Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ayubu 11
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Ayubu—Yaliyomo

      • Sofari azungumza kwa mara ya kwanza (1-20)

        • Amshutumu Ayubu kwa sababu ya maneno yake yasiyo na maana (2, 3)

        • Amwambia Ayubu aache uovu (14)

Ayubu 11:1

Marejeo

  • +Ayu 20:1; 42:9

Ayubu 11:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mwenye kujigamba atakuwa bila kosa?”

Ayubu 11:3

Marejeo

  • +Ayu 12:4

Ayubu 11:4

Marejeo

  • +Ayu 6:10
  • +Ayu 6:29; 10:7

Ayubu 11:5

Marejeo

  • +Ayu 38:1

Ayubu 11:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mipaka ya.”

Ayubu 11:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.

Ayubu 11:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Wakati tu punda mwitu atakapozaliwa akiwa mwanadamu.”

Ayubu 11:20

Marejeo

  • +Ayu 8:13, 14; 18:5, 14

Jumla

Ayu. 11:1Ayu 20:1; 42:9
Ayu. 11:3Ayu 12:4
Ayu. 11:4Ayu 6:10
Ayu. 11:4Ayu 6:29; 10:7
Ayu. 11:5Ayu 38:1
Ayu. 11:20Ayu 8:13, 14; 18:5, 14
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Ayubu 11:1-20

Ayubu

11 Sofari+ Mnaamathi akajibu:

 2 “Je, maneno haya yote yatakosa kujibiwa,

Au kuongea mengi kutamfanya mtu asiwe na kosa?*

 3 Je, maneno yako yasiyo na maana yatawanyamazisha watu?

Unadhani hakuna atakayekukemea kwa sababu ya maneno yako ya dhihaka?+

 4 Kwa sababu unasema, ‘Mafundisho yangu ni safi,+

Nami niko safi machoni pako.’+

 5 Lakini laiti Mungu angezungumza

Na kukufungulia midomo yake!+

 6 Ndipo angekufunulia siri za hekima,

Kwa maana hekima inayotumika ina vipengele vingi.

Kisha ungetambua kwamba Mungu huruhusu baadhi ya makosa yako yasahauliwe.

 7 Je, unaweza kugundua mambo ya Mungu yenye kina

Au kugundua kila jambo kumhusu* Mweza-Yote?

 8 Hekima yake iko juu kuliko mbingu. Wewe unaweza kutimiza nini?

Ina kina kuliko Kaburi.* Wewe unaweza kujua nini?

 9 Ni ndefu kuliko dunia

Na pana kuliko bahari.

10 Akipita na kumkamata mtu na kuweka kikao cha mahakama,

Ni nani anayeweza kumpinga?

11 Kwa maana anajua watu wanapokuwa wadanganyifu.

Akiona uovu, je, hatautambua?

12 Lakini mtu asiye na akili ataelewa

Wakati tu punda mwitu atakapoweza kuzaa mwanadamu.*

13 Laiti ungeutayarisha moyo wako

Na kumnyooshea mikono yako.

14 Ikiwa mkono wako unatenda mabaya, utupilie mbali,

Nawe usiruhusu uovu ukae katika mahema yako.

15 Ndipo utakapoinua uso wako bila lawama;

Utaweza kusimama imara, bila woga.

16 Ndipo utakapoisahau taabu yako;

Utaikumbuka kama maji yaliyopita karibu nawe na kwenda zake.

17 Maisha yako yatang’aa kuliko adhuhuri;

Hata giza lake litakuwa kama asubuhi.

18 Utakuwa na ujasiri kwa sababu kuna tumaini,

Nawe utatazama huku na huku na kulala kwa usalama.

19 Utalala na hakuna yeyote atakayekuogopesha,

Na watu wengi watajipendekeza kwako.

20 Lakini macho ya waovu yatadhoofika;

Nao hawatapata mahali pa kukimbilia,

Na tumaini lao pekee litakuwa kifo.”+

Tanzanian sign language publications (2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki