-
Kutoka 8:7Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
7 Lakini, makuhani wenye kufanya uchawi wakafanya jambo lilelile kwa ufundi wao wa siri, na wakafanya vyura wakuje juu ya inchi ya Misri.+
-
-
Kumbukumbu la Torati 18:10-12Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
10 Asipatikane katikati yako mutu yeyote mwenye kupitisha mutoto wake mwanaume ao mutoto wake mwanamuke katika moto,+ mutu yeyote mwenye kufanya uaguzi,+ mutu yeyote mwenye kufanya uchawi,+ mutu yeyote mwenye kutafuta alama za mambo yenye yatatokea,+ mulozi,+ 11 mutu yeyote mwenye anafunga wengine kwa uchawi, mutu yeyote mwenye anatafuta shauri kwa mutu mwenye kupashana habari na pepo wachafu+ ao mutu mwenye kutabiri matukio,+ ao mutu yeyote mwenye kuuliza habari kwa wafu.+ 12 Kwa maana kila mutu mwenye kufanya mambo hayo ni chukizo kwa Yehova, na kwa sababu ya mazoea hayo yenye kuchukiza, Yehova Mungu wako anafukuza mataifa hayo mbele yako.
-
-
Ufunuo 21:8Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
8 Lakini wale wenye woga na wale wenye hawana imani+ na wale wenye kuchukiza katika uchafu wao na wauaji+ na waasherati*+ na wale wenye wanazoea kupashana habari na pepo wachafu na waabudu-sanamu na waongo wote,+ fungu lao litakuwa ndani ya lile ziwa lenye linawaka moto na kiberiti.+ Hili linamaanisha kifo cha pili.”+
-