Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w25 Mwezi wa 11 uku. 2-7
  • Uendelee Kuwa na Furaha mu Wakati wa Buzee

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Uendelee Kuwa na Furaha mu Wakati wa Buzee
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • JUU YA NINI INAWEZA KUWA NGUVU KUENDELEA KUWA NA FURAHA?
  • NAMNA YA KUENDELEA KUWA NA FURAHA
  • NAMNA BENGINE BANAWEZA KUSAIDIA
  • Uone Ndugu na Dada Wenye Walishazeeka Kuwa wa Maana Sana
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
  • Maneno ya Mwisho-Mwisho ya Banaume Baaminifu Inakufundisha Nini?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Itika Kama Kuko Mambo Yenye Haujue
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Namna ya Kufurahia Zaidi Mahubiri
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
w25 Mwezi wa 11 uku. 2-7

HABARI YA KUJIFUNZA YA 44

WIMBO 138 Uzuri wa Kichwa Yenye Imvi

Uendelee Kuwa na Furaha mu Wakati wa Buzee

‘Wakati wa uzee . . . watasitawi.’ —ZB. 92:14.

WAZO KUBWA

Juu ya nini ni jambo ya maana benye kuzeeka baendelee kuwa na furaha. Na namna banaweza kufanya vile.

1-2. Yehova iko na mawazo gani juu ya batumishi yake baaminifu benye kuzeeka? (Zaburi 92:12-14; ona pia ku jalada.)

KILA mutu iko na mawazo yake kuhusu kuzeeka. Kwa mufano, unakumbuka wakati uliona imvi mara ya kwanza mu kichwa yako? Pengine ulipendaka kuitosha mbele mutu mwingine aione. Lakini ukaelewa kama kuitosha haitafanya ingine isiote. Ile mufano inaonyesha vile batu mingi habapendake kuzeeka.

2 Lakini, Baba yetu wa mbinguni iko na mawazo tofauti juu ya batumishi yake benye kuzeeka. (Mez. 16:31) Anabafananisha na miti yenye kupendeza. (Soma Zaburi 92:12-14.) Juu ya nini? Mara mingi miti yenye ilishakawia inakuwaka na mayani na maua ya mingi sana. Kwa mufano mu Japon muko aina ya muti yenye inaishi miaka mingi. Mu ile aina ya muti, miti ya kupendeza sana iko na miaka zaidi ya elfu moya. Sawa vile tu ile miti yenye ilishakawia, batumishi ya Yehova benye kuzeeka ni ba maana kwake. Yehova haonake tu imvi ku benye kuzeeka, lakini anaonaka pia sifa zabo za muzuri, sawa vile uvumilivu na ushikamanifu wabo, pia anaonaka vile bamemutumikia kwa uaminifu kwa miaka mingi.

Bibi na bwana benye kuzeeka banaikala inje, na miti ya maua inabazunguuka.

Sawa tu vile muti wenye kukomala sana wenye kupendeza na wenye unaendelea kutoa maua, ndugu na dada baaminifu benye kuzeeka ni benye kupendeza na banaendelea kutoa matunda. (Ona fungu ya 2)


3. Toa mufano wenye unaonyesha namna Yehova alitumikisha benye kuzeeka juu ya kutimiza kusudi yake.

3 Yehova anaendelea kutuona ba maana hata kama tulishazeeka.a Na hata mara mingi Yehova anatumikishaka benye balishazeeka juu ya kutimiza kusudi yake. Kwa mufano, Sara alikuwa alishazeeka wakati Yehova alimuambia kama atakuwa mama wa taifa kubwa yenye itatokeza Masiya. (Mwa. 17:15-19) Pia, Musa alikuwa alishakuwa mutu muzima wakati Yehova alimupatia mugao wa kuongoza Baisraeli kutoka Misri. (Kut. 7:6, 7) Na mutume Yohana alikuwa alishazeeka wakati Yehova alimuongoza aandike bitabu tano bya Biblia.

4. Kulingana na Mezali 15:15, ni nini inaweza kusaidia benye balishazeeka bavumilie magumu? (Ona pia picha.)

4 Benye kuzeeka banapataka magumu ya mingi yenye inakuyaka na buzee. Dada moya alisema hivi: “Kuzeeka haiko muzaha.” Lakini kuwa na furahab kunaweza kusaidia benye balishazeeka bavumilie magumu yenye inakuyaka na buzee. (Soma Mezali 15:15.) Mu hii habari tutazungumuzia mambo yenye Bakristo benye balishazeeka banaweza kufanya juu baendelee kuwa na furaha. Tutaona pia mambo yenye bengine banaweza kufanya mu kutaniko juu ya kubasaidia. Kwanza, tuone juu ya nini inaweza kuwa nguvu kuendelea kuwa na furaha wakati tunazeeka.

Bibi na bwana benye tuliona ku picha yenye ilitangulia, banakamatana na biko nacheka wakati banasimama chini ya muti yenye iko na maua.

Kama unaona na kufurahia mambo yote yenye Yehova iko nakufanyia utakuwa na furaha hata kama uko na magumu (Ona fungu ya 4)


JUU YA NINI INAWEZA KUWA NGUVU KUENDELEA KUWA NA FURAHA?

5. Ni nini inaweza kufanya batu fulani benye kuzeeka bavunjike moyo?

5 Nini njo inaweza kufanya uvunjike moyo? Pengine unajisikia mubaya juu hauwezi kufanya byenye ulikuwaka nafanya zamani. Unaweza kuwaza hivi: ‘Kama ningekuwa ningali kijana na afya ya muzuri, ningefanya hivi na hivi.’ (Muh. 7:10) Kwa mufano, dada mwenye jina yake Ruby anasema hivi: “Ni nguvu kwangu kujivalisha manguo juu mara mingi ninakuwaka na maumivu na siwezi kujitikisa-tikisa sawa zamani. Kitu ya mwepesi sawa tu kunyangula mugulu juu ya kuvala mashosete ilishakuwa nguvu kwangu. Mikono yangu inanilumaka na siwezake kutumikisha muzuri hata bidole yangu. Ile inafanya ikuwe nguvu kwangu kufanya hata kazi za mwepesi.” Ndugu Harold, mwenye alikuwaka natumikia ku Beteli, anasema hivi: “Siamini kama miye njo nilishakuwa hivi. Wakati nilikuwaka kijana nilikuwaka na nguvu ya mingi. Nilikuwaka napenda sana michezo. Bengine balikuwaka nasema, ‘mupatie Harold kabumbu yeye njo hashindwake.’ Lakini leo, ninawaza kama siwezi hata kutupa kabumbu. Ninajisikiaka mubaya kuona vile nilishakuwa.”

6. (a) Ni nini ingine inaweza kufanya batu fulani benye kuzeeka bavunjike moyo? (b) Nini njo inaweza kusaidia benye kuzeeka baamue kama banaweza kuendelea kutembeza gari ao hapana? (Ona habari “Niache Kutembeza?” yenye iko mu hii gazeti)

6 Unaweza kuvunjika moyo wakati hauweze tena kufanya mambo fulani weye peke, zaidi sana kama uko na lazima ya mutu wa kukuhangaikia ao kama inaomba uhamie kwa mutoto wako. Pengine unaweza kuvunjika moyo juu hauwezi kuenda fasi weye peke, ao hauwezi kutembeza gari juu afya yako ilishaharibika ao juu hauonake tena muzuri. Ile inaweza kufanya ujisikie mubaya sana! Lakini hata kama hauwezi kujihangaikia weye peke, kuishi weye peke, ao kutembeza gari, ukumbuke kama uko wa maana sana kwa Yehova na kwa bengine. Kukumbuka ile kunaweza kukutia moyo. Pia ukuwe hakika kama Yehova anaelewa vile uko najisikia. Yehova anajua kama unamupenda sana na unapenda pia bandugu na badada yako. Njo maana anakuona kuwa wa maana sana.—1 Sa. 16:7.

7. Nini njo inaweza kukusaidia kama unahuzunika juu unawaza kama mwisho utafika na hauko tena muzima?

7 Inawezekana unahuzunika juu unawaza kama pengine mwisho utakuya na hauko tena muzima. Nini njo inaweza kukusaidia kama unajisikia vile? Ujikaze kukumbuka kama Yehova iko nangoya kwa hamu kuharibu huu ulimwengu muovu. (Isa. 30:18) Lakini kuko sababu yenye inafanya aendelee kuvumilia. Ile uvumilivu yake inapatia batu mingi nafasi ya kufikia kumujua na kumutumikia. (2 Pe. 3:9) Kwa hiyo kama unavunjika moyo, ukumbuke kama batu mingi banaweza kufikia kumujua Yehova mbele mwisho ufike na banaweza kuokolewa. Mutu hajuake, pengine kati yabo kutakuwa batu ya familia yako.

8. Wakati mutu mwenye kuzeeka anagonjwa ao iko na maumivu, ile inaweza kumufanya atende namna gani?

8 Ikuwe tulishazeeka ao hapana, wakati tunajisikia mubaya inakuwaka mwepesi kusema ao kufanya jambo yenye tutahuzunikia kisha. (Muh. 7:7; Yak. 3:2) Kwa mufano, juu ya magumu mingi yenye mwanaume muaminifu Yobu alipata, wakati fulani alikuwa na “mazungumuzo ya ovyoovyo.” (Yob. 6:1-3) Zaidi ya ile, magonjwa inaweza kufanya benye balishazeeka baseme ao kufanya mambo yenye habangesema ao kufanya kama habangekuwa bagonjwa. Hata vile, tukumbuke kama haiko juu tu tulishazeeka ao tuko bagonjwa njo tunakuwa na sheria ya kutendea bengine mubaya ao kubakaza bafanye byenye siye tunapenda. Njo maana kama tunatambua kama tulishasema jambo fulani yenye haikufurahisha mutu, tukuwe tayari kumulomba musamaha.—Mt. 5:23, 24.

NAMNA YA KUENDELEA KUWA NA FURAHA

Tawi ya muti yenye maua; picha zenye kuonyesha namna ndugu na dada benye kuzeeka banaweza kuendelea kuwa na furaha. Zile picha zinafasiriwa mu fungu ya 9-13.

Unaweza kufanya nini juu uendelee kuwa na furaha hata kama uko napambana na magumu ya buzee? (Ona fungu ya 9-13)


9. Juu ya nini unapaswa kuitika musaada wa bengine? (Ona pia picha.)

9 Kubali musaada wa bengine. (Gal. 6:2) Inaweza kuwa nguvu kukubali musaada wa bengine. Dada mwenye jina yake Gretl anasema hivi: “Wakati fulani inakuwaka nguvu kwangu kukubali musaada wa bengine juu ninaonaka sawa vile nitakuwa muzigo kwabo. Imenikamata wakati mingi juu ya kubadilisha ile mawazo na kuitika kama niko na lazima ya musaada.” Wakati unaitika bengine bakusaidie, unabapatia nafasi ya kuwa na furaha ya kutoa. (Mdo. 20:35) Na bila shaka utafurahi kuona vile bengine banakupenda na banakuhangaikia.

Dada mwenye kuzeeka anakamata mukono wa dada kijana wakati biko mu soko.

(Ona fungu ya 9)


10. Juu ya nini unapaswa kukumbuka kuonyesha shukrani? (Ona pia picha.)

10 Onyesha shukrani. (Kol. 3:15; 1 Te. 5:18) Wakati bengine banatufanyia mambo ya muzuri, tunakuwaka benye shukrani. Lakini, tunaweza kusaabu kuonyesha shukrani. Kwa hiyo, kama barafiki yetu banatufanyia jambo fulani ya muzuri, tunaweza kuonyesha sura ya kicheko na kusema aksanti. Ile inaweza kufanya baone kama tulifurahia byenye balitufanyia. Leah, mwenye anahangaikiaka benye kuzeeka ku Beteli anasema hivi: “Dada mumoya mwenye ninahangaikiaka, ananiandikiaka ku karatasi maneno ya kunishukuru. Inakuwaka tu maneno ya mufupi lakini inanigusaka sana. Napendaka sana kusoma byenye aliniandikia. Nafurahiaka kujua kama anaona musaada wangu kuwa maana.”

Dada mwenye kuzeeka iko naandika ku karte maneno ya shukrani.

(Ona fungu ya 10)


11. Namna gani unaweza kusaidia bengine? (Ona pia picha.)

11 Ujikaze kusaidia bengine. Kama unatumikisha wakati wako na nguvu yako juu ya kusaidia bengine, ile itakusaidia usikazie sana magumu yako. Mezali moya ya Afrika inalinganisha benye kuzeeka na bitabu bya hekima. Lakini kama bile bitabu binaikala tu mu kabati habitasaidia kitu. Vilevile kama batu benye kuzeeka banaikala tu kimya, vijana hawawezi kujifunza kitu kutoka kwabo. Uulize vijana maulizo na uwasikilize. Uwasaidie waelewe juu ya nini kutumikisha kanuni za Yehova kunakuwaka tu na faida na kunaletaka furaha. Bila shaka utakuwa na furaha sana wakati unafariji na kutia nguvu vijana.—Zb. 71:18.

Ndugu mwenye kuzeeka iko nasikiliza wakati ndugu kijana iko namufungulia moyo wake.

(Ona fungu ya 11)


12. Sawa vile Isaya 46:4 inaonyesha, Yehova anaahidi kufanyia nini benye balishazeeka? (Ona pia picha.)

12 Umuombe Yehova akupatie nguvu. Unaweza kuchoka kimwili ao kiakili, lakini Yehova yeye “hachokake wala kuishiwa nguvu.” (Isa. 40:28) Yehova anatumikisha namna gani nguvu yake yenye haina mipaka? Anaitumikishaka mu njia za mingi, sawa vile kutia nguvu batumishi yake baaminifu benye balishazeeka. (Isa. 40:29-31) Na hata, anaahidi kama atabasaidia. (Soma Isaya 46:4.) Na tunajua kama ahadi zake zote zinatimiaka. (Yos. 23:14; Isa. 55:10, 11) Wakati unasali na unajionea vile Yehova anakupenda na kukutegemeza, ile itakuletea furaha.

Ndugu mwenye kuzeeka iko nasali.

(Ona fungu ya 12)


13. Sawa tu vile 2 Wakorinto 4:16-18 inaonyesha, tunapaswa kukumbuka nini? (Ona pia picha.)

13 Kumbuka kama hali yako ni ya wakati kidogo tu. Wakati tunakumbuka kama magumu yetu ni ya wakati kidogo, ile inafanya ikuwe mwepesi kwetu kuivumilia. Na Biblia inatuhakikishia kama buzee na magonjwa, nayo ni ya wakati kidogo, itaisha. (Yob. 33:25; Isa. 33:24) Kwa hiyo, utakuwa na furaha kama unakumbuka kama maisha yenye ulikuwaka nayo wakati ulikuwa kijana haiko kitu kama unailinganisha na maisha yenye utakuwa nayo wakati wenye kuya. (Soma 2 Wakorinto 4:16-18.) Sasa, siye bengine tunaweza kufanya nini juu ya kusaidia benye kuzeeka?

Dada mwenye kuzeeka iko mu kinga ya bilema na iko nasoma Biblia. Anajiwazia iko mu Paradiso na alishakuwa kijana, anaacha kinga yake ya bilema na anaanza kutembea.

(Ona fungu ya 13)


NAMNA BENGINE BANAWEZA KUSAIDIA

14. Juu ya nini ni jambo ya maana kutembelea na kuita benye kuzeeka?

14 Ukuwe na zoezi ya kutembelea na kuita benye kuzeeka. (Ebr. 13:16) Benye kuzeeka banaweza kujisikia kuwa peke yabo. Ndugu Camille mwenye hawezi kutoka ku nyumba anasema hivi: “Ninabakiaka mu nyumba kuanzia asubui mupaka mangaribi. Ile inafanyaka nisikie buvivu sana. Wakati fulani ninajisikiaka sawa simba wa kuzeeka mwenye balishafungia mu lupango. Ile inafanyaka nikuwe na mahangaiko na nisikie bisirani.” Wakati tunatembelea benye kuzeeka, tunabaonyesha kama ni ba maana kwetu na kama tunabapenda. Pengine, kuko siku tulipangaka kuenda tembelea ndugu mwenye kuzeeka wa mu kutaniko yetu, lakini hatukuendaka. Ni kweli siye bote tunakuwaka na bya mingi bya kufanya. Lakini, nini njo inaweza kukusaidia ‘uhakikishe mambo ya maana zaidi,’ sawa vile kutembelea benye kuzeeka? (Flp. 1:10) Kitu moya yenye inaweza kukusaidia, ni kutia alama ku kalendrie juu ikukumbushe kutumia ujumbe ao kuita mutu mwenye kuzeeka wa mu kutaniko yako. Unaweza pia kupanga wakati wenye utamutembelea, na uchagule siku na saa juu usisaabu kuenda.

15. Vijana na benye kuzeeka banaweza kufanya nini pamoya?

15 Kama uko kijana unaweza kujiuliza utaongea nini, ao utafanya nini pamoya na mutu mwenye alishazeeka. Lakini usijihangaishe juu ya ile, ukuwe tu rafiki muzuri. (Mez. 17:17) Zungumuza na benye kuzeeka mbele na kisha mikutano. Kwa mufano, unaweza kuuliza mutu mwenye kuzeeka ni andiko gani njo anapendaka sana, ao ni kitu gani ya mu butoto ya kuchekesha yenye anakumbuka. Ao tena unaweza kumualika juu muangalie pamoya programe ya Télédiffusion. Kuko mambo ingine yenye unaweza kufanyia mutu mwenye kuzeeka. Kwa mufano, unaweza kuangalia kama tablete yake ao telefone yake iko natumika muzuri, na kama iko na bichapo bya mupya. Dada mwenye jina yake Carol anasema hivi: “Ufanye pamoya na benye kuzeeka mambo yenye unapendaka kufanya. Hata kama nilishazeeka ninapendaka tu kufurahia maisha. Ninapendaka kuenda kuuza bitu, kuenda kula ku restora, na kutembelea fasi za muzuri juu ya kuona uumbaji.” Na dada mwenye jina yake Maira anasema hivi: “Rafiki yangu mumoya iko na miaka 90. Ananishinda miaka 57, lakini sikumbukake kama hatuna miaka moya juu tunachekaka pamoya na kuangalia mafilme pamoya. Na wakati mumoya wetu anapata magumu, analombaka mwenzake mashauri.”

16. Juu ya nini inaweza kuwa muzuri kusindikiza benye kuzeeka ku hopitali?

16 Ubasindikize ku hopitali. Unaweza kupeleka ndugu ao dada mwenye kuzeeka ku hopitali, na kubakia pale pamoya naye juu ya kuwa hakika kama banganga biko namutendea muzuri, na biko namupatia musaada wenye iko nao lazima. (Isa. 1:17) Wakati iko naongea na munganga, unaweza kuandika byenye munganga iko nasema. Dada mwenye kuzeeka mwenye kuitwa Ruth anasema hivi: “Mara mingi, wakati ninaenda miye peke ku hopitali, munganga haaminiake byenye niko nasema. Anaweza kusema maneno sawa vile, ‘ni mu kichwa tu njo uko nawaza kama unagonjwa, lakini uko tu sawa.’ Lakini kama mutu ananisindikiza, munganga ananitendeaka muzuri zaidi. Ninashukuru bandugu na badada yangu benye bananisindikizaka.”

17. Ni mu njia gani mbalimbali tunaweza kuhubiri na benye kuzeeka?

17 Hubiri pamoya nabo. Bakristo fulani benye kuzeeka habana nguvu ya kuhubiri nyumba kwa nyumba. Kwa hiyo unaweza kualika dada mwenye kuzeeka juu uhubiri pamoya naye ku prezantware. Unaweza hata kumuletea kiti juu aikale pembeni ya prezantware. Ao unaweza kuongoza funzo yako ya Biblia pamoya na ndugu mwenye kuzeeka. Pengine, unaweza hata kubeba mwanafunzi wako kwake. Bazee ya kutaniko banaweza kamata mipango juu mikutano ya mahubiri ifanywe kwa Mukristo mwenye kuzeeka juu ikuwe mwepesi kwake kuhuzuria. Yehova anafurahiaka sana wakati tunajikaza kuonyesha benye kuzeeka upendo na heshima.—Mez. 3:27; Ro. 12:10.

18. Tutazungumuzia nini mu habari yenye kufuata?

18 Tunaona kama Yehova anapenda batumishi yake benye kuzeeka na anabaona kuwa ba maana. Na siye pia tunabapenda na kubaona kuwa ba maana! Buzee bunakuyaka na magumu yake, lakini kwa musaada wa Yehova unaweza kuendelea kuwa na furaha. (Zb. 37:25) Inatia moyo kujua kama bya muzuri biko mbele yako hapana nyuma yako! Tuseme nini sasa juu ya bale benye biko nahangaikia mutu wa familia mwenye alishazeeka, mutoto, ao rafiki mwenye iko mugonjwa? Banaweza kufanya nini juu baendelee kuwa na furaha? Tutazungumuzia ile mu habari yenye kufuata.

UTAJIBU NAMNA GANI?

  • Ni mambo gani yenye inaweza kufanya bandugu na badada benye kuzeeka bapoteze furaha yabo?

  • Benye kuzeeka banaweza kufanya nini juu baendelee kuwa na furaha?

  • Tunaweza kufanya nini mu kutaniko juu ya kusaidia benye kuzeeka?

WIMBO 30 Baba Yangu, Mungu Wangu, na Rafiki Yangu

a Ona ku jw.org ao ku JW Library® video, Wakristo Wenye Kuzeeka Ni wa Maana.

b MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Furaha ni sifa yenye kuwa sehemu ya tunda ya roho ya Mungu. (Gal. 5:22) Kuwa na urafiki wa karibu pamoya na Yehova njo kunaletaka furaha ya kweli.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine