Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ezekieli 14
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Ezekieli—Yaliyomo

      • Wanaoabudu sanamu washutumiwa (1-11)

      • Hukumu dhidi ya Yerusalemu haiwezi kuepukika (12-23)

        • Noa, Danieli, na Ayubu waliokuwa waadilifu (14, 20)

Ezekieli 14:1

Marejeo

  • +Eze 33:30, 31

Ezekieli 14:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Huenda neno la Kiebrania linahusiana na neno “mavi,” nalo hutumiwa kuonyesha dharau.

Marejeo

  • +2Fa 3:13; Isa 1:15; Yer 11:11

Ezekieli 14:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “nitawakamata watu wa nyumba ya Israeli katika moyo wao.”

Marejeo

  • +Yer 2:5

Ezekieli 14:6

Marejeo

  • +Isa 55:7

Ezekieli 14:7

Marejeo

  • +Yer 21:1, 2; Eze 33:31

Ezekieli 14:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Nitaukaza uso wangu dhidi ya.”

Marejeo

  • +Law 20:2, 3

Ezekieli 14:9

Marejeo

  • +1Fa 22:21, 22; Yer 4:10; 2Th 2:10, 11

Ezekieli 14:11

Marejeo

  • +Yer 24:7; Eze 11:19, 20

Ezekieli 14:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “kuvunja fito zake za mikate.” Labda ni fito zilizotumiwa kuhifadhia mikate.

Marejeo

  • +Law 26:26
  • +Isa 3:1; Yer 15:2
  • +Yer 7:20

Ezekieli 14:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “wangeokoa nafsi zao.”

Marejeo

  • +Mwa 6:8, 9; Ebr 11:7
  • +Da 10:11
  • +Ayu 1:8; 42:8
  • +Met 11:4; Yer 15:1; 2Pe 2:9

Ezekieli 14:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “na kuwaua watoto.”

Marejeo

  • +Law 26:22; Yer 15:3

Ezekieli 14:17

Marejeo

  • +Law 26:25; Yer 25:9; Eze 21:3
  • +Sef 1:3

Ezekieli 14:19

Marejeo

  • +Kum 28:21, 22

Ezekieli 14:20

Marejeo

  • +Mwa 7:1
  • +Da 10:11
  • +Ayu 1:8; 42:8
  • +Eze 18:20; Sef 2:3

Ezekieli 14:21

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “matendo yangu manne ya hukumu yanayodhuru.”

Marejeo

  • +Yer 15:2
  • +Eze 5:17; 33:27
  • +Yer 32:43

Ezekieli 14:22

Marejeo

  • +Kum 4:31; 2Nya 36:20; Eze 6:8; Mik 5:7

Ezekieli 14:23

Marejeo

  • +Ne 9:33; Yer 22:8, 9; Eze 9:9; Da 9:7

Jumla

Eze. 14:1Eze 33:30, 31
Eze. 14:32Fa 3:13; Isa 1:15; Yer 11:11
Eze. 14:5Yer 2:5
Eze. 14:6Isa 55:7
Eze. 14:7Yer 21:1, 2; Eze 33:31
Eze. 14:8Law 20:2, 3
Eze. 14:91Fa 22:21, 22; Yer 4:10; 2Th 2:10, 11
Eze. 14:11Yer 24:7; Eze 11:19, 20
Eze. 14:13Law 26:26
Eze. 14:13Isa 3:1; Yer 15:2
Eze. 14:13Yer 7:20
Eze. 14:14Mwa 6:8, 9; Ebr 11:7
Eze. 14:14Da 10:11
Eze. 14:14Ayu 1:8; 42:8
Eze. 14:14Met 11:4; Yer 15:1; 2Pe 2:9
Eze. 14:15Law 26:22; Yer 15:3
Eze. 14:17Law 26:25; Yer 25:9; Eze 21:3
Eze. 14:17Sef 1:3
Eze. 14:19Kum 28:21, 22
Eze. 14:20Mwa 7:1
Eze. 14:20Da 10:11
Eze. 14:20Ayu 1:8; 42:8
Eze. 14:20Eze 18:20; Sef 2:3
Eze. 14:21Yer 15:2
Eze. 14:21Eze 5:17; 33:27
Eze. 14:21Yer 32:43
Eze. 14:22Kum 4:31; 2Nya 36:20; Eze 6:8; Mik 5:7
Eze. 14:23Ne 9:33; Yer 22:8, 9; Eze 9:9; Da 9:7
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Ezekieli 14:1-23

Ezekieli

14 Na baadhi ya wazee wa Israeli wakaja na kuketi mbele yangu.+ 2 Kisha neno la Yehova likanijia likisema: 3 “Mwana wa binadamu, wanaume hawa wameazimia kufuata sanamu zao zinazochukiza,* nao wameweka kikwazo kinachowafanya watu watende dhambi. Je, niwaruhusu waniombe ushauri?+ 4 Sasa zungumza nao uwaambie, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Ikiwa Mwisraeli ameazimia kufuata sanamu zake zinazochukiza na kuweka kikwazo kinachowafanya watu watende dhambi kisha anaenda kuomba ushauri kutoka kwa nabii, mimi, Yehova, nitamjibu ipasavyo kulingana na sanamu zake nyingi zinazochukiza. 5 Kwa maana nitatia hofu katika mioyo ya watu wa nyumba ya Israeli* kwa sababu wote wameniacha na kuzifuata sanamu zao zinazochukiza.”’+

6 “Basi waambie watu wa nyumba ya Israeli, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: “Rudini na mziache sanamu zenu zinazochukiza na mgeuze nyuso zenu kutoka kwenye mazoea yenu yanayochukiza.+ 7 Kwa maana ikiwa Mwisraeli yeyote au mgeni anayeishi Israeli anajitenga nami na kuazimia kufuata sanamu zake zinazochukiza na kuweka kikwazo kinachowafanya watu watende dhambi, kisha aje kuomba ushauri kutoka kwa nabii wangu,+ mimi, Yehova, nitamjibu mimi mwenyewe. 8 Nitamkataa* mtu huyo na kumfanya awe ishara ya kuonya na methali, nami nitamwangamiza kabisa kutoka kati ya watu wangu;+ nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.”’

9 “‘Lakini nabii akipumbazwa naye atoe ushauri, ni mimi, Yehova, ambaye nimempumbaza nabii huyo.+ Ndipo nitakapounyoosha mkono wangu dhidi yake na kumwangamiza kutoka kwa watu wangu Waisraeli. 10 Nao lazima wataibeba hatia yao; hatia ya mwenye kuomba ushauri itakuwa sawa na hatia ya nabii, 11 ili watu wa nyumba ya Israeli waache kutangatanga mbali nami na kuacha kujichafua kwa makosa yao yote. Nao watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”

12 Na neno la Yehova likanijia tena likisema: 13 “Mwana wa binadamu, ikiwa nchi itanitendea dhambi kwa kukosa uaminifu, nitaunyoosha mkono wangu dhidi yake na kufanya chakula kisipatikane*+ na kuleta njaa kali nchini+ na kuwaangamiza kabisa wanadamu na wanyama kutoka humo.”+ 14 “‘Hata ikiwa watu hawa watatu—Noa,+ Danieli,+ na Ayubu+—wangekuwa humo, wangejiokoa wao wenyewe* tu kwa sababu ya uadilifu wao,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”

15 “‘Au nikifanya wanyama hatari wa mwituni wapite kotekote nchini na kuwaua watu wengi* na kuifanya nchi iwe ukiwa hivi kwamba hakuna mtu atakayepita humo kwa sababu ya wanyama wa mwituni,+ 16 kama ninavyoishi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘hata ikiwa watu hao watatu wangekuwa humo, hawangewaokoa wana wao wala mabinti wao; wangejiokoa wao wenyewe tu, na nchi ingekuwa ukiwa.’”

17 “‘Au kama nikileta upanga dhidi ya nchi hiyo+ na kusema: “Upanga na upite kotekote nchini,” na kuwaangamiza wanadamu na wanyama kutoka humo,+ 18 hata ikiwa watu hao watatu wangekuwa humo, kwa hakika kama ninavyoishi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘hawangewaokoa wana wao wala mabinti wao; wangejiokoa wao wenyewe tu.’”

19 “‘Au nikileta ugonjwa hatari katika nchi hiyo+ na kuimwagia ghadhabu yangu kwa umwagaji wa damu ili kuwaangamiza wanadamu na wanyama kutoka humo, 20 hata ikiwa Noa,+ Danieli,+ na Ayubu+ wangekuwa humo, kwa hakika kama ninavyoishi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘hawangewaokoa wana wao wala mabinti wao; wangejiokoa wao wenyewe tu kwa sababu ya uadilifu wao.’”+

21 “Kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Ndivyo itakavyokuwa nitakapoleta adhabu zangu nne*+—upanga, njaa kali, wanyama hatari wa mwituni, na ugonjwa hatari+—dhidi ya jiji la Yerusalemu ili kuwaangamiza kabisa wanadamu na wanyama kutoka humo.+ 22 Lakini, baadhi ya watu waliobaki humo wataponyoka na kutolewa nje,+ wana na mabinti. Wanakuja kwenu, nanyi mtakapoona njia zao na matendo yao, kwa hakika mtafarijiwa kuhusiana na msiba ambao nilileta dhidi ya Yerusalemu, kuhusu kila jambo ambalo nilitenda dhidi ya jiji hilo.’”

23 “‘Watawafariji mtakapoona njia zao na matendo yao, nanyi mtajua kwamba sikutenda bila sababu yale niliyolazimika kulitendea jiji hilo,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki