Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mathayo 6
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Mathayo—Yaliyomo

      • MAHUBIRI YA MLIMANI (1-34)

        • Msijionyeshe kuwa waadilifu (1-4)

        • Jinsi ya kusali (5-15)

          • Sala ya mfano (9-13)

        • Kufunga (16-18)

        • Hazina duniani na mbinguni (19-24)

        • Acheni kuhangaika (25-34)

          • Endeleeni kuutafuta kwanza Ufalme (33)

Mathayo 6:1

Marejeo

  • +Mt 23:5

Mathayo 6:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “unapowapa maskini zawadi.” Angalia Kamusi.

Mathayo 6:4

Marejeo

  • +Met 19:17; Mt 10:42

Mathayo 6:5

Marejeo

  • +Lu 18:11
  • +Mt 6:16; 23:5

Mathayo 6:6

Marejeo

  • +Lu 6:12

Mathayo 6:8

Marejeo

  • +Lu 12:30

Mathayo 6:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “litukuzwe; lionwe kuwa takatifu.”

Marejeo

  • +Lu 11:2-4
  • +Kut 6:3; Zb 83:18
  • +Eze 36:23

Mathayo 6:10

Marejeo

  • +Da 2:44; Mt 6:33; Ufu 11:15
  • +Mt 26:42; 1Ti 2:4; Ufu 4:11
  • +Zb 37:10; Lu 23:43; Mdo 24:15

Mathayo 6:11

Marejeo

  • +Zb 37:25; Met 30:8; Mt 6:34; 1Ti 6:8

Mathayo 6:12

Marejeo

  • +Mt 18:21; Mk 11:25

Mathayo 6:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “utuokoe.”

Marejeo

  • +Mt 26:41; 1Ko 10:13; Ufu 3:10
  • +Yoh 17:15; 1Yo 5:19

Mathayo 6:14

Marejeo

  • +Efe 4:32; Kol 3:13

Mathayo 6:15

Marejeo

  • +Mt 18:35; Yak 2:13

Mathayo 6:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “hawatunzi sura au mwonekano wao.”

Marejeo

  • +Mdo 13:2, 3; 14:23
  • +Isa 58:5; Lu 18:11, 12

Mathayo 6:19

Maelezo ya Chini

  • *

    Aina ya wadudu.

Marejeo

  • +Mt 13:22; Lu 12:20; Yak 5:3

Mathayo 6:20

Maelezo ya Chini

  • *

    Aina ya wadudu.

Marejeo

  • +Mt 19:21; Mk 10:21; Lu 12:33, 34; 18:22
  • +1Pe 1:3, 4

Mathayo 6:22

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “linaona vizuri.” Tnn., “ni rahisi.”

  • *

    Au “utajawa na nuru.”

Marejeo

  • +Met 4:25; Lu 11:34; Efe 1:18

Mathayo 6:23

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “ni bovu; lina uovu.”

Marejeo

  • +Mt 20:15

Mathayo 6:24

Marejeo

  • +Yak 4:4
  • +Mt 13:22; Lu 16:13

Mathayo 6:25

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nafsi zenu.”

  • *

    Au “nafsi.”

Marejeo

  • +Zb 55:22; Flp 4:6; 1Pe 5:6, 7
  • +1Ti 6:8; Ebr 13:5
  • +Lu 12:22-28

Mathayo 6:26

Marejeo

  • +Ayu 38:41; Zb 147:9; Mt 10:29

Mathayo 6:27

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Nyongeza B14.

Marejeo

  • +Zb 39:5

Mathayo 6:28

Maelezo ya Chini

  • *

    Aina ya maua.

Mathayo 6:29

Marejeo

  • +1Fa 10:4, 5

Mathayo 6:31

Marejeo

  • +Lu 10:41
  • +Lu 12:29-31

Mathayo 6:33

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, uadilifu wa Mungu.

Marejeo

  • +Zb 37:25

Mathayo 6:34

Marejeo

  • +Kut 16:4, 19

Jumla

Mt. 6:1Mt 23:5
Mt. 6:4Met 19:17; Mt 10:42
Mt. 6:5Lu 18:11
Mt. 6:5Mt 6:16; 23:5
Mt. 6:6Lu 6:12
Mt. 6:8Lu 12:30
Mt. 6:9Lu 11:2-4
Mt. 6:9Kut 6:3; Zb 83:18
Mt. 6:9Eze 36:23
Mt. 6:10Da 2:44; Mt 6:33; Ufu 11:15
Mt. 6:10Mt 26:42; 1Ti 2:4; Ufu 4:11
Mt. 6:10Zb 37:10; Lu 23:43; Mdo 24:15
Mt. 6:11Zb 37:25; Met 30:8; Mt 6:34; 1Ti 6:8
Mt. 6:12Mt 18:21; Mk 11:25
Mt. 6:13Mt 26:41; 1Ko 10:13; Ufu 3:10
Mt. 6:13Yoh 17:15; 1Yo 5:19
Mt. 6:14Efe 4:32; Kol 3:13
Mt. 6:15Mt 18:35; Yak 2:13
Mt. 6:16Mdo 13:2, 3; 14:23
Mt. 6:16Isa 58:5; Lu 18:11, 12
Mt. 6:19Mt 13:22; Lu 12:20; Yak 5:3
Mt. 6:20Mt 19:21; Mk 10:21; Lu 12:33, 34; 18:22
Mt. 6:201Pe 1:3, 4
Mt. 6:22Met 4:25; Lu 11:34; Efe 1:18
Mt. 6:23Mt 20:15
Mt. 6:24Yak 4:4
Mt. 6:24Mt 13:22; Lu 16:13
Mt. 6:25Zb 55:22; Flp 4:6; 1Pe 5:6, 7
Mt. 6:251Ti 6:8; Ebr 13:5
Mt. 6:25Lu 12:22-28
Mt. 6:26Ayu 38:41; Zb 147:9; Mt 10:29
Mt. 6:27Zb 39:5
Mt. 6:291Fa 10:4, 5
Mt. 6:31Lu 10:41
Mt. 6:31Lu 12:29-31
Mt. 6:33Zb 37:25
Mt. 6:34Kut 16:4, 19
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Mathayo 6:1-34

Kulingana na Mathayo

6 “Iweni waangalifu msionyeshe uadilifu wenu mbele ya watu ili wawaone;+ la sivyo hamtapata thawabu kutoka kwa Baba yenu aliye mbinguni. 2 Basi unapotoa zawadi za rehema,* usipige tarumbeta mbele yako kama wanavyofanya wanafiki katika masinagogi na barabarani, ili wasifiwe na watu. Kwa kweli ninawaambia, wanapata thawabu yao kikamili. 3 Lakini wewe, unapotoa zawadi za rehema, usiache mkono wako wa kushoto ujue kile ambacho mkono wako wa kulia unafanya, 4 ili utoe zawadi za rehema kwa siri. Naye Baba yako anayetazama akiwa mahali pa siri atakulipa.+

5 “Pia, mnaposali msifanye kama wanafiki,+ kwa maana wanapenda kusali wakiwa wamesimama katika masinagogi na kwenye kona za barabara kuu ili watu wawaone.+ Kwa kweli ninawaambia, wanapata thawabu yao kikamili. 6 Lakini unaposali, ingia ndani ya chumba chako faraghani, baada ya kufunga mlango wako, sali kwa Baba yako aliye mahali pa siri.+ Naye Baba yako anayetazama akiwa mahali pa siri atakulipa. 7 Mnaposali msiseme mambo yaleyale tena na tena, kama vile watu wa mataifa wanavyofanya, kwa maana wao hufikiri watasikiwa kwa kutumia maneno mengi. 8 Kwa hiyo, msiwe kama wao, kwa sababu Baba yenu anajua kile mnachohitaji+ hata kabla hamjamwomba.

