwangu: 9 “Yehova anasema hivi: ‘Kwa njia ileile nitaharibu kiburi cha Yuda na kiburi kingi cha Yerusalemu.+ 10 Watu hawa waovu wenye wanakataa kutii maneno yangu,+ wenye kwa kichwa-nguvu wanafuata moyo wao wenyewe,+ na wenye wanafuata miungu mingine, wakiitumikia na kuiinamia, watakuwa tu kama mukaba* huu wenye hauna mafaa kabisa.’ 11 ‘Kwa maana kama vile mukaba* unashikamana na kiuno cha mutu, ni vile nilifanya nyumba yote ya Israeli na nyumba yote ya Yuda washikamane na mimi,’ ni vile Yehova anasema, ‘ili wakuwe kwangu watu,+ jina,+ sifa, na kitu kizuri. Lakini hawakutii.’+

12 “Na unapaswa pia kuwapatia ujumbe huu, ‘Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: “Kila mutungi mukubwa unapaswa kujazwa divai.”’ Na watakujibu, ‘Je, tayari hatujue kwamba kila mutungi mukubwa unapaswa kujazwa divai?’ 13 Kisha uwaambie, ‘Yehova anasema hivi: “Angalia, ninajaza ulevi wakaaji wote wa inchi hii,+ wafalme wenye kukaa kwenye kiti cha ufalme cha Daudi, makuhani na manabii, na wakaaji wote wa Yerusalemu. 14 Na nitawagonganisha mumoja na mwenzake, baba na wana pia,” ni vile Yehova anasema.+ “Sitawaonea huruma wala kuwa na huzuni wala kuwaonyesha rehema yoyote; hakuna kitu chenye kitanizuia kuwaharibu.”’+

15 Musikie na mukaze uangalifu.

Musikuwe na majivuno, kwa maana Yehova amesema.

16 Mumupatie Yehova Mungu wenu utukufu

Mbele alete giza

Na mbele ya miguu yenu kujikwaa kwenye milima mangaribi.

Mutatumaini kupata mwangaza,

Lakini ataleta kivuli kizito;

Ataugeuza kuwa giza nzito.+

17 Na kama munakataa kusikiliza,

Nitalia* kwa uficho kwa sababu ya kiburi chenu.

Nitatoa machozi mengi, na macho yangu yatatiririka machozi,+

Kwa sababu kundi la Yehova+ limekamatwa na kupelekwa mateka.

18 Mumuambie mufalme na malkia mama ya mufalme,*+ ‘Mukae mahali pa chini,

Kwa maana taji lenu lenye kupendeza litaanguka kutoka kwenye vichwa vyenu.’

19 Miji ya kusini imefungwa,* na hakuna mutu wa kuifungua.

Yuda yote imepelekwa katika uhamisho, imepelekwa katika uhamisho kabisa.+

20 Inua macho yako uone wale wenye wanakuja kutoka kaskazini.+

Liko wapi kundi lenye ulipewa, kondoo wako wenye kupendeza?+

21 Utasema nini wakati azabu yako itafika

Kutoka kwa marafiki wako wa karibu wenye ulifundisha tangu mwanzo?+

Je, maumivu ya kuzaa hayatakushika, kama ya mwanamuke mwenye kuzaa?+

22 Na wakati unasema katika moyo wako, ‘Sababu gani mambo haya yamenipata?’+

Ni kwa sababu ya kosa lako kubwa ndiyo maana umevuliwa pindo zako+

Na visigino vyako vimetendewa kwa jeuri.

23 Je, Mukushi* anaweza kubadilisha ngozi yake, ao chui madoa yake?+

Kama ni vile, basi munaweza kufanya mema,

Ninyi wenye mulizoezwa kufanya mabaya.

24 Basi nitawatawanya kama nyasi zenye kupeperushwa na upepo wa jangwa.+

25 Hii ndiyo kura yako, fungu lenye nimekupimia,” ni vile Yehova anasema,

“Kwa sababu umenisahau+ na unategemea uongo.+

26 Kwa hiyo, nitainua pindo zako juu ya uso wako,

Na haya yako itaonekana,+

27 Matendo yako ya uzinifu+ na milio yako ya tamaa kubwa ya ngono,

Ukahaba wako wenye kupotoka.*

Juu ya vilima, katika eneo la mashamba,

Nimeona mwenendo wako wenye kuchukiza.+

Ole wako, Ee Yerusalemu!

Utaendelea kuwa muchafu mupaka wakati gani?”+

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine