Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ayubu 38
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Ayubu—Yaliyomo

      • Yehova afundisha kuhusu udogo wa mwanadamu (1-41)

        • ‘Ulikuwa wapi nilipoiumba dunia?’ (4-6)

        • Wana wa Mungu walishangilia kwa sauti (7)

        • Maswali kuhusu matukio ya asili (8-32)

        • “Sheria zinazoongoza mbingu” (33)

Ayubu 38:1

Marejeo

  • +Kut 19:16, 19; 1Fa 19:11

Ayubu 38:2

Marejeo

  • +Ayu 42:3

Ayubu 38:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “jifunge.”

Ayubu 38:4

Marejeo

  • +Mwa 1:1; Ne 9:6; Zb 136:6; Met 8:29; Ebr 1:10

Ayubu 38:6

Marejeo

  • +Zb 104:5

Ayubu 38:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Msemo wa Kiebrania unaorejelea malaika, wana wa Mungu.

Marejeo

  • +Ufu 22:16
  • +Mwa 6:2; 1Fa 22:19; Ayu 1:6; 2:1; Zb 89:6

Ayubu 38:8

Marejeo

  • +Zb 33:7; Met 8:29

Ayubu 38:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kuifungafunga katika.”

Ayubu 38:10

Marejeo

  • +Mwa 1:9; Yer 5:22

Ayubu 38:11

Marejeo

  • +Met 8:29

Ayubu 38:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Je, katika siku zako umeiamuru.”

Marejeo

  • +Mwa 1:5; Zb 74:16

Ayubu 38:13

Marejeo

  • +Ayu 24:15; 1Th 5:7

Ayubu 38:16

Marejeo

  • +Mwa 1:2; Zb 77:19

Ayubu 38:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kivuli cha kifo.”

Marejeo

  • +Zb 9:13; Mt 16:18
  • +Ayu 10:21, 22

Ayubu 38:18

Marejeo

  • +Zb 74:17; 89:11

Ayubu 38:19

Marejeo

  • +Isa 45:7

Ayubu 38:21

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Na idadi ya siku zako ni nyingi?”

Ayubu 38:22

Marejeo

  • +Ayu 37:6
  • +Yos 10:11; Isa 30:30

Ayubu 38:23

Marejeo

  • +Kut 9:24; Eze 13:13

Ayubu 38:24

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “Radi.”

Marejeo

  • +Zb 135:7

Ayubu 38:25

Marejeo

  • +Ayu 28:26

Ayubu 38:26

Marejeo

  • +Zb 104:13; 107:35

Ayubu 38:27

Marejeo

  • +Zb 147:7, 8

Ayubu 38:28

Marejeo

  • +1Sa 12:18; Isa 30:23; Yer 5:24
  • +Mwa 27:28

Ayubu 38:29

Marejeo

  • +Zb 147:16

Ayubu 38:30

Marejeo

  • +Ayu 37:10

Ayubu 38:31

Maelezo ya Chini

  • *

    Labda ni nyota zinazoitwa Pleiadesi katika kundi la nyota la Taurusi, au Ng’ombe.

  • *

    Labda ni kundi la nyota la Orioni.

Marejeo

  • +Amo 5:8

Ayubu 38:32

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Mazarothi.” Kwenye 2Fa 23:5, neno linalohusiana na hilo ambalo liko katika wingi linarejelea makundi ya nyota za unajimu.

  • *

    Labda ni kundi la nyota la Dubu Mkubwa (Kundi Kubwa la Ursa).

Ayubu 38:33

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “mamlaka Yake.”

Marejeo

  • +Met 3:19; Yer 31:35; 33:25

Ayubu 38:34

Marejeo

  • +Zek 10:1

Ayubu 38:36

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “ndani ya mwanadamu.”

  • *

    Au labda, “kuweka uelewaji akilini.”

Marejeo

  • +Yer 10:12
  • +Zb 136:5; Met 3:20

Ayubu 38:37

Marejeo

  • +Yer 10:13

Ayubu 38:39

Marejeo

  • +Zb 104:21; 145:15, 16; Nah 2:12

Ayubu 38:41

Marejeo

  • +Zb 147:9; Mt 6:26; Lu 12:24

Jumla

Ayu. 38:1Kut 19:16, 19; 1Fa 19:11
Ayu. 38:2Ayu 42:3
Ayu. 38:4Mwa 1:1; Ne 9:6; Zb 136:6; Met 8:29; Ebr 1:10
Ayu. 38:6Zb 104:5
Ayu. 38:7Ufu 22:16
Ayu. 38:7Mwa 6:2; 1Fa 22:19; Ayu 1:6; 2:1; Zb 89:6
Ayu. 38:8Zb 33:7; Met 8:29
Ayu. 38:10Mwa 1:9; Yer 5:22
Ayu. 38:11Met 8:29
Ayu. 38:12Mwa 1:5; Zb 74:16
Ayu. 38:13Ayu 24:15; 1Th 5:7
Ayu. 38:16Mwa 1:2; Zb 77:19
Ayu. 38:17Zb 9:13; Mt 16:18
Ayu. 38:17Ayu 10:21, 22
Ayu. 38:18Zb 74:17; 89:11
Ayu. 38:19Isa 45:7
Ayu. 38:22Ayu 37:6
Ayu. 38:22Yos 10:11; Isa 30:30
Ayu. 38:23Kut 9:24; Eze 13:13
Ayu. 38:24Zb 135:7
Ayu. 38:25Ayu 28:26
Ayu. 38:26Zb 104:13; 107:35
Ayu. 38:27Zb 147:7, 8
Ayu. 38:281Sa 12:18; Isa 30:23; Yer 5:24
Ayu. 38:28Mwa 27:28
Ayu. 38:29Zb 147:16
Ayu. 38:30Ayu 37:10
Ayu. 38:31Amo 5:8
Ayu. 38:33Met 3:19; Yer 31:35; 33:25
Ayu. 38:34Zek 10:1
Ayu. 38:36Yer 10:12
Ayu. 38:36Zb 136:5; Met 3:20
Ayu. 38:37Yer 10:13
Ayu. 38:39Zb 104:21; 145:15, 16; Nah 2:12
Ayu. 38:41Zb 147:9; Mt 6:26; Lu 12:24
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
  • 36
  • 37
  • 38
  • 39
  • 40
  • 41
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Ayubu 38:1-41

Ayubu

38 Kisha Yehova akamjibu Ayubu kutoka katika dhoruba ya upepo:+

 2 “Ni nani huyu anayepotosha mashauri yangu

Na kuzungumza bila ujuzi?+

 3 Tafadhali, jitayarishe* kama mwanamume;

Nitakuuliza maswali, nawe unijibu.

 4 Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia?+

Niambie, ikiwa unafikiri unaelewa.

 5 Ni nani aliyeweka vipimo vyake, ikiwa unajua,

Au ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?

 6 Nguzo zake zilizamishwa ndani ya nini,

Au ni nani aliyeweka jiwe lake la pembeni,+

 7 Nyota za asubuhi+ zilipopaza kelele pamoja kwa shangwe,

Na wana wote wa Mungu*+ wakaanza kushangilia kwa sauti?

 8 Na ni nani aliyeizuia bahari nyuma ya milango+

Ilipotoka kwa nguvu katika tumbo la uzazi,

 9 Nilipoivalisha mawingu

Na kuifunika kwa* giza zito,

10 Nilipoiwekea mpaka wangu

Na kuweka makomeo yake na milango yake mahali pake,+

11 Nami nikaiambia, ‘Unaweza kufika hapa, lakini usipite hapa;

Hapa ndipo mawimbi yako ya kifahari yatakapokomea’?+

12 Je, umewahi kuiamuru* asubuhi

Au kuyafanya mapambazuko yajue mahali pake,+

13 Ili yaenee mpaka kwenye miisho ya dunia

Na kuwakung’uta waovu kutoka humo?+

14 Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi utiwapo muhuri,

Na vitu vilivyomo hung’aa kama mapambo ya vazi.

15 Lakini waovu hunyimwa nuru yao,

Na mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.

16 Je, umeshuka chini kwenye chemchemi za bahari

Au kuchunguza vilindi vya maji?+

17 Je, umeonyeshwa malango ya kifo,+

Au umeona malango ya giza zito?*+

18 Je, umeelewa upana mkubwa sana wa dunia?+

Niambie, ikiwa unajua haya yote.

19 Nuru hukaa upande gani?+

Na makao ya giza yako wapi,

20 Ili ulipeleke katika eneo lake

Na kuelewa vijia vinavyoelekea nyumbani kwake?

21 Je, unajua hayo kwa sababu ulikuwa tayari umezaliwa

Na idadi ya miaka yako ni mingi?*

22 Je, umeingia kwenye maghala ya theluji,+

Au umeyaona maghala ya mvua ya mawe,+

23 Ambayo nimeyahifadhi kwa ajili ya wakati wa taabu,

Kwa ajili ya siku ya mapigano na vita?+

24 Nuru* hutawanywa kutoka upande gani,

Na upepo wa mashariki huvuma duniani kutoka wapi?+

25 Ni nani amechimba mtaro kwa ajili ya mafuriko

Na kutengeneza kijia kwa ajili ya mawingu ya dhoruba yenye ngurumo,+

26 Na kuifanya mvua inyeshe mahali ambapo watu hawaishi,

Nyikani ambako hakuna wanadamu,+

27 Ili kutosheleza maeneo yaliyoharibiwa yenye ukiwa

Na kufanya majani yachipuke?+

28 Je, mvua ina baba,+

Au ni nani baba ya matone ya umande?+

29 Barafu ilitoka kwenye tumbo la uzazi la nani,

Na ni nani aliyeizaa theluji ya mbinguni+

30 Maji yanapofunikwa kana kwamba na jiwe,

Na sehemu ya juu ya vilindi vya maji inapoganda kabisa?+

31 Je, unaweza kufunga kamba za kundi la nyota la Kima*

Au kufungua kamba za kundi la nyota la Kesili?*+

32 Je, unaweza kuliongoza nje kundi la nyota* katika majira yake

Au kulielekeza kundi la nyota la Ashi* pamoja na wanawe?

33 Je, unajua sheria zinazoongoza mbingu,+

Au unaweza kutumia mamlaka ya sheria hizo* duniani?

34 Je, unaweza kuinua sauti yako mpaka mawinguni

Ili kusababisha mafuriko ya maji yakufunike?+

35 Je, unaweza kuutuma umeme wa radi?

Je, utakuja na kukwambia, ‘Niko hapa!’?

36 Ni nani aliyeweka hekima mawinguni*+

Au kuyapa uelewaji matukio ya angani?*+

37 Ni nani aliye na hekima ya kutosha kuhesabu mawingu,

Au ni nani anayeweza kuinamisha mitungi ya maji ya mbinguni+

38 Mavumbi yanapomiminika na kugandamana

Na mabonge ya udongo yanaposhikamana?

39 Je, unaweza kumwindia simba mawindo

Au kutosheleza hamu ya chakula ya wanasimba+

40 Wanapojikunyata katika maficho yao

Au wanaponyemelea mapangoni mwao?

41 Ni nani anayemtayarishia chakula kunguru+

Makinda wake wanapomlilia Mungu wakiomba msaada

Na kutangatanga kwa sababu hawana chakula?

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki