Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo ya Walawi 14:49-53
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 49 Ili kuitakasa nyumba hiyo isiyo safi,* atachukua ndege wawili, tawi la mwerezi, kitambaa cha rangi nyekundu, na tawi la hisopo.+ 50 Atamchinjia ndege mmoja kwenye chombo cha udongo chenye maji ya kijito. 51 Kisha atamchukua ndege aliye hai na kumtumbukiza pamoja na tawi la mwerezi, kitambaa cha rangi nyekundu, na tawi la hisopo ndani ya damu ya ndege aliyechinjiwa kwenye maji ya kijito, naye atainyunyiza kuelekea nyumba hiyo mara saba.+ 52 Naye ataitakasa nyumba hiyo isiyo safi* kwa kutumia damu ya ndege huyo, maji ya kijito, yule ndege aliye hai, tawi la mwerezi, tawi la hisopo, na kitambaa cha rangi nyekundu. 53 Kisha atamwachilia ndege aliye hai aende zake mashambani nje ya jiji, naye ataitolea nyumba hiyo dhabihu ya kufunika dhambi, nayo itakuwa safi.

  • Hesabu 19:6
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 6 Halafu kuhani atachukua tawi la mwerezi, tawi la hisopo,+ na kitambaa chekundu na kutupa vitu hivyo katika moto unaomteketeza ng’ombe huyo.

  • Hesabu 19:9
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    • 9 “‘Mtu aliye safi atayakusanya majivu ya ng’ombe huyo+ na kuyapeleka mahali safi nje ya kambi, yatahifadhiwa na Waisraeli ili yatumiwe kutengenezea maji ya kutakasa.+ Ni dhabihu ya dhambi.

  • Zaburi 51:7
    Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
    •  7 Nisafishe kutoka katika dhambi yangu kwa hisopo, ili niwe safi;+

      Nioshe, ili niwe mweupe kuliko theluji.+

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki