Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 22
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Mwanzo—Yaliyomo

      • Abrahamu aambiwa amtoe Isaka (1-19)

        • Uzao wa Abrahamu utaleta baraka (15-18)

      • Familia ya Rebeka (20-24)

Mwanzo 22:1

Marejeo

  • +Ebr 11:17

Mwanzo 22:2

Marejeo

  • +Yoh 3:16
  • +Mwa 17:19; Yos 24:3; Ro 9:7
  • +2Nya 3:1

Mwanzo 22:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kisu cha kuchinjia.”

Mwanzo 22:8

Marejeo

  • +Yoh 1:29; 1Pe 1:18, 19

Mwanzo 22:9

Marejeo

  • +Yoh 10:17, 18

Mwanzo 22:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kisu cha kuchinjia.”

Marejeo

  • +Ebr 11:17

Mwanzo 22:12

Marejeo

  • +Ebr 11:17-19; Yak 2:21

Mwanzo 22:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Maana yake “Yehova Ataandaa; Yehova Atahakikisha Jambo Hilo.”

Marejeo

  • +Mwa 22:2; 2Nya 3:1

Mwanzo 22:16

Marejeo

  • +Ebr 6:13, 14
  • +Yoh 3:16; Ro 8:32; Ebr 11:17

Mwanzo 22:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “mbegu.”

  • *

    Tnn., “mbegu.”

  • *

    Au “majiji ya.”

Marejeo

  • +Mwa 13:14, 16; 15:1, 5; Mdo 3:25
  • +Zb 2:8; Da 2:44

Mwanzo 22:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “mbegu yako.”

Marejeo

  • +Mwa 3:15; Ro 9:7; Gal 3:16
  • +Gal 3:8

Mwanzo 22:19

Marejeo

  • +Mwa 21:31

Mwanzo 22:20

Marejeo

  • +Mwa 11:26, 29

Mwanzo 22:22

Marejeo

  • +Mwa 25:20

Mwanzo 22:23

Marejeo

  • +Mwa 24:15; Ro 9:10

Jumla

Mwa. 22:1Ebr 11:17
Mwa. 22:2Yoh 3:16
Mwa. 22:2Mwa 17:19; Yos 24:3; Ro 9:7
Mwa. 22:22Nya 3:1
Mwa. 22:8Yoh 1:29; 1Pe 1:18, 19
Mwa. 22:9Yoh 10:17, 18
Mwa. 22:10Ebr 11:17
Mwa. 22:12Ebr 11:17-19; Yak 2:21
Mwa. 22:14Mwa 22:2; 2Nya 3:1
Mwa. 22:16Ebr 6:13, 14
Mwa. 22:16Yoh 3:16; Ro 8:32; Ebr 11:17
Mwa. 22:17Mwa 13:14, 16; 15:1, 5; Mdo 3:25
Mwa. 22:17Zb 2:8; Da 2:44
Mwa. 22:18Mwa 3:15; Ro 9:7; Gal 3:16
Mwa. 22:18Gal 3:8
Mwa. 22:19Mwa 21:31
Mwa. 22:20Mwa 11:26, 29
Mwa. 22:22Mwa 25:20
Mwa. 22:23Mwa 24:15; Ro 9:10
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Mwanzo 22:1-24

Mwanzo

22 Sasa baada ya mambo hayo Mungu wa kweli akamjaribu+ Abrahamu, akamwambia: “Abrahamu!” akajibu: “Mimi hapa!” 2 Kisha Mungu akamwambia: “Tafadhali, mchukue mwana wako, mwana wako wa pekee unayempenda sana,+ Isaka,+ usafiri kwenda katika nchi ya Moria+ nawe umtoe kuwa dhabihu ya kuteketezwa juu ya mlima mmoja nitakaokuonyesha.”

3 Kwa hiyo Abrahamu akaamka asubuhi na mapema, akaweka matandiko juu ya punda wake na kuchukua wawili kati ya watumishi wake pamoja na Isaka mwanawe. Akapasua kuni kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa, kisha akafunga safari kwenda mahali ambapo Mungu wa kweli alimwonyesha. 4 Siku ya tatu, Abrahamu aliinua macho, akapaona mahali hapo kwa mbali. 5 Sasa Abrahamu akawaambia watumishi wake: “Ninyi kaeni hapa pamoja na punda, lakini mimi na mvulana huyu tutaenda kule ili kuabudu, halafu tutarudi.”

6 Kwa hiyo Abrahamu akachukua kuni kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa na kumtwika Isaka mwanawe. Halafu akabeba moto na kisu* mikononi, na wote wawili wakaendelea kutembea pamoja. 7 Kisha Isaka akamwambia Abrahamu baba yake: “Baba!” Akajibu: “Naam, mwanangu!” Halafu Isaka akauliza: “Hapa kuna moto na kuni, lakini yuko wapi kondoo kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa?” 8 Abrahamu akajibu: “Mwanangu, Mungu mwenyewe ataandaa kondoo kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa.”+ Na wote wawili wakaendelea kutembea.

9 Mwishowe wakafika mahali ambapo Mungu wa kweli alikuwa amemwonyesha, Abrahamu akajenga madhabahu hapo na kupanga kuni juu yake. Akamfunga Isaka mwanawe mikono na miguu na kumlaza kwenye madhabahu juu ya zile kuni.+ 10 Kisha Abrahamu akaunyoosha mkono wake na kuchukua kisu* ili amuue mwanawe.+ 11 Lakini malaika wa Yehova akamwita kutoka mbinguni: “Abrahamu, Abrahamu!” naye akajibu: “Mimi hapa!” 12 Kisha akasema: “Usimdhuru mvulana huyo, wala usimtendee lolote, kwa maana sasa ninajua kwamba unamwogopa Mungu kwa sababu hukuninyima+ mwana wako, mwana wako wa pekee.” 13 Ndipo Abrahamu akainua macho yake, na hapo karibu mbele yake kulikuwa na kondoo dume aliyenaswa kwa pembe zake kichakani. Kwa hiyo Abrahamu akaenda na kumchukua kondoo dume huyo na kumtoa dhabihu ya kuteketezwa badala ya mwanawe. 14 Naye Abrahamu akapaita mahali hapo Yehova-yire.* Ndiyo sababu mpaka leo inasemwa: “Katika mlima wa Yehova itaandaliwa.”+

15 Na malaika wa Yehova akamwita Abrahamu mara ya pili kutoka mbinguni, 16 akamwambia: “‘Naapa kwa nafsi yangu,’ asema Yehova,+ ‘kwamba kwa kuwa umetenda jambo hili nawe hujaninyima mwana wako, mwana wako wa pekee,+ 17 hakika nitakubariki, nami hakika nitaufanya uzao* wako uwe mwingi kama nyota za mbinguni na kama chembe za mchanga kwenye ufuo wa bahari,+ na uzao* wako utamiliki lango la* maadui wake.+ 18 Na kupitia uzao wako*+ mataifa yote ya dunia yatajipatia baraka kwa sababu umeisikiliza sauti yangu.’”+

19 Baada ya hayo Abrahamu akarudi kwa watumishi wake, wakaondoka wote pamoja na kurudi Beer-sheba;+ na Abrahamu akaendelea kuishi Beer-sheba.

20 Baadaye Abrahamu akaambiwa: “Tazama, Milka amemzalia pia Nahori ndugu yako+ wana hawa: 21 Usi mzaliwa wake wa kwanza, Buzi ndugu yake, Kemueli baba ya Aramu, 22 Kesedi, Hazo, Pildashi, Yidlafu, na Bethueli.”+ 23 Bethueli akamzaa Rebeka.+ Milka alimzalia Nahori ndugu ya Abrahamu wana hao wanane. 24 Suria wake, aliyeitwa Reuma, alimzalia pia wana hawa: Teba, Gahamu, Tahashi, na Maaka.

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki