Cha Pili cha Samweli
22 Na Daudi akamuambia Yehova maneno ya wimbo huu+ siku yenye Yehova alimuokoa katika mukono wa maadui wake wote+ na katika mukono wa Sauli.+ 2 Akasema:
“Yehova ni mwamba wangu na ngome yangu+ na Ule mwenye ananiokoa.+
3 Mungu wangu ni mwamba wangu,+ mwenye ninakimbilia,
Ngao yangu+ na pembe* yangu ya wokovu,* kimbilio langu salama*+
Na mahali pangu pa kukimbilia,+ mwokozi wangu;+ wewe mwenye unaniokoa katika jeuri.
4 Ninamuitia Yehova, mwenye anastahili kusifiwa,
Na nitaokolewa kutoka kwa maadui wangu.
5 Mawimbi ya kifo yalinizunguka pande zote;+
Mafuriko ya kushitukia ya watu wenye hawana mafaa yoyote yaliniogopesha sana.+
7 Katika taabu yangu nilimuitia Yehova,+
Niliendelea kumuita Mungu wangu.
Kisha akiwa katika hekalu lake akasikia sauti yangu,
Na kilio changu cha kuomba musaada kikafika katika masikio yake.+
8 Dunia ikaanza kutetemeka na kutikisika huku na huku;+
Misingi ya mbingu ikatetemeka+
Na kutikisika huku na huku kwa sababu alikuwa amekasirishwa.+
9 Moshi ulipanda kutoka katika matundu ya pua yake,
Na moto wenye kuteketeza ukatoka katika kinywa chake;+
Makaa yenye kuwaka yakatoka kwake.
11 Alipanda juu ya kerubi+ na akakuja akiruka.
Alionekana juu ya mabawa ya roho.*+
12 Kisha akatia giza kumuzunguka kama kibanda,+
Katika maji yenye giza na mawingu mazito.
13 Kutoka katika mwangaza wenye kuwa mbele yake makaa yenye moto yaliwaka.
14 Kisha Yehova akaanza kunguruma akiwa mbinguni;+
Mwenye Kuwa Juu Zaidi akafanya sauti yake isikike.+
16 Sehemu ya chini ya bahari ikaonekana;+
Misingi ya inchi ikafunuliwa kwa kemeo la Yehova,
Kwa mulipuko wa pumuzi kutoka katika matundu ya pua yake.+
17 Akiwa juu, alininyooshea mukono;
Akanishika na kunikokota kutoka katika maji yenye kuenda chini sana.+
18 Aliniokoa kutoka kwa adui yangu mwenye nguvu,+
Kutoka kwa wale wenye kunichukia, wenye walikuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
19 Walinishambulia katika siku ya musiba wangu,+
Lakini Yehova alikuwa tegemeo langu.
21 Yehova ananipatia zawabu kulingana na haki yangu;+
Ananilipa kulingana na kutokuwa na hatia kwa* mikono yangu.+
22 Kwa maana nimeshika njia za Yehova,
Na sijamuacha kwa uovu Mungu wangu.
26 Kwa mutu mushikamanifu unatenda kwa ushikamanifu;+
Kwa mutu mwenye hana lawama, mwenye nguvu, unatenda bila lawama;+
27 Kwa mwenye kuwa safi unajionyesha kuwa safi,+
Lakini kwa mwenye kupotoka unajionyesha kuwa mwenye busara.*+
30 Kwa musaada wako ninaweza kushambulia kikundi cha wanyanganyi;
Kwa nguvu za Mungu ninaweza kupanda ukuta.+
Yeye ni ngao kwa wote wenye kumukimbilia.+
32 Kwa maana ni nani iko* Mungu isipokuwa Yehova?+
Na ni nani iko* mwamba isipokuwa Mungu wetu?+
34 Anafanya miguu yangu ikuwe kama ya paa;
Ananifanya nisimame mahali pa juu.+
35 Anazoeza mikono yangu kwa ajili ya vita;
Mikono yangu inaweza kukunja upinde wa shaba.
38 Nitafuatilia maadui wangu na kuwaharibu;
Sitarudia mupaka wakati watakuwa wamefutwa.
39 Na nitawafuta na kuwaponda-ponda, na hivyo hawatasimama;+
Wataanguka chini ya miguu yangu.
42 Wanalilia musaada, lakini hakuna mutu wa kuwaokoa;
Hata wanamulilia Yehova, lakini yeye hawajibu.+
43 Nitawatwanga ili wakuwe laini kama mavumbi ya dunia;
Nitawaponda-ponda na kuwakanyanga-kanyanga kama matope katika barabara.
44 Utaniokoa kutokana na tabia ya watu wangu ya kutafuta-tafuta makosa.+
45 Wageni watakuja wakijikunja kwa woga mbele yangu;+
Mambo yenye watasikia kunihusu yatawafanya wanitii.*
46 Wageni watakosa uhodari;*
Watakuja wakitetemeka kutoka katika ngome zao.
47 Yehova ni mwenye kuishi! Mwamba wangu asifiwe!+
Mungu wa mwamba wa wokovu wangu atukuzwe.+