9 “Basi, salini hivi:+

“‘Baba yetu uliye mbinguni, jina lako+ na litakaswe.*+ 10 Ufalme wako+ na uje. Mapenzi yako+ na yatendeke duniani+ kama ilivyo mbinguni. 11 Utupatie leo mkate wetu kwa ajili ya siku hii;+ 12 na utusamehe madeni yetu, kama vile tunavyowasamehe wadeni wetu.+ 13 Na usituingize katika majaribu,+ bali utukomboe* kutoka kwa yule mwovu.’+

14 “Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao, Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi pia;+ 15 lakini msipowasamehe watu makosa yao, naye Baba yenu hatawasamehe makosa yenu.+

16 “Mnapofunga,+ msiwe na nyuso zenye huzuni kama wanafiki, kwa maana wao hukunja nyuso zao* ili watu waone kwamba wanafunga.+ Kwa kweli ninawaambia, wanapata thawabu yao kikamili. 17 Lakini wewe unapofunga, paka kichwa chako mafuta na unawe uso, 18 ili usionekane kwamba unafunga kwa wanadamu bali kwa Baba yako aliye mahali pa siri. Naye Baba yako anayeona akiwa mahali pa siri atakulipa.

19 “Acheni kujiwekea hazina duniani,+ ambako nondo* na kutu hula na ambako wezi huvunja na kuiba. 20 Badala yake, jiwekeeni hazina mbinguni,+ ambako hazitaliwa na nondo* wala kutu,+ na ambako wezi hawatavunja na kuiba. 21 Kwa maana mahali ilipo hazina yako, ndipo moyo wako utakapokuwa pia.

22 “Taa ya mwili ni jicho.+ Basi, ikiwa jicho lako linakazia jambo hususa,* mwili wako wote utakuwa mwangavu.* 23 Lakini ikiwa jicho lako lina wivu,*+ mwili wako wote utakuwa na giza. Ikiwa nuru iliyo ndani yako kwa kweli ni giza, basi giza hilo ni kubwa sana!

24 “Hakuna anayeweza kuwatumikia mabwana wawili; kwa maana atamchukia mmoja na kumpenda mwingine,+ au atashikamana na mmoja na kumdharau mwingine. Hamwezi kutumikia Mungu na Utajiri.+

25 “Kwa hiyo ninawaambia: Acheni kuhangaikia+ uhai wenu* kuhusu kile mtakachokula au kunywa, au juu ya miili yenu kuhusu kile mtakachovaa.+ Je, uhai* si zaidi ya chakula na mwili zaidi ya mavazi?+ 26 Waangalieni kwa makini ndege wa angani;+ hawapandi mbegu, hawavuni, wala kukusanya ghalani, na bado Baba yenu wa mbinguni huwalisha. Je, ninyi si wenye thamani kuliko wao? 27 Ni nani kati yenu ambaye kwa kuhangaika anaweza kurefusha uhai wake kwa mkono mmoja?*+ 28 Pia, kwa nini mnahangaika kuhusu mavazi? Jifunzeni kutoka kwa mayungiyungi* ya shambani, jinsi yanavyokua; hayafanyi kazi, wala hayasokoti; 29 lakini ninawaambia hata Sulemani+ katika utukufu wake wote hakupambwa kama maua hayo. 30 Basi, ikiwa Mungu huivika hivyo mimea ya shambani, ambayo ipo hapa leo na kesho hutupwa ndani ya jiko, je, hatawavika vizuri zaidi ninyi wenye imani ndogo? 31 Kwa hiyo msihangaike+ kamwe na kusema, ‘Tutakula nini?’ au, ‘Tutakunywa nini?’ au, ‘Tutavaa nini?’+ 32 Kwa maana mataifa yanatafuta vitu hivi vyote kwa bidii. Baba yenu wa mbinguni anajua kwamba mnahitaji vitu hivi vyote.

33 “Basi, endeleeni kuutafuta kwanza Ufalme na uadilifu wake,* nanyi mtaongezewa hivi vitu vingine vyote.+ 34 Basi, msihangaike kamwe kuhusu kesho,+ kwa maana kesho itakuwa na mahangaiko yake yenyewe. Kila siku ina matatizo yake ya kutosha.

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki