Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ayubu 10
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Ayubu—Yaliyomo

      • Ayubu aendelea kujibu (1-22)

        • ‘Kwa nini Mungu anapambana nami?’ (2)

        • Mungu si kama Ayubu anayeweza kufa (4-12)

        • ‘Naomba nipate kitulizo kidogo’ (20)

Ayubu 10:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Nafsi yangu inachukia sana.”

  • *

    Au “kwa uchungu mwingi sana wa nafsi yangu!”

Marejeo

  • +Hes 11:11, 15; 1Fa 19:3, 4; Ayu 7:16; Yon 4:3

Ayubu 10:3

Marejeo

  • +Ayu 14:15; Zb 138:8; Isa 64:8

Ayubu 10:5

Marejeo

  • +Zb 90:2

Ayubu 10:6

Marejeo

  • +Ayu 10:14

Ayubu 10:7

Marejeo

  • +Ayu 1:8; Zb 139:1
  • +Kum 32:39

Ayubu 10:8

Marejeo

  • +Zb 119:73; 139:13-16

Ayubu 10:9

Marejeo

  • +Mwa 2:7; Isa 45:9; 64:8; Ro 9:21
  • +Mwa 3:19; Zb 104:29; Mhu 12:7

Ayubu 10:11

Marejeo

  • +Zb 139:15

Ayubu 10:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “pumzi yangu; uhai wangu.”

Marejeo

  • +Zb 8:4

Ayubu 10:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Na mambo haya umeyaficha moyoni mwako.”

Ayubu 10:14

Marejeo

  • +Zb 139:1

Ayubu 10:15

Marejeo

  • +Ayu 9:15
  • +Zb 119:153

Ayubu 10:16

Marejeo

  • +Isa 38:13

Ayubu 10:18

Marejeo

  • +Ayu 3:11; Yer 20:18

Ayubu 10:20

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nichangamke kidogo.”

Marejeo

  • +Ayu 7:6; 14:1, 2; Zb 39:5, 6; 103:15, 16
  • +Ayu 9:27

Ayubu 10:21

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “yenye giza na kivuli cha kifo.”

Marejeo

  • +Ayu 7:9; Zb 115:17; Isa 38:11
  • +Ayu 38:17; Zb 88:12; Mhu 9:10

Jumla

Ayu. 10:1Hes 11:11, 15; 1Fa 19:3, 4; Ayu 7:16; Yon 4:3
Ayu. 10:3Ayu 14:15; Zb 138:8; Isa 64:8
Ayu. 10:5Zb 90:2
Ayu. 10:6Ayu 10:14
Ayu. 10:7Ayu 1:8; Zb 139:1
Ayu. 10:7Kum 32:39
Ayu. 10:8Zb 119:73; 139:13-16
Ayu. 10:9Mwa 2:7; Isa 45:9; 64:8; Ro 9:21
Ayu. 10:9Mwa 3:19; Zb 104:29; Mhu 12:7
Ayu. 10:11Zb 139:15
Ayu. 10:12Zb 8:4
Ayu. 10:14Zb 139:1
Ayu. 10:15Ayu 9:15
Ayu. 10:15Zb 119:153
Ayu. 10:16Isa 38:13
Ayu. 10:18Ayu 3:11; Yer 20:18
Ayu. 10:20Ayu 7:6; 14:1, 2; Zb 39:5, 6; 103:15, 16
Ayu. 10:20Ayu 9:27
Ayu. 10:21Ayu 7:9; Zb 115:17; Isa 38:11
Ayu. 10:21Ayu 38:17; Zb 88:12; Mhu 9:10
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Ayubu 10:1-22

Ayubu

10 “Nayachukia sana* maisha yangu.+

Nitamwaga malalamiko yangu.

Nitasema waziwazi katika mateso yangu makali!*

 2 Nitamwambia Mungu: ‘Usinitangaze kuwa mwenye hatia.

Niambie kwa nini unapambana nami.

 3 Je, unafaidika unaponikandamiza,

Unapodharau kazi ya mikono yako+

Huku ukipendelea ushauri wa waovu?

 4 Je, una macho ya kimwili,

Au je, unaona kama mwanadamu anayeweza kufa anavyoona?

 5 Je, siku zako ni kama siku za wanadamu wanaoweza kufa,

Au je, miaka yako ni kama ya mwanadamu,+

 6 Hivi kwamba utafute kosa langu

Na kuendelea kutafuta dhambi yangu?+

 7 Unajua kwamba sina hatia;+

Na hakuna yeyote anayeweza kuniokoa kutoka mkononi mwako.+

 8 Mikono yako mwenyewe ilinifinyanga na kuniumba,+

Lakini sasa unataka kuniangamiza kabisa.

 9 Tafadhali, kumbuka kwamba uliniumba kwa udongo,+

Lakini sasa unanirudisha mavumbini.+

10 Je, hukunimwaga kama maziwa

Na kunigandisha kama jibini?

11 Ulinivisha ngozi na nyama,

Na kunifuma kwa mifupa na misuli.+

12 Umenipa uhai na kunipenda kwa ushikamanifu;

Umeilinda na kuitunza roho yangu.*+

13 Lakini ulikusudia kwa siri kufanya mambo haya.*

Najua kwamba mambo haya yametoka kwako.

14 Ikiwa ningetenda dhambi, ungenitazama,+

Nawe hungenisamehe kosa langu.

15 Kama nina hatia, ole wangu!

Na hata kama sina hatia, siwezi kuinua kichwa changu,+

Kwa sababu nimejaa aibu na mateso.+

16 Nikiinua kichwa changu juu, unaniwinda kama simba+

Na kuonyesha tena nguvu zako dhidi yangu.

17 Unaleta mashahidi wapya dhidi yangu

Na kuzidisha hasira yako dhidi yangu,

Huku shida baada ya shida ikinikabili.

18 Basi kwa nini ulinitoa katika tumbo la mama yangu?+

Laiti ningekufa kabla ya jicho lolote kuniona.

19 Ingekuwa kana kwamba sikuwahi kuwepo;

Ningetolewa moja kwa moja tumboni na kupelekwa kaburini.’

20 Je, siku zangu si chache?+ Naomba aniache;

Na ayageuze macho yake mbali nami, ili nipate kitulizo kidogo*+

21 Kabla sijaenda zangu—nami sitarudi+—

Katika nchi yenye giza zito kabisa,*+

22 Kwenye nchi yenye giza totoro,

Nchi ya kivuli kizito na vurugu,

Ambako hata nuru ni kama giza.”

Tanzanian sign language publications (2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki