Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zaburi 69
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Zaburi—Yaliyomo

      • Sala ya kuokolewa

        • “Bidii kwa ajili ya nyumba yako imenila” (9)

        • “Nijibu haraka” (17)

        • ‘Walinipa siki ninywe’ (21)

Zaburi 69:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nafsi yangu.”

Marejeo

  • +Zb 144:7; Omb 3:54; Yon 2:5

Zaburi 69:2

Marejeo

  • +Zb 40:2
  • +Zb 32:6; Yon 2:3

Zaburi 69:3

Marejeo

  • +Zb 22:2
  • +Zb 119:82, 123; Isa 38:14

Zaburi 69:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Wale ambao ni maadui wangu bila sababu.”

Marejeo

  • +Lu 23:22; Yoh 15:24, 25

Zaburi 69:7

Marejeo

  • +Zb 22:6; Yer 15:15
  • +Isa 50:6; Mt 26:67; 27:29

Zaburi 69:8

Marejeo

  • +Ayu 19:13; Zb 31:11; Yoh 1:11; 7:5

Zaburi 69:9

Marejeo

  • +1Fa 19:10; Zb 119:139; Mt 21:12, 13; Mk 11:15-17; Yoh 2:13-17
  • +Ro 15:3

Zaburi 69:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Nilipoinyenyekeza nafsi yangu.”

  • *

    Au labda, “Nilipolia na kufunga.”

Zaburi 69:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Nilikuwa methali kwao.”

Zaburi 69:13

Marejeo

  • +Isa 49:8; Ebr 5:7
  • +Zb 68:20

Zaburi 69:14

Marejeo

  • +Zb 144:7

Zaburi 69:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “shimo lifumbe.”

Marejeo

  • +Zb 69:2
  • +Zb 16:10

Zaburi 69:16

Marejeo

  • +Zb 63:3; 109:21
  • +Zb 25:16

Zaburi 69:17

Marejeo

  • +Zb 27:9; 102:2
  • +Zb 31:9; 40:13

Zaburi 69:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Ikaribie nafsi yangu uikomboe.”

Zaburi 69:19

Marejeo

  • +Zb 22:6

Zaburi 69:20

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “nami nimefikia hatua ya kukata tamaa.”

Marejeo

  • +Zb 142:4
  • +Ayu 19:14

Zaburi 69:21

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “mmea wenye sumu.”

Marejeo

  • +Mt 27:34; Mk 15:23
  • +Mt 27:48; Mk 15:36; Lu 23:36; Yoh 19:29

Zaburi 69:22

Marejeo

  • +Ro 11:9, 10

Zaburi 69:24

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “hasira yako kali.”

Marejeo

  • +Zb 21:9

Zaburi 69:25

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “Kambi yao iliyozingirwa na ukuta.”

Marejeo

  • +Mdo 1:20

Zaburi 69:28

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “kitabu cha uzima.”

Marejeo

  • +Kut 32:33
  • +Flp 4:3; Ufu 3:5; 13:8

Zaburi 69:29

Marejeo

  • +Zb 109:22

Zaburi 69:31

Marejeo

  • +Zb 50:13-15; Ho. 14:2

Zaburi 69:33

Marejeo

  • +Zb 10:17; 102:17; Isa 66:2
  • +Zb 146:7; Isa 61:1; Lu 4:18

Zaburi 69:34

Marejeo

  • +Zb 96:11; Isa 49:13

Zaburi 69:35

Maelezo ya Chini

  • *

    Yaani, ile nchi.

Marejeo

  • +Zb 51:18

Zaburi 69:36

Marejeo

  • +Isa 61:9; 66:22
  • +Zb 91:14; Yak 1:12

Jumla

Zab. 69:1Zb 144:7; Omb 3:54; Yon 2:5
Zab. 69:2Zb 40:2
Zab. 69:2Zb 32:6; Yon 2:3
Zab. 69:3Zb 22:2
Zab. 69:3Zb 119:82, 123; Isa 38:14
Zab. 69:4Lu 23:22; Yoh 15:24, 25
Zab. 69:7Zb 22:6; Yer 15:15
Zab. 69:7Isa 50:6; Mt 26:67; 27:29
Zab. 69:8Ayu 19:13; Zb 31:11; Yoh 1:11; 7:5
Zab. 69:91Fa 19:10; Zb 119:139; Mt 21:12, 13; Mk 11:15-17; Yoh 2:13-17
Zab. 69:9Ro 15:3
Zab. 69:13Isa 49:8; Ebr 5:7
Zab. 69:13Zb 68:20
Zab. 69:14Zb 144:7
Zab. 69:15Zb 69:2
Zab. 69:15Zb 16:10
Zab. 69:16Zb 63:3; 109:21
Zab. 69:16Zb 25:16
Zab. 69:17Zb 27:9; 102:2
Zab. 69:17Zb 31:9; 40:13
Zab. 69:19Zb 22:6
Zab. 69:20Zb 142:4
Zab. 69:20Ayu 19:14
Zab. 69:21Mt 27:34; Mk 15:23
Zab. 69:21Mt 27:48; Mk 15:36; Lu 23:36; Yoh 19:29
Zab. 69:22Ro 11:9, 10
Zab. 69:24Zb 21:9
Zab. 69:25Mdo 1:20
Zab. 69:28Kut 32:33
Zab. 69:28Flp 4:3; Ufu 3:5; 13:8
Zab. 69:29Zb 109:22
Zab. 69:31Zb 50:13-15; Ho. 14:2
Zab. 69:33Zb 10:17; 102:17; Isa 66:2
Zab. 69:33Zb 146:7; Isa 61:1; Lu 4:18
Zab. 69:34Zb 96:11; Isa 49:13
Zab. 69:35Zb 51:18
Zab. 69:36Isa 61:9; 66:22
Zab. 69:36Zb 91:14; Yak 1:12
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
  • 36
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Zaburi 69:1-36

Zaburi

Kwa kiongozi; umepatanishwa na mtindo wa “Mayungiyungi.” Wa Daudi.

