MAMBO YA KUFANYA WAKATI BITU BINAPANDA BEI
Ukuwe na Tumaini
Bitu binapanda bei sana mu inchi yenu kupita hata makuta yenye unapataka? Uko najiuliza namna gani utapata bitu byenye weye na familia yako muko nabyo lazima? Kama ni vile, pengine unaweza kuogopa juu ya wakati yako yenye iko nakuya. Lakini hata mu hali ya nguvu vile, ni jambo ya maana sana kukuwa na tumaini.
JUU YA NINI NI JAMBO YA MAANA KUKUWA NA TUMAINI
Mutu mwenye iko na tumaini hatazamie tu kama mambo ya muzuri itafika. Tumaini inamusaidia afanye pia kile kyenye anaweza mu hali yenye anajikuta. Kwa mufano, batu fulani bamevumbula kama mutu mwenye iko na tumaini . . .
- anawezaka kuvumilia muzuri zaidi hali ya nguvu 
- anakuwaka tayari kujipatanisha na kila hali 
- anakamataka maamuzi ya muzuri, na ile inafanya akuwe na afya ya muzuri na maisha ya muzuri 
UNAWEZA KUFANYA NINI
Kwanza, ona namna Biblia inaweza kukusaidia leo. Biblia iko na mashauri ya mingi yenye inaweza kukusaidia ujue mambo ya kufanya wakati bitu binapanda bei. Tena, inaweza kukusaidia juu usijisikie sawa vile hauna tumaini lakini ujue mambo ya kufanya leo na mu wakati yenye iko nakuya kama hali inakuwa nguvu.
Pili, ona mambo yenye Biblia inasema juu ya wakati yenye iko nakuya. Wakati utatambua kama mashauri yenye iko mu Biblia ni ya hekima, ile itakuchochea ujifunze mambo mingi zaidi kuhusu byenye Biblia inasema juu ya wakati yenye iko nakuya. Kwa mufano, utajifunza kama Mungu anapenda ukuwe na “wakati wenye kuja wa muzuri na tumaini,” na anakupatia pia sababu ya kuamini kama ile tumaini ni ya kweli kabisa. (Yeremia 29:11) Ile sababu ya tumaini yetu ni Ufalme wa Mungu.
UFALME WA MUNGU NI NINI, NA UTAFANYA NINI?
Ufalme wa Mungu ni guvernema (ao serikali) yenye itatawala dunia muzima. (Danieli 2:44; Matayo 6:10) Ile wakati, bumaskini na mateso yote itaisha kabisa, na kila mutu ataishi kwa amani na atakuwa na kila kitu yenye iko nayo lazima juu aendelea kuwa na furaha. Ona vile Biblia inasema juu ya ile mambo.
Mamilioni ya batu leo banaamini zile ahadi juu banaamini kama Mungu “hawezi kusema uongo.” (Tito 1:2) Kwa hiyo ni jambo ya muzuri ukuwe najisomea Biblia weye peke. Tumaini yenye Biblia inaleta inaweza kukusaidia uvumilie wakati wa magumu na ukuwe hakika kama wakati yenye iko nakuya itakuwa ya muzuri.