-
Kutoka 7:5Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
5 Na Wamisri watajua kwa hakika kwamba mimi ni Yehova+ nitakapounyoosha mkono wangu dhidi ya Misri na kuwatoa Waisraeli miongoni mwao.”
-
-
Kutoka 7:17Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
17 Yehova anasema hivi: “Kwa jambo hili utajua kwamba mimi ni Yehova.+ Tazama ninayapiga maji ya Mto Nile kwa fimbo hii iliyo mkononi mwangu, nayo yatabadilika na kuwa damu.
-
-
Kutoka 8:9, 10Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
9 Kisha Musa akamwambia Farao: “Kwa heshima yako niambie wakati unaotaka nimwombe Mungu awaondoe vyura kutoka kwako, kutoka kwa watumishi wako, kutoka kwa watu wako, na kutoka katika nyumba zenu. Watabaki katika Mto Nile tu.” 10 Farao akamwambia: “Kesho.” Basi Musa akasema: “Itakuwa kama unavyosema, ili ujue kwamba hakuna yeyote aliye kama Yehova Mungu wetu.+
-
-
Zaburi 24:1Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
-
-
24 Dunia na vyote vilivyomo ni vya Yehova,+
Nchi inayozaa na wale wanaokaa ndani yake.
-