Zaburi
3 Jivunieni jina lake takatifu.+
Mioyo ya wale wanaomtafuta Yehova na ishangilie.+
4 Mtafuteni Yehova+ na nguvu zake.
Utafuteni uso* wake daima.
5 Kumbukeni kazi zinazostaajabisha alizofanya,
Miujiza yake na hukumu alizotangaza,+
6 Enyi uzao wa* Abrahamu mtumishi wake,+
Enyi wana wa Yakobo, watu wake aliowachagua.+
7 Yeye ni Yehova Mungu wetu.+
Hukumu zake ziko duniani kote.+
8 Anakumbuka agano lake milele,+
Ahadi aliyotoa,* hata kufikia vizazi elfu,+
9 Agano alilofanya na Abrahamu,+
Na kiapo alichomwapia Isaka,+
10 Alichotoa kama amri kwa Yakobo
Na kama agano la kudumu kwa Israeli,
11 Akisema, “Nitakupa nchi ya Kanaani+
Kuwa urithi wako uliogawiwa.”+
13 Walitembeatembea kutoka taifa moja hadi taifa lingine,
Kutoka ufalme mmoja hadi ufalme mwingine.+
14 Hakumruhusu mtu yeyote awakandamize,+
Lakini kwa sababu yao aliwakaripia wafalme,+
15 Akisema, “Msiwaguse watiwa-mafuta wangu,
Wala msiwatendee manabii wangu jambo lolote baya.”+
17 Alimtuma mtu awatangulie
Ambaye aliuzwa kuwa mtumwa, Yosefu.+
18 Waliifunga* miguu yake kwa pingu,+
Shingo yake ilitiwa katika vyuma;*
19 Mpaka wakati ambapo neno lake lilitimia,+
Neno la Yehova ndilo lililomsafisha.
20 Mfalme aliamuru afunguliwe,+
Mtawala wa mataifa akamweka huru.
21 Akamweka kuwa bwana mkubwa wa nyumba yake,
Mtawala wa mali zake zote,+
22 Ili awe na mamlaka juu ya* wakuu wake kama alivyopenda*
Na kuwafundisha wazee wake hekima.+
23 Kisha Israeli akaja Misri,+
Na Yakobo akakaa akiwa mgeni katika nchi ya Hamu.
24 Mungu aliwafanya watu wake waongezeke sana;+
Aliwafanya wawe na nguvu kuliko maadui wao,+
25 Akaruhusu mioyo yao ibadilike ili wawachukie watu wake,
Ili wapange njama dhidi ya watumishi wake.+
27 Walifanya ishara zake kati yao,
Miujiza yake katika nchi ya Hamu.+
28 Alilituma giza na nchi ikawa giza;+
Hawakuasi maneno yake.
29 Alibadili maji yao yakawa damu
Na kuwaua samaki wao.+
30 Nchi yao ikajaa vyura,+
Hata katika vyumba vya mfalme.
33 Aliipiga mizabibu yao na mitini yao
Na kuivunjavunja miti ya eneo lao.
34 Aliagiza nzige wavamie,
Nzige wachanga wasio na idadi.+
35 Walikula kabisa mimea yote nchini,
Nao wakala kabisa mazao ya ardhi.
36 Kisha akamuua kila mzaliwa wa kwanza katika nchi yao,+
Mwanzo wa nguvu zao za uzazi.
37 Aliwatoa nje watu wake wakiwa na fedha na dhahabu;+
Na hakuna yeyote katika makabila yake aliyejikwaa.
42 Kwa maana aliikumbuka ahadi takatifu aliyompa Abrahamu mtumishi wake.+
43 Kwa hiyo akawatoa watu wake wakishangilia,+
Watu wake aliowachagua aliwatoa kwa kilio cha shangwe.
44 Aliwapa nchi za mataifa;+
Walirithi vitu ambavyo mataifa mengine yalikuwa yametaabika kuvipata,+
45 Ili waweze kutii maagizo yake+
Na kushika sheria zake.
Msifuni Yah!*