HABARI YA KUJIFUNZA YA 46
Yehova Anatuhakikishia Kama Atatimiza Ahadi ya Kuleta Paradiso
“Kila mutu mwenye anajitafutia baraka katika dunia abarikiwe na Mungu wa kweli.”—ISA. 65:16.
WIMBO 3 Nguvu Yangu, Tumaini Yangu, Ninakutegemea
KIFUPI YA HABARIa
1. Nabii Isaya alitolea Waisraeli wenzake ujumbe gani?
NABII Isaya alimuita Yehova kuwa “Mungu wa kweli.” Neno yenye kutafsiriwa “kweli” inamaanisha neno kwa neno “amina.” (Isa. 65:16, na maelzo ya chini.) “Amina” maana yake “ikuwe vile,” ao “hakika.” Wakati neno “amina” inatumiwa kuhusu Yehova ao Yesu mu Biblia, ni ili kuhakikisha kama jambo fulani ni ya kweli. Kwa hiyo, ujumbe wa Isaya kwa Waisraeli wenzake ulikuwa wazi, ni kusema, mambo yenye Yehova anaahidi ni yenye kutumainika siku zote. Yehova mwenyewe alionyesha vile kwa kutimiza kila jambo yenye aliahidi.
2. Juu ya nini tunaweza kutumainia ahadi za Yehova kuhusu wakati wetu wenye kuya, na tutazungumuzia maulizo gani?
2 Je, tunaweza pia kutumainia kama atatimiza ahadi zake kuhusu wakati wetu wenye kuja? Miaka karibu 800 kisha wakati wa Isaya, mutume Paulo alifasiria juu ya nini ahadi za Mungu ni zenye kutumainika siku zote. Paulo alisema hivi: “Haiwezekane Mungu aseme uongo.” (Ebr. 6:18) Vile tu chemchemi haiwezi kutosha maji ya muzuri na wakati uleule kutosha maji ya chumvi, Yehova, Chemchemi ao Chanzo ya kweli, hawezi kusema uongo. Kwa hiyo tunaweza kutumainia kabisa mambo yenye Yehova anasema kutia ndani ahadi zake kuhusu wakati wetu wenye kuya. Mu hii habari, tutazungumuzia hii maulizo: Yehova ameahidi kutupatia nini wakati wenye kuya? Na ni uhakikisho gani wenye Yehova ametupatia wenye unaonyesha kama ahadi zake zitatimia?
YEHOVA AMEAHIDI NINI?
3. (a) Watu wa Mungu wanapendaka sana ahadi gani? (Ufunuo 21:3, 4) (b) Watu fulani wanatendaka namna gani wakati tunawaonyesha ile ahadi?
3 Mu dunia yote watumishi wa Mungu wanapendaka sana ahadi yenye tutazungumuzia. (Soma Ufunuo 21:3, 4.) Yehova ameahidi kama kutakuwa wakati wenye “kifo hakitakuwa tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu havitakuwa tena.” Wakati tunahubiria wengine, wengi kati yetu tunatumiaka hii andiko yenye kutia moyo yenye kuzungumuzia namna maisha itakuwa mu Paradiso. Watu fulani wanatendaka namna gani wakati tunawaonyesha ile ahadi? Wanaweza kusema: “Ile ni ndoto tu.”
4. (a) Yehova alijua nini mbele ya wakati? (b) Zaidi ya kutoa ahadi Yehova alifanya nini ingine?
4 Bila shaka, wakati Yehova aliongoza mutume Yohana kuandika ile ahadi yenye kuzungumuzia namna maisha itakuwa mu Paradiso, Yehova alijua kama mu wakati wetu tutaelezea wengine kuhusu ile ahadi saa tunawahubiria ujumbe wa Ufalme. Pia Yehova alijua kama itakuwa nguvu kwa watu wengi kuamini ile ahadi yenye kuzungumuzia “mambo ya mupya.” (Isa. 42:9; 60:2; 2 Ko. 4:3, 4) Kwa hiyo, namna gani tunaweza kuhakikishia wengine na kujihakikishia wenyewe kama baraka zenye kuzungumuziwa mu Ufunuo 21:3, 4 zitatimia? Yehova hakutoa tu ile ahadi yenye kugusa moyo, lakini alitoa pia sababu zenye kuonyesha juu ya nini tunaweza kutumainia ile ahadi. Ni sababu gani njo zenye alitoa?
YEHOVA ANATOA UHAKIKISHO KAMA AHADI YAKE ITATIMIA
5. Tuko na sababu gani za kutumainia ahadi ya Mungu ya Paradiso, na tunaweza kuzipata wapi?
5 Mu mistari yenye kufuata tunapata sababu zenye zinatuchochea tutumainie ahadi ya Yehova kuhusu Paradiso. Ile mistari inasema hivi: “Ule mwenye kukaa kwenye kiti cha ufalme akasema: ‘Angalia! Ninafanya vitu vyote kuwa vipya.’ Tena anasema: ‘Andika, kwa maana maneno haya ni ya uaminifu na ya kweli.’ Na akaniambia: ‘Yamefanyika! Mimi ndiye Alfa na Omega, mwanzo na mwisho.’”—Ufu. 21:5, 6a.
6. Juu ya nini uhakikisho mbalimbali wenye kuwa mu Ufunuo 21:5, 6 unafanya tutumainie zaidi ahadi ya Mungu?
6 Juu ya nini ile andiko inafanya tutumainie zaidi ahadi ya Mungu? Kitabu Upeo wa Ufunuo inasema mambo yenye kufuata juu ya ile mistari: “Ni sawa vile Yehova mwenyewe alikuwa natilia wanadamu waaminifu sinyatire ya uhakikisho yenye kuonyesha kama zile baraka za wakati wenye kuya zitatimia.”b Ahadi ya Mungu inapatikana mu Ufunuo 21:3, 4. Kisha mu mustari wa 5 na wa 6, tunapata sinyatire ya mufano yenye kuhakikisha kama ile ahadi itatimia. Tuchunguze basi maneno yenye Yehova anatumia ili kuhakikisha kama ile ahadi itatimia.
7. Ni nani njo anaanza kuzungumuza mu mustari wa 5, na juu ya nini ile ni jambo ya pekee?
7 Mustari wa 5 unaanza na hii maneno: “Ule mwenye kukaa kwenye kiti cha ufalme akasema.” (Ufu. 21:5a) Ile ni maneno ya pekee juu inatanguliza maneno ya Yehova. Mu kitabu ya Ufunuo Yehova anazungumuza tu mara tatu na ile ni moja kati ya ile mara tatu. Kwa hiyo, haiko malaika mwenye nguvu ao hata Yesu mwenye kufufuliwa lakini Yehova mwenyewe njo anatoa ule uhakikisho! Ile inaonyesha kama tunaweza kutumainia kabisa maneno yenye kufuata. Juu ya nini? Juu Yehova “hawezi kusema uongo.” (Tit. 1:2) Ile inafanya maneno yenye tunasoma mu Ufunuo 21:5, 6 ikuwe yenye kutumainika kabisa.
“ANGALIA! NINAFANYA VITU VYOTE KUWA VIPYA”
8. Namna gani Yehova anakazia kama ahadi yake itatimia? (Isaya 46:10)
8 Sasa tuzungumuzie neno “Angalia!” (Ufu. 21:5) Neno ya Kigiriki yenye inatafsiriwa “angalia!” inarudiliwa mara mingi mu kitabu ya Ufunuo. Kitabu fulani inasema kama “ile neno ya mushangao inatumiwa ili kuchochea musomaji akazie uangalifu mambo yenye inafuata.” Ni mambo gani yenye inafuata kisha ile neno ya mushangao? Maneno yenye Mungu anasema: “Ninafanya vitu vyote kuwa vipya.” Bila shaka Yehova iko nazungumuzia mabadiliko ya wakati wenye kuya. Kwake ile ahadi ni ya hakika kabisa, kwa hiyo anazungumuzia ile mabadiliko sawa vile iko nafanyika tayari.—Soma Isaya 46:10.
9. (a) Maneno “ninafanya vitu vyote kuwa vipya” inaonyesha mambo gani mbili yenye Yehova atafanya? (b) Nini njo itafikia “mbingu” na “dunia” ya sasa?
9 Tuzungumuzie basi hii maneno yenye kufuata ya mu Ufunuo 21:5: “Ninafanya vitu vyote kuwa vipya.” Mu ile sura ile maneno inaonyesha mambo mbili yenye Yehova atafanya. Kwanza, ataharibu mupangilio wa zamani wa mambo. Pili, ataleta mupangilio mupya wa mambo. Ufunuo 21:1 inasema hivi: “Mbingu ya kwanza na dunia ya kwanza vilikuwa vimepita.” “Mbingu ya kwanza” ni serikali zenye kuchochewa na Shetani na mashetani wake. (Mt. 4:8, 9; 1 Yo. 5:19) Mu Biblia neno “dunia” inaweza kumaanisha wakaaji wa dunia. (Mwa. 11:1; Zb. 96:1) Kwa hiyo, “dunia ya kwanza” inamaanisha watu wabaya wenye kuishi mu dunia leo. Yehova hatatengeneza “mbingu” na “dunia” ya leo, lakini ataiharibu kabisa-kabisa. Pa nafasi ya mbingu na dunia ya leo ataweka “mbingu mupya na dunia mupya.” Ni kusema ataweka serikali ya mupya na mu dunia mutakuwa watu wenye haki.
10. Yehova atafanya nini kuwa upya?
10 Wakati tunaendelea kusoma Ufunuo 21:5, tunaona mambo yenye Yehova anasema kuhusu vitu vyenye atafanya kuwa vipya. Ona kama Yehova hakusema: “Ninafanya vitu vyote vipya.” Lakini alisema: “Ninafanya vitu vyote kuwa vipya.” Yehova atafanya kuwa upya dunia na wanadamu kwa kufanya wanadamu na dunia kuwa wakamilifu. Sawa vile Isaya alitabiri, dunia yote itafanywa kuwa bustani yenye kupendeza sawa bustani ya Edeni. Kila mutu kipekee atafanywa kuwa upya. Vilema, vipofu, na viziwi wataponyeshwa na hata wafu watafufuliwa.—Isa. 25:8; 35:1-7.
“MANENO HAYA NI YA UAMINIFU NA YA KWELI. . . . YAMEFANYIKA!”
11. Yehova aliamuru Yohana afanye nini, na juu nini alimuambia afanye vile?
11 Ni uhakikisho gani mwingine wenye unaonyesha kama ahadi ya Mungu itatimia? Yehova alisema hivi: “Andika, kwa maana maneno haya ni ya uaminifu na ya kweli.” (Ufu. 21:5) Yehova hakumuamuru tu Yohana ‘aandike,’ alimuambia pia sababu ya kufanya vile. Alisema hivi: “Kwa maana maneno haya ni ya uaminifu na ya kweli.” Ni kusema, maneno ya Mungu ni yenye kutegemeka na ni ya kweli. Tuko wenye furaha sana juu Yohana alitii wakati Mungu alimuamuru ‘aandike.’ Kwa sababu alifanya vile, tunaweza kusoma kuhusu ahadi ya Mungu ya kuleta Paradiso na kutafakari juu ya baraka za muzuri zenye ziko natungojea.
12. Juu ya nini Yehova iko na haki ya kusema: “Yamefanyika!”
12 Sasa Mungu anasema nini kisha? “Yamefanyika!” (Ufu. 21:6) Sasa Yehova anazungumuza mu njia yenye kuonyesha kama mambo yote yenye imezungumuziwa kuhusu Paradiso ilishatimia. Na iko na haki ya kuzungumuza vile juu hakuna kitu yenye inaweza kumuzuia kutimiza kusudi yake. Yehova anasema jambo ingine yenye inatuhakikishia kabisa kama ahadi yake itatimia. Anasema nini?
“MIMI NDIYE ALFA NA OMEGA”
13. Juu ya nini Yehova alisema: “Mimi ndiye Alfa na Omega”?
13 Sawa vile tuliona, Yehova mwenyewe alizungumuza mara tatu mu maono yenye Yohana aliona. (Ufu. 1:8; 21:5, 6; 22:13) Mu ile mara tatu Yehova alisema maneno ileile: “Mimi ndiye Alfa na Omega.” Alfa njo herufi ya kwanza mu alfabeti ya Kigiriki na omega njo herufi ya mwisho. Kwa kutumia maneno “Alfa na Omega,” Yehova anaonyesha kama wakati anaanza jambo fulani anaendelea nayo mupaka ifikie mwisho kabisa.
Wakati Yehova anaanza kufanya kitu fulani anaendelea mupaka kifikie mwisho (Ona fungu ya 14, 17)
14. (a) Toa mufano wenye kuonyesha wakati wenye kwa njia ya mufano Yehova alisema “Alpha,” na wakati wenye kwa njia ya mufano atasema “Omega.” (b) Mu Mwanzo 2:1-3 muko uhakikisho gani?
14 Kisha Yehova kuumba Adamu na Eva alionyesha kusudi yake kwa ajili ya wanadamu na dunia. Biblia inasema hivi: “Mungu akawaambia: ‘Muzae na mukuwe wengi, mujaze dunia na kuitawala.’” (Mwa. 1:28) Ile wakati ni sawa vile Yehova alisema “Alfa.” Alionyesha waziwazi kusudi yake: Kutakuwa wakati wenye wazao wa Adamu na Eva wenye kuwa wakamilifu na watiifu watajaza dunia na kuifanya kuwa Paradiso. Wakati ile itatimia ni sawa vile atasema “Omega.” Kisha kumaliza kuumba “mbingu na dunia pamoja na vitu vyote vyenye kuwa ndani yake,” Yehova alisema jambo fulani yenye ilihakikisha kama kusudi yake itatimia kabisa. Ile jambo inapatikana mu Mwanzo 2:1-3. (Soma.) Yehova alitia pembeni siku ya saba kuwa siku takatifu. Maana yake nini? Yehova alitoa uhakikisho kama bila shaka angetimiza kusudi yake kwa wanadamu na dunia. Ingetimia kabisa ku mwisho wa siku ya saba.
15. Juu ya nini ingeweza kuonekana kama Shetani alizuia kusudi ya Mungu isitimie?
15 Kisha Adamu na Eva kuasi, wakakuwa watenda-zambi na wakapitishia wazao wao zambi na kifo. (Ro. 5:12) Matokeo ilikuwa nini? Ingeweza kuonekana sawa vile Shetani alizuia kusudi ya Mungu ya kufanya dunia ijae wanadamu wakamilifu na watiifu. Ile ilionekana sawa vile Shetani alifanya isiwezekane kwa Yehova kusema “Omega.” Pengine Shetani aliwaza kama Yehova hakukuwa na jambo ingine ya kufanya. Jambo moja yenye angeweza kufanya ni kuua Adamu na Eva na kuumba bibi na bwana wengine wakamilifu ili aweze kutimiza kusudi yake kwa wanadamu. Lakini kama Mungu angefanya vile Ibilisi angemushitaki kuwa ni muongo. Juu ya nini? Juu sawa vile Mwanzo 1:28 inaonyesha, Yehova alikuwa ameambia Adamu na Eva kama ni wazao wao njo wangejaza dunia.
16. Juu ya nini pengine Shetani aliwaza kama angeweza kusema kama Yehova ameshindwa kutimiza ahadi yake?
16 Pengine Shetani aliwaza kawa Mungu angeamua kufanya nini ingine? Pengine Shetani aliwaza kama Yehova angeruhusu Adamu na Eva wazae watoto wenye hawako wakamilifu na wenye hawangefikiaka kuwa wakamilifu. (Muh. 7:20; Ro. 3:23) Yehova angefanya vile bila shaka Ibilisi angemushitaki kuwa ameshindwa. Juu ya nini? Juu ile haingetimiza kusudi ya Mungu ya kufanya dunia ijae wazao wa Adamu na Eva wenye kuwa wakamilifu na watiifu.
17. Namna gani Yehova alishugulikia uasi wa Shetani na wa wanadamu wa kwanza, na ku mwisho matokeo itakuwa nini? (Ona pia picha.)
17 Yehova alishugulikia uasi wa Shetani na wa wanadamu wa kwanza mu njia yenye Shetani hangewazia hata kidogo. (Zb. 92:5) Kuliko kuonekana kuwa muongo, Yehova alionyesha kama anasemaka kweli siku zote kwa kuruhusu Adamu na Eva wakuwe na watoto. Na kuliko kuonekana kuwa ameshindwa alifanya mambo mu njia yenye ilifanya apate ushindi. Alifanya kusudi yake iendelee kwa kutokeza “uzao” wenye ungeokoa wazao watiifu wa Adamu na Eva. (Mwa. 3:15; 22:18) Mupango wa Yehova wa bei ya ukombozi ulifanya Shetani aishiwe kabisa. Juu ya nini? Kwa sababu ule mupango unaonyesha kama Yehova iko na upendo wa kweli kabisa. (Mt. 20:28; Yoh. 3:16) Shetani hakuwake na ile sifa hata kidogo. Sasa mupango wa bei ya ukombozi ungekuwa na matokeo gani? Ku mwisho wa ile miaka elfu wazao wa Adamu na Eva wenye kuwa wakamilifu na watiifu wataishi mu dunia, sawa vile tu Yehova alikusudia tangu mwanzo. Ile wakati ni sawa vile Yehova atasema “Omega.”
NAMNA YA KUTUMAINIA ZAIDI AHADI YA YEHOVA YA KULETA PARADISO
18. Mungu anatupatia uhakikisho gani tatu? (Ona kisanduku “Sababu Tatu za Kutumainia Ahadi za Yehova.”)
18 Kulingana na mambo yenye tumeona, namna gani unaweza kuhakikishia wale wenye kuwa na mashaka kama ahadi ya Mungu ya kuleta Paradiso itatimia? Kwanza, ni Yehova mwenyewe njo ametoa ile ahadi. Kitabu ya Ufunuo inasema hivi: “Ule mwenye kukaa kwenye kiti cha ufalme akasema: “Angalia! Ninafanya vitu vyote kuwa vipya.’” Iko na hekima, iko na nguvu, na anapenda kabisa kutimiza ile ahadi. Pili, iko hakika kabisa kama ahadi yake itatimia njo maana anaizungumuzia mu njia yenye kuonyesha kama ilishatimia. Njo maana anasema hivi: “Maneno haya ni ya uaminifu na ya kweli. . . . Yamefanyika!” Tatu, wakati Yehova anaanza kufanya kitu fulani anaendelea mupaka kifikie mwisho, sawa vile maneno “mimi ndiye Alfa na Omega” inaonyesha. Yehova ataonyesha kama Shetani ni muongo na ameshidwa.
19. Wakati watu wako na mashaka kuhusu ahadi ya Mungu ya Paradiso, unaweza kufanya nini?
19 Kumbuka kama kila wakati wenye unahakikishia watu wenye unakutana nao mu mahubiri kama ahadi za Mungu zitatimia, unajihakikishia weye mwenyewe zaidi. Kwa hiyo wakati utasomea tena mutu ahadi yenye kutia moyo kuhusu Paradiso, yenye kuwa mu Ufunuo 21:4, kisha mutu anasema, “Ile ni ndoto tu,” unaweza kufanya nini? Hauone kama ni muzuri ikiwa unamusomea na kumufasiria mustari wa 5 na wa 6? Umuonyeshe namna Yehova amehakikisha kuwa ahadi yake itatimia kwa kuitilia yeye wenyewe sinyatire ya mufano.—Isa. 65:16.
WIMBO 145 Mungu Anatoa Ahadi ya Paradiso
a Mu hii habari tutaona uhakikisho mbalimbali wenye Yehova ametupatia wenye kuonyesha kama ahadi yake ya kuleta Paradiso itatimia. Kila wakati tunaambia wengine kuhusu ahadi za Yehova, ile inafanya siye wenyewe tuzitumainie zaidi.