Ayubu
38 Kisha Yehova akamjibu Ayubu kutoka katika dhoruba ya upepo:+
2 “Ni nani huyu anayepotosha mashauri yangu
Na kuzungumza bila ujuzi?+
3 Tafadhali, jitayarishe* kama mwanamume;
Nitakuuliza maswali, nawe unijibu.
4 Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia?+
Niambie, ikiwa unafikiri unaelewa.
5 Ni nani aliyeweka vipimo vyake, ikiwa unajua,
Au ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
6 Nguzo zake zilizamishwa ndani ya nini,
Au ni nani aliyeweka jiwe lake la pembeni,+
7 Nyota za asubuhi+ zilipopaza kelele pamoja kwa shangwe,
8 Na ni nani aliyeizuia bahari nyuma ya milango+
Ilipotoka kwa nguvu katika tumbo la uzazi,
9 Nilipoivalisha mawingu
Na kuifunika kwa* giza zito,
10 Nilipoiwekea mpaka wangu
Na kuweka makomeo yake na milango yake mahali pake,+
11 Nami nikaiambia, ‘Unaweza kufika hapa, lakini usipite hapa;
Hapa ndipo mawimbi yako ya kifahari yatakapokomea’?+
12 Je, umewahi kuiamuru* asubuhi
Au kuyafanya mapambazuko yajue mahali pake,+
13 Ili yaenee mpaka kwenye miisho ya dunia
Na kuwakung’uta waovu kutoka humo?+
14 Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi utiwapo muhuri,
Na vitu vilivyomo hung’aa kama mapambo ya vazi.
15 Lakini waovu hunyimwa nuru yao,
Na mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
16 Je, umeshuka chini kwenye chemchemi za bahari
Au kuchunguza vilindi vya maji?+
18 Je, umeelewa upana mkubwa sana wa dunia?+
Niambie, ikiwa unajua haya yote.
19 Nuru hukaa upande gani?+
Na makao ya giza yako wapi,
20 Ili ulipeleke katika eneo lake
Na kuelewa vijia vinavyoelekea nyumbani kwake?
21 Je, unajua hayo kwa sababu ulikuwa tayari umezaliwa
Na idadi ya miaka yako ni mingi?*
22 Je, umeingia kwenye maghala ya theluji,+
Au umeyaona maghala ya mvua ya mawe,+
23 Ambayo nimeyahifadhi kwa ajili ya wakati wa taabu,
Kwa ajili ya siku ya mapigano na vita?+
25 Ni nani amechimba mtaro kwa ajili ya mafuriko
Na kutengeneza kijia kwa ajili ya mawingu ya dhoruba yenye ngurumo,+
26 Na kuifanya mvua inyeshe mahali ambapo watu hawaishi,
Nyikani ambako hakuna wanadamu,+
27 Ili kutosheleza maeneo yaliyoharibiwa yenye ukiwa
Na kufanya majani yachipuke?+
29 Barafu ilitoka kwenye tumbo la uzazi la nani,
Na ni nani aliyeizaa theluji ya mbinguni+
30 Maji yanapofunikwa kana kwamba na jiwe,
Na sehemu ya juu ya vilindi vya maji inapoganda kabisa?+
31 Je, unaweza kufunga kamba za kundi la nyota la Kima*
32 Je, unaweza kuliongoza nje kundi la nyota* katika majira yake
Au kulielekeza kundi la nyota la Ashi* pamoja na wanawe?
34 Je, unaweza kuinua sauti yako mpaka mawinguni
Ili kusababisha mafuriko ya maji yakufunike?+
35 Je, unaweza kuutuma umeme wa radi?
Je, utakuja na kukwambia, ‘Niko hapa!’?
37 Ni nani aliye na hekima ya kutosha kuhesabu mawingu,
Au ni nani anayeweza kuinamisha mitungi ya maji ya mbinguni+
38 Mavumbi yanapomiminika na kugandamana
Na mabonge ya udongo yanaposhikamana?
39 Je, unaweza kumwindia simba mawindo
Au kutosheleza hamu ya chakula ya wanasimba+
40 Wanapojikunyata katika maficho yao
Au wanaponyemelea mapangoni mwao?
41 Ni nani anayemtayarishia chakula kunguru+
Makinda wake wanapomlilia Mungu wakiomba msaada
Na kutangatanga kwa sababu hawana chakula?