Methali
2 Mtumishi mwenye ufahamu atamtawala mwana anayetenda kwa aibu;
Atapokea urithi kama ndugu za mwana huyo.
3 Chungu cha kusafishia ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu,+
Lakini Yehova ndiye mchunguzaji wa mioyo.+
4 Mtu mwovu husikiliza maneno yanayoumiza,
Na mtu mdanganyifu husikiliza ulimi unaodhuru.+
5 Yeyote anayemdhihaki maskini anamtukana Muumba wake,+
Na yeyote anayeshangilia msiba wa mwingine hatakosa kuadhibiwa.+
7 Maneno manyoofu* hayamfai mpumbavu.+
Sembuse maneno ya uwongo kwa mtawala!*+
9 Yeyote anayesamehe* kosa hutafuta upendo,+
Lakini yule anayeendelea kuongea kuhusu jambo huwatenganisha marafiki wa karibu.+
11 Mtu mwovu hutafuta uasi tu,
Lakini mjumbe mkatili atatumwa kumwadhibu.+
12 Ni afadhali kukutana na dubu aliyenyang’anywa watoto wake
Kuliko kukutana na mtu mpumbavu katika ujinga wake.+
13 Mtu yeyote akilipa uovu kwa wema,
Uovu hautaondoka katika nyumba yake.+
15 Yeyote anayetangaza kwamba mwovu hana hatia na yeyote anayemshutumu mwadilifu+
—Wote wawili wanamchukiza Yehova.
17 Rafiki wa kweli hupenda nyakati zote+
Naye ni ndugu ambaye amezaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu.+
19 Mtu anayependa ugomvi anapenda dhambi.+
Yeyote anayeliinua juu lango lake anaalika msiba.+
20 Mtu aliyepotoka moyoni hatapata mafanikio,*+
Na yule anayesema maneno ya udanganyifu ataanguka kwenye maangamizi.
21 Baba anayezaa mtoto mpumbavu atahuzunika;
Na baba ya mtoto asiye na akili hana shangwe.+
24 Hekima iko mbele kabisa ya uso wa mtu mwenye utambuzi,
Lakini macho ya mpumbavu hutangatanga mpaka kwenye miisho ya dunia.+
26 Si vema kumwadhibu* mwadilifu,
Na kuwapiga viboko watu wanaoheshimiwa si jambo linalofaa.
28 Hata mjinga anayekaa kimya ataonwa kuwa mwenye hekima,
Na yule anayefunga midomo yake, ataonwa kuwa mwenye utambuzi.