Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Methali 27
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Methali—Yaliyomo

    • METHALI ZA SULEMANI ZILIZONAKILIWA NA WATU WA MFALME HEZEKIA (25:1–29:27)

Methali 27:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “itazaa nini.”

Marejeo

  • +Lu 12:19, 20; Yak 4:13, 14

Methali 27:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “mtu asiyekujua.”

  • *

    Tnn., “Wageni.”

Marejeo

  • +Met 25:27; Yer 9:23; 2Ko 10:18

Methali 27:3

Marejeo

  • +1Sa 25:25

Methali 27:4

Marejeo

  • +Mwa 37:9-11; Met 14:30; Mdo 17:5

Methali 27:5

Marejeo

  • +Law 19:17; Mt 18:15

Methali 27:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “si ya unyoofu; ni ya kulazimishwa.”

Marejeo

  • +2Sa 12:7, 9; Zb 141:5; Ufu 3:19

Methali 27:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “huikanyagia chini.”

Methali 27:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “anayekimbia.”

Methali 27:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “shauri la nafsi.”

Marejeo

  • +1Sa 23:16; Met 15:23; 16:24

Methali 27:10

Marejeo

  • +Met 17:17; 18:24

Methali 27:11

Marejeo

  • +Met 10:1; 23:15; 2Yo 4
  • +Ayu 1:8, 9

Methali 27:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “adhabu.”

Marejeo

  • +Met 18:10; Isa 26:20; Ebr 11:7

Methali 27:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mgeni.”

Marejeo

  • +Met 20:16

Methali 27:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “msumbufu.”

Marejeo

  • +Met 21:9, 19

Methali 27:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “anavyounoa uso wa.”

Marejeo

  • +1Sa 23:16; Ebr 10:24, 25

Methali 27:18

Marejeo

  • +Met 13:4
  • +Mwa 39:2; Met 17:2

Methali 27:19

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “yanavyoakisi.”

  • *

    Au “unavyoakisi.”

Methali 27:20

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Sheoli na Abadoni.”

Marejeo

  • +Met 30:15, 16

Methali 27:21

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Vivyo hivyo mtu hulingana na sifa yake.”

Marejeo

  • +Met 17:3

Methali 27:22

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mtwangio.”

Methali 27:23

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Uweke moyo kwa; Wakazie uangalifu.”

Marejeo

  • +Kol 3:23

Methali 27:24

Marejeo

  • +Met 23:4, 5; 1Ti 6:17

Jumla

Met. 27:1Lu 12:19, 20; Yak 4:13, 14
Met. 27:2Met 25:27; Yer 9:23; 2Ko 10:18
Met. 27:31Sa 25:25
Met. 27:4Mwa 37:9-11; Met 14:30; Mdo 17:5
Met. 27:5Law 19:17; Mt 18:15
Met. 27:62Sa 12:7, 9; Zb 141:5; Ufu 3:19
Met. 27:91Sa 23:16; Met 15:23; 16:24
Met. 27:10Met 17:17; 18:24
Met. 27:11Met 10:1; 23:15; 2Yo 4
Met. 27:11Ayu 1:8, 9
Met. 27:12Met 18:10; Isa 26:20; Ebr 11:7
Met. 27:13Met 20:16
Met. 27:15Met 21:9, 19
Met. 27:171Sa 23:16; Ebr 10:24, 25
Met. 27:18Met 13:4
Met. 27:18Mwa 39:2; Met 17:2
Met. 27:20Met 30:15, 16
Met. 27:21Met 17:3
Met. 27:23Kol 3:23
Met. 27:24Met 23:4, 5; 1Ti 6:17
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Methali 27:1-27

Methali

27 Usijigambe kuhusu kesho,

Kwa maana hujui siku italeta nini.*+

 2 Acha mtu mwingine* akusifu, wala si kinywa chako mwenyewe;

Wengine,* wala si midomo yako mwenyewe.+

 3 Jiwe ni zito na mchanga ni mzito sana,

Lakini usumbufu unaosababishwa na mjinga ni mzito kuliko vyote viwili.+

 4 Kuna ukatili wa ghadhabu na mafuriko ya hasira,

Lakini ni nani anayeweza kustahimili wivu?+

 5 Karipio la wazi ni afadhali kuliko upendo uliofichwa.+

 6 Majeraha yanayosababishwa na rafiki ni ya uaminifu,+

Lakini mabusu ya adui ni mengi.*

 7 Yule aliyetosheleza hamu yake hukataa* asali ya sega,

Lakini kwa mwenye njaa, hata kilicho kichungu ni kitamu.

 8 Kama ndege anayeenda* mbali kutoka kwenye kiota chake

Ndivyo alivyo mtu anayetangatanga mbali kutoka nyumbani kwake.

 9 Mafuta na uvumba huufanya moyo ushangilie;

Ndivyo ulivyo urafiki mtamu unaochipuka kutokana na shauri la unyoofu.*+

10 Usimwache rafiki yako au rafiki ya baba yako,

Wala usiingie katika nyumba ya ndugu yako siku ya msiba wako;

Ni afadhali jirani aliye karibu kuliko ndugu aliye mbali.+

11 Uwe na hekima, mwanangu, na kuufanya moyo wangu ushangilie,+

Ili niweze kumjibu yule anayenidhihaki.+

12 Mtu mwerevu huona hatari na kujificha,+

Lakini wajinga husonga mbele na kupata madhara.*

13 Chukua vazi la mtu ikiwa amemdhamini mtu asiyemjua;

Chukua dhamana kutoka kwake ikiwa alimfanyia hivyo mwanamke mgeni.*+

14 Mtu akimbariki jirani yake kwa sauti kubwa asubuhi na mapema,

Itaonwa kuwa laana.

15 Mke mgomvi* ni kama paa linalovuja maji mfululizo siku ya mvua.+

16 Yeyote anayeweza kumzuia anaweza kuuzuia upepo

Naye anaweza kuyakamata mafuta kwa mkono wake wa kulia.

17 Kama chuma kinavyonoa chuma,

Ndivyo mtu anavyomnoa* rafiki yake.+

18 Anayeutunza mtini atakula matunda yake,+

Na anayemtunza bwana wake ataheshimiwa.+

19 Kama maji yanavyoonyesha* uso wa mtu,

Ndivyo moyo wa mtu unavyoonyesha* moyo wa mwingine.

20 Kaburi na mahali pa maangamizi* havitosheki kamwe,+

Wala macho ya mwanadamu hayatosheki kamwe.

21 Chungu cha kusafishia ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu,+

Vivyo hivyo mtu hupimwa kwa sifa anayopokea.*

22 Hata ukimtwanga mpumbavu kwa mchi*

Kama nafaka iliyopondwa katika kinu,

Upumbavu wake hautamtoka.

23 Unapaswa kujua vizuri hali ya kundi lako.

Watunze vizuri* kondoo wako,+

24 Kwa maana mali haidumu milele,+

Wala taji halidumu vizazi vyote.

25 Majani mabichi hutoweka, na majani mapya huchipuka,

Na majani ya milimani yanakusanywa.

26 Wanakondoo dume hukupatia mavazi yako,

Na mbuzi dume hukupatia malipo ya shamba.

27 Nawe utakuwa na maziwa ya mbuzi yanayotosha kukulisha wewe,

Kuilisha familia yako, na kuwategemeza vijakazi wako.

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki