Methali
4 Yehova amefanya kila kitu kitimize kusudi lake,
Hata waovu kwa ajili ya siku ya msiba.+
5 Kila mtu mwenye kiburi moyoni humchukiza Yehova.+
Uwe na hakika kwamba* hatakosa kuadhibiwa.
6 Kwa upendo mshikamanifu na uaminifu, kosa husamehewa,+
Na kwa kumwogopa Yehova mtu hujiepusha na uovu.+
7 Yehova anapofurahia njia za mtu,
Huwafanya hata maadui wake wawe na amani naye.+
9 Mtu anaweza kupanga njia yake moyoni mwake,
Lakini Yehova ndiye anayezielekeza hatua zake.+
11 Mizani na vipimo vya unyoofu hutoka kwa Yehova;
Mawe yote ya kupimia yaliyo katika mfuko ni kazi yake.+
13 Maneno ya uadilifu huwafurahisha wafalme.
Wanampenda mtu anayeongea kwa unyoofu.+
15 Katika nuru ya uso wa mfalme kuna uzima;
Kibali chake ni kama wingu la mvua wakati wa masika.+
16 Jinsi lilivyo jambo bora kupata hekima kuliko dhahabu!+
Ni bora kuchagua uelewaji kuliko fedha.+
17 Barabara kuu ya wanyoofu huepuka uovu.
Yeyote anayelinda njia yake huhifadhi uhai wake.*+
18 Kiburi hutangulia kuanguka kwa kishindo,
Na roho ya majivuno hutangulia kujikwaa.+
20 Mtu anayeonyesha ufahamu katika jambo atapata mafanikio,*
Na mwenye furaha ni yule anayemtumaini Yehova.
21 Watu wenye hekima moyoni wataitwa watu wenye uelewaji,+
22 Ufahamu ni chemchemi ya uzima kwa walio nao,
Lakini wajinga hutiwa nidhamu kwa ujinga wao wenyewe.
23 Moyo wa mwenye hekima hukipatia kinywa chake ufahamu+
Na huongeza ushawishi kwenye maneno yake.
25 Kuna njia inayoonekana kuwa sawa machoni pa mtu,
Lakini mwishowe inaongoza kwenye kifo.+
26 Hamu ya chakula* ya mfanyakazi humfanya afanye kazi kwa bidii
29 Mtu mkatili humshawishi jirani yake
Na kumwongoza katika njia isiyofaa.
30 Hukonyeza jicho lake anapopanga njama zinazodhuru.
Huibanabana midomo yake pamoja anapotekeleza hila.