Cha Pili cha Wafalme
11 Sasa wakati Atalia+ mama ya Ahazia aliona kwamba mwana wake alikuwa amekufa,+ akasimama na kuharibu ukoo wote wa kifalme.*+ 2 Lakini, Yehosheba binti ya Mufalme Yehoramu, dada ya Ahazia, akamuchukua Yehoashi+ mwana wa Ahazia na akamuiba kutoka kati ya wana wa mufalme wenye walipaswa kuuawa, na akamuweka yeye pamoja na mutu wake wa kumulea katika chumba kimoja cha ndani cha kulala. Wakaweza kumuficha ili Atalia asimuone, kwa hiyo hakuuawa. 3 Akakaa pamoja naye kwa miaka sita (6), akiwa amefichwa kwenye nyumba ya Yehova, wakati Atalia alikuwa anatawala juu ya inchi.
4 Katika mwaka wa saba (7), Yehoyada alituma watu waite wakubwa wa mamia wa walinzi Wakari na wa walinzi* wa nyumba za mufalme+ na wakaletwa kwake katika nyumba ya Yehova. Akafanya mapatano* pamoja nao na kuwaapisha juu ya jambo hilo katika nyumba ya Yehova, na kisha akawaonyesha mwana wa mufalme.+ 5 Akawaagiza: “Ni hivi munapaswa kufanya: Sehemu moja ya tatu (1/3) kati yenu watakuwa na mugao wa kutimiza katika siku ya Sabato na watafanya ulinzi mukali juu ya nyumba ya mufalme,+ 6 sehemu ingine moja ya tatu (1/3) watakuwa kwenye Mulango Mukubwa wa Musingi, na sehemu ingine moja ya tatu (1/3) watakuwa kwenye mulango mukubwa nyuma ya walinzi wa nyumba ya mufalme. Mutalinda nyumba hiyo kwa kubadilishana. 7 Vikundi vyenu mbili vyenye vinapaswa kupumuzika katika siku ya Sabato vinapaswa kufanya ulinzi mukali juu ya nyumba ya Yehova ili kumulinda mufalme. 8 Munapaswa kuzunguka mufalme pande zote, kila mumoja akiwa na silaha zake katika mukono. Mutu yeyote mwenye anaingia katikati ya majeshi atauawa. Mubakie na mufalme kila mahali anaenda.”*
9 Wakubwa wa mamia+ wakafanya sawasawa na mambo yenye Yehoyada kuhani alikuwa ameamuru. Basi kila mumoja akachukua wanaume wake wenye walikuwa na mugao siku ya Sabato, pamoja na wale wenye hawakukuwa na mugao siku ya Sabato, na wakaingia kwa Yehoyada kuhani.+ 10 Kisha kuhani akapatia wakubwa wa mamia mikuki na ngao za muviringo zenye zilikuwa za Mufalme Daudi, zenye zilikuwa katika nyumba ya Yehova. 11 Na walinzi wa nyumba ya mufalme+ wakasimama mahali pao, kila mumoja akiwa na silaha zake katika mukono, kuanzia upande wa kuume wa nyumba mupaka upande wa kushoto wa nyumba, pembeni ya mazabahu+ na pembeni ya nyumba hiyo, kuzunguka mufalme pande zote. 12 Kisha Yehoyada akamuleta mwana wa mufalme+ inje na akaweka juu yake taji na Ushuhuda,*+ na wakamufanya kuwa mufalme na kumutia mafuta. Wakaanza kupiga mikono yao na kusema: “Mufalme aishi siku nyingi!”+
13 Wakati Atalia alisikia sauti ya watu wenye kukimbia, mara moja akakuja kwa watu kwenye nyumba ya Yehova.+ 14 Kisha akamuona mufalme akiwa amesimama pale karibu na nguzo kulingana na desturi.+ Wakubwa na wapiga-tarumbeta+ walikuwa pamoja na mufalme, na watu wote wa inchi walikuwa wanafurahi na kupiga tarumbeta. Halafu Atalia akapasua nguo zake na kusema kwa sauti kubwa: “Ni mupango mubaya! Ni mupango mubaya!” 15 Lakini Yehoyada kuhani akaamuru wakubwa wa mamia,+ wale wenye waliwekwa juu ya jeshi, na kuwaambia: “Mumutoshe katikati ya majeshi, na kama mutu yeyote anamufuata, mumuue kwa upanga!” Kwa maana kuhani alikuwa amesema: “Musimuue ndani ya nyumba ya Yehova.” 16 Basi wakamukamata, na wakati alifika mahali kwenye farasi wanaingilia katika nyumba ya mufalme,+ akauawa pale.
17 Kisha Yehoyada akafanya agano kati ya Yehova na mufalme na watu,+ kwamba wataendelea kuwa watu wa Yehova, na akafanya pia agano kati ya mufalme na watu.+ 18 Kisha, watu wote wa inchi wakakuja kwenye nyumba ya* Baali na wakabomoa mazabahu zake,+ wakavunja kabisa sanamu zake,+ na wakamuua Matani kuhani wa Baali+ mbele ya zile mazabahu.
Kisha kuhani akaweka waangalizi juu ya nyumba ya Yehova.+ 19 Tena, akachukua wakubwa wa mamia,+ walinzi Wakari, walinzi wa nyumba ya mufalme,+ na watu wote wa inchi ili wasindikize mufalme kushuka kutoka kwenye nyumba ya Yehova, na wakakuja kwenye nyumba ya mufalme kupitia njia ya mulango mukubwa wa walinzi wa nyumba ya mufalme. Kisha akakaa kwenye kiti cha wafalme.+ 20 Basi watu wote wa inchi wakafurahi na muji ukatulia, kwa maana walikuwa wamemuua Atalia kwa upanga kwenye nyumba ya mufalme.
21 Yehoashi+ alikuwa na miaka saba (7) wakati alikuwa mufalme.+