69 Niokoe, Ee Mungu, kwa maana maji yanahatarisha uhai wangu.*+

 2 Nimezama chini katika matope yenye kina, mahali pasipo na udongo mgumu.+

Nimefika katika maji yenye kina,

Na kijito kinachotiririka haraka kimenifagilia mbali.+

 3 Nimechoka kupaza sauti;+

Koo langu limekauka.

Macho yangu yamechoka nikimngojea Mungu wangu.+

 4 Wale wanaonichukia bila sababu+

Ni wengi sana kuliko nywele za kichwa changu.

Wale wanaotaka kuniangamiza,

Maadui wangu wenye hila,* wamekuwa wengi.

Nililazimishwa kurudisha kitu ambacho sikuiba.

 5 Ee Mungu, unajua upumbavu wangu,

Na hatia yangu haijafichika mbele zako.

 6 Acha wale wanaokutumaini wasiaibishwe kwa sababu yangu,

Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi.

Wale wanaokutafuta na wasifedheheshwe kwa sababu yangu,

Ee Mungu wa Israeli.

 7 Ninashutumiwa kwa sababu yako;+

Aibu imefunika uso wangu.+

 8 Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu,

Mgeni kwa wana wa mama yangu.+

 9 Bidii kwa ajili ya nyumba yako imenila,+

Na shutuma za wale wanaokushutumu zimeniangukia.+

10 Nilipojinyenyekeza* kwa kufunga,*

Nilishutumiwa kwa sababu hiyo.

11 Nilipoyafanya magunia kuwa mavazi yangu,

Nikawa kitu cha kudharauliwa nao.*

12 Wale wanaoketi kwenye lango la jiji huzungumza kunihusu,

Na walevi huimba juu yangu katika nyimbo zao.

13 Lakini sala yangu na ikufikie,

Ee Yehova, kwa wakati unaofaa.+

Katika upendo wako mwingi mshikamanifu, Ee Mungu,

Nijibu kwa matendo yako hakika ya wokovu.+

14 Niokoe kutoka katika matope;

Usiache nizame.

Niokoe kutoka kwa wale wanaonichukia

Na kutoka katika maji yenye kina.+

15 Usiache mafuriko yenye kasi yanifagilie mbali,+

Wala kilindi kinimeze,

Wala kisima kifumbe* kinywa chake juu yangu.+

16 Nijibu, Ee Yehova, kwa maana upendo wako mshikamanifu ni mwema.+

Nigeukie kulingana na rehema zako nyingi,+

17 Wala usimfiche mtumishi wako uso wako.+

Nijibu haraka, kwa maana ninataabika.+

18 Nikaribie uniokoe;*

Nikomboe kwa sababu ya maadui wangu.

19 Unajua shutuma yangu na aibu yangu na fedheha yangu.+

Unawaona maadui wangu wote.

20 Shutuma imeuvunja moyo wangu, na jeraha haliwezi kuponywa.*

Nilitarajia kuhurumiwa, lakini sikuhurumiwa hata kidogo,+

Nilitarajia kupata watu wa kunifariji, lakini sikupata yeyote.+

21 Lakini walinipa sumu* kuwa chakula,+

Na wakanipa siki ninywe ili nikate kiu.+

22 Meza yao na iwe mtego kwao,

Na ufanisi wao uwe kitu cha kuwanasa.+

23 Acha macho yao yatiwe giza wasiweze kuona,

Na ufanye viuno vyao vitetemeke daima.

24 Wamwagie ghadhabu yako,*

Na hasira yako inayowaka iwapate.+

25 Kambi yao* na iwe ukiwa;

Mahema yao yasiwe na mkaaji yeyote.+

26 Kwa maana wanamfuatia yule uliyempiga,

Nao huendelea kusimulia kuhusu maumivu ya wale uliowajeruhi.

27 Ongeza hatia zaidi juu ya hatia yao,

Nao wasiwe na fungu lolote katika uadilifu wako.

28 Na wafutwe kutoka katika kitabu cha walio hai,*+

Na wasiorodheshwe miongoni mwa waadilifu.+

29 Lakini ninateseka, nami nina maumivu.+

Ee Mungu, nguvu zako za kuokoa na zinilinde.

30 Nitaliimbia sifa jina la Mungu,

Nami nitamtukuza kwa kutoa shukrani.

31 Jambo hilo litampendeza Yehova kuliko ng’ombe dume,

Kuliko ng’ombe dume mchanga mwenye pembe na kwato.+

32 Wapole wataona jambo hilo na kushangilia.

Mioyo yenu na ihuishwe, ninyi mnaomtafuta Mungu.

33 Kwa maana Yehova anawasikiliza maskini,+

Naye hatawadharau watu wake waliotekwa.+

34 Mbingu na dunia na zimsifu,+

Bahari na kila kitu kinachoogelea ndani yake.

35 Kwa maana Mungu ataliokoa Sayuni+

Naye atayajenga upya majiji ya Yuda,

Nao watakaa humo na kuimiliki.*

36 Wazao wa watumishi wake watairithi,+

Na wale wanaolipenda jina lake+ wataishi humo.

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki