Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yeremia 18
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Yeremia—Yaliyomo

      • Udongo mikononi mwa mfinyanzi (1-12)

      • Yehova awageuzia Israeli mgongo (13-17)

      • Njama dhidi ya Yeremia; ombi lake (18-23)

Yeremia 18:2

Marejeo

  • +Yer 19:1

Yeremia 18:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kama ilivyokuwa sawa machoni pa mfinyanzi kukitengeneza.”

Yeremia 18:6

Marejeo

  • +Ro 9:20, 21

Yeremia 18:7

Marejeo

  • +Yer 1:10; 12:14; 25:9; 45:4

Yeremia 18:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nitaghairi.”

Marejeo

  • +1Fa 8:33, 34; Zb 106:45; Yer 7:3; 26:3; Eze 18:21; Yoe 2:13; Yon 3:5, 10

Yeremia 18:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nitaghairi.”

Yeremia 18:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “ninatengeneza.”

Marejeo

  • +Isa 1:16; Eze 18:23

Yeremia 18:12

Marejeo

  • +Yer 2:25
  • +Kum 29:19, 20; Yer 7:24

Yeremia 18:13

Marejeo

  • +Yer 2:13

Yeremia 18:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “moshi wa dhabihu.”

  • *

    Au “ambazo hazijatengenezwa.”

Marejeo

  • +Yer 2:19; 3:21
  • +Yer 10:14, 15
  • +Yer 6:16

Yeremia 18:16

Marejeo

  • +Law 26:33; Eze 6:14
  • +1Fa 9:8; Yer 19:8; Omb 2:15; Mik 6:16
  • +Kum 28:37

Yeremia 18:17

Marejeo

  • +Kum 31:17

Yeremia 18:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mafundisho hayatatoweka.”

  • *

    Tnn., “tumpige kwa ulimi.”

Marejeo

  • +Yer 11:19

Yeremia 18:20

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “wameichimbia shimo nafsi yangu.”

Marejeo

  • +Zb 35:7

Yeremia 18:21

Marejeo

  • +Yer 12:3
  • +Omb 5:3
  • +2Nya 36:17

Yeremia 18:22

Marejeo

  • +Zb 38:12

Yeremia 18:23

Marejeo

  • +Yer 11:19, 20
  • +Zb 35:4
  • +Yer 15:15

Jumla

Yer. 18:2Yer 19:1
Yer. 18:6Ro 9:20, 21
Yer. 18:7Yer 1:10; 12:14; 25:9; 45:4
Yer. 18:81Fa 8:33, 34; Zb 106:45; Yer 7:3; 26:3; Eze 18:21; Yoe 2:13; Yon 3:5, 10
Yer. 18:11Isa 1:16; Eze 18:23
Yer. 18:12Yer 2:25
Yer. 18:12Kum 29:19, 20; Yer 7:24
Yer. 18:13Yer 2:13
Yer. 18:15Yer 2:19; 3:21
Yer. 18:15Yer 10:14, 15
Yer. 18:15Yer 6:16
Yer. 18:16Law 26:33; Eze 6:14
Yer. 18:161Fa 9:8; Yer 19:8; Omb 2:15; Mik 6:16
Yer. 18:16Kum 28:37
Yer. 18:17Kum 31:17
Yer. 18:18Yer 11:19
Yer. 18:20Zb 35:7
Yer. 18:21Yer 12:3
Yer. 18:21Omb 5:3
Yer. 18:212Nya 36:17
Yer. 18:22Zb 38:12
Yer. 18:23Yer 11:19, 20
Yer. 18:23Zb 35:4
Yer. 18:23Yer 15:15
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Yeremia 18:1-23

Yeremia

18 Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Yehova: 2 “Inuka na ushuke mpaka kwenye nyumba ya mfinyanzi,+ na huko nitakuambia maneno yangu.”

3 Basi nikashuka mpaka kwenye nyumba ya mfinyanzi, naye alikuwa akifanya kazi kwenye magurudumu ya mfinyanzi. 4 Lakini chombo alichokuwa akitengeneza kikaharibika mikononi mwake. Basi mfinyanzi akakitengeneza upya kuwa chombo kingine, kama alivyopenda.*

5 Kisha neno la Yehova likanijia likisema: 6 “‘Je, siwezi kuwatendea kama mfinyanzi huyu alivyotenda, enyi watu wa nyumba ya Israeli?’ asema Yehova. ‘Tazama! Kama udongo mikononi mwa mfinyanzi, ndivyo mlivyo mikononi mwangu, enyi watu wa nyumba ya Israeli.+ 7 Wakati wowote nitakaposema kuhusu kung’oa na kubomoa na kuharibu taifa au ufalme,+ 8 na taifa hilo liache uovu wake niliotangaza dhidi yake, mimi pia nitabadili nia yangu* kuhusu msiba niliokusudia kuuleta dhidi yake.+ 9 Lakini wakati wowote ninaposema kuhusu kujenga na kupanda taifa au ufalme, 10 na taifa hilo litende maovu machoni pangu na kukosa kuitii sauti yangu, mimi pia nitabadili nia yangu* kuhusu mema niliyokusudia kulitendea.’

11 “Sasa, tafadhali, waambie watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalemu, ‘Yehova anasema hivi: “Ninatayarisha* msiba na kupanga njama dhidi yenu. Geukeni, tafadhali, kutoka kwenye njia zenu mbaya, na mrekebishe njia zenu na matendo yenu.”’”+

12 Lakini wakasema: “Hakuna tumaini lolote!+ Kwa maana tutafuata mawazo yetu wenyewe, na kila mmoja wetu atatenda kulingana na ukaidi wa moyo wake mwovu.”+

13 Kwa hiyo Yehova anasema hivi:

“Ulizeni wenyewe, tafadhali, kati ya mataifa.

Ni nani amesikia jambo kama hili?

Bikira wa Israeli ametenda jambo linalochukiza sana.+

14 Je, theluji ya Lebanoni inatoweka kwenye miamba iliyo kwenye miteremko yake?

Au, je, maji baridi yanayotiririka kutoka mbali yatakauka?

15 Lakini watu wangu wamenisahau.+

Kwa maana wanakitolea dhabihu* kitu cha ubatili,+

Nao wanawafanya watu wajikwae katika njia zao, vijia vya kale,+

Ili wapite kwenye barabara za vichochoroni ambazo hazijasawazishwa na ambazo si tambarare,*

16 Ili kuifanya nchi yao kuwa kitu cha kutisha+

Na kitu cha kupigiwa mluzi milele.+

Kila mtu atakayepita kando yake atatazama kwa mshtuko na kutikisa kichwa chake.+

17 Kama upepo wa mashariki, nitawatawanya mbele ya adui.

Nitawaonyesha mgongo, si uso wangu, siku ya msiba wao.”+

18 Nao wakasema: “Njooni, tupange njama dhidi ya Yeremia,+ kwa maana sheria haitatoweka* kutoka kwa makuhani wetu au shauri kutoka kwa watu wenye hekima au neno kutoka kwa manabii. Njooni tumshambulie kwa maneno,* nasi tusisikilize anachosema.”

19 Nitegee sikio, Ee Yehova,

Nawe usikilize wanachosema wapinzani wangu.

20 Je, wema unapaswa kulipwa kwa uovu?

Kwa maana wameuchimbia shimo uhai wangu.*+

Kumbuka jinsi nilivyosimama mbele zako ili kusema mema kuwahusu,

Ili kuwaondolea ghadhabu yako.

21 Basi waache wana wao wapatwe na njaa kali,

Na uwatie mikononi mwa nguvu za upanga.+

Wake zao na wafiwe na watoto na kuwa wajane.+

Wanaume wao na wauawe kwa ugonjwa unaoua,

Vijana wao wauawe kwa upanga vitani.+

22 Kilio na kisikiwe kutoka katika nyumba zao

Utakapowaletea wavamizi kwa ghafla.

Kwa maana wamechimba shimo ili kunikamata

Nao wametega mitego ya kuinasa miguu yangu.+

23 Lakini wewe, Ee Yehova,

Unajua vema njama zao zote za kuniua.+

Usilifunike kosa lao,

Wala usiifute dhambi yao kutoka mbele zako.

Na wakwazike mbele zako+

Utakapowachukulia hatua kwa hasira yako.+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki