-
Kumbukumbu la Torati 16:9-11Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
9 “Utahesabia majuma saba (7). Unapaswa kuanza kuhesabia majuma saba kuanzia wakati unatia mundu* kwa mara ya kwanza kwenye nafaka yenye kusimama.+ 10 Kisha utafanya Sikukuu ya Majuma kwa ajili ya Yehova Mungu wako+ kupitia toleo la kujipendea kutoka katika mukono wako, lenye utatoa kulingana na namna Yehova Mungu wako anakubariki.+ 11 Na unapaswa kushangilia mbele ya Yehova Mungu wako, wewe na mutoto wako mwanaume, mutoto wako mwanamuke, mutumwa wako mwanaume, mutumwa wako mwanamuke, Mulawi mwenye kuwa ndani ya miji yako,* mukaaji mugeni, mutoto mwenye hana baba,* na mujane, wenye kuwa katikati yako, mahali kwenye Yehova Mungu wako atachagua jina lake likae.+
-