Zaburi
Kwa kiongozi; umepatanishwa na mtindo wa “Mayungiyungi.” Wa Daudi.
69 Niokoe, Ee Mungu, kwa maana maji yanahatarisha uhai wangu.*+
2 Nimezama chini katika matope yenye kina, mahali pasipo na udongo mgumu.+
Nimefika katika maji yenye kina,
Na kijito kinachotiririka haraka kimenifagilia mbali.+
3 Nimechoka kupaza sauti;+
Koo langu limekauka.
Macho yangu yamechoka nikimngojea Mungu wangu.+
4 Wale wanaonichukia bila sababu+
Ni wengi sana kuliko nywele za kichwa changu.
Wale wanaotaka kuniangamiza,
Maadui wangu wenye hila,* wamekuwa wengi.
Nililazimishwa kurudisha kitu ambacho sikuiba.
5 Ee Mungu, unajua upumbavu wangu,
Na hatia yangu haijafichika mbele zako.
6 Acha wale wanaokutumaini wasiaibishwe kwa sababu yangu,
Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi.
Wale wanaokutafuta na wasifedheheshwe kwa sababu yangu,
Ee Mungu wa Israeli.
8 Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu,
Mgeni kwa wana wa mama yangu.+
11 Nilipoyafanya magunia kuwa mavazi yangu,
Nikawa kitu cha kudharauliwa nao.*
12 Wale wanaoketi kwenye lango la jiji huzungumza kunihusu,
Na walevi huimba juu yangu katika nyimbo zao.
13 Lakini sala yangu na ikufikie,
Ee Yehova, kwa wakati unaofaa.+
Katika upendo wako mwingi mshikamanifu, Ee Mungu,
Nijibu kwa matendo yako hakika ya wokovu.+
14 Niokoe kutoka katika matope;
Usiache nizame.
Niokoe kutoka kwa wale wanaonichukia
Na kutoka katika maji yenye kina.+
15 Usiache mafuriko yenye kasi yanifagilie mbali,+
Wala kilindi kinimeze,
16 Nijibu, Ee Yehova, kwa maana upendo wako mshikamanifu ni mwema.+
Nijibu haraka, kwa maana ninataabika.+
18 Nikaribie uniokoe;*
Nikomboe kwa sababu ya maadui wangu.
19 Unajua shutuma yangu na aibu yangu na fedheha yangu.+
Unawaona maadui wangu wote.
20 Shutuma imeuvunja moyo wangu, na jeraha haliwezi kuponywa.*
Nilitarajia kuhurumiwa, lakini sikuhurumiwa hata kidogo,+
Nilitarajia kupata watu wa kunifariji, lakini sikupata yeyote.+
22 Meza yao na iwe mtego kwao,
Na ufanisi wao uwe kitu cha kuwanasa.+
23 Acha macho yao yatiwe giza wasiweze kuona,
Na ufanye viuno vyao vitetemeke daima.
26 Kwa maana wanamfuatia yule uliyempiga,
Nao huendelea kusimulia kuhusu maumivu ya wale uliowajeruhi.
27 Ongeza hatia zaidi juu ya hatia yao,
Nao wasiwe na fungu lolote katika uadilifu wako.
29 Lakini ninateseka, nami nina maumivu.+
Ee Mungu, nguvu zako za kuokoa na zinilinde.
30 Nitaliimbia sifa jina la Mungu,
Nami nitamtukuza kwa kutoa shukrani.
31 Jambo hilo litampendeza Yehova kuliko ng’ombe dume,
Kuliko ng’ombe dume mchanga mwenye pembe na kwato.+
32 Wapole wataona jambo hilo na kushangilia.
Mioyo yenu na ihuishwe, ninyi mnaomtafuta Mungu.
34 Mbingu na dunia na zimsifu,+
Bahari na kila kitu kinachoogelea ndani yake.