Zaburi
Wimbo wa Safari za Kupanda. Wa Daudi.
124 “Kama Yehova hangekuwa pamoja nasi”+
—Watu wa Israeli na waseme sasa—
2 “Kama Yehova hangekuwa pamoja nasi+
Watu walipokuja kutushambulia,+
3 Basi wangetumeza tukiwa hai+
Hasira yao ilipokuwa ikiwaka dhidi yetu.+
4 Kisha maji yangetufagilia mbali,
Mafuriko yangetufunika.+
5 Maji yenye nguvu yangetulemea.
6 Yehova na asifiwe,
Kwa maana hakututia katika meno yao kama mawindo.
7 Sisi* ni kama ndege aliyeponyoka
Kutoka katika mtego wa mwindaji;+
Mtego ulivunjika,
Nasi tukaponyoka.+
8 Msaada wetu uko katika jina la Yehova,+
Muumba wa mbingu na dunia.”