Zaburi
KITABU CHA KWANZA
(Zaburi 1-41)
1 Mwenye furaha ni mutu mwenye hatembee kulingana na shauri la waovu
Na hasimame katika njia ya watenda-zambi+
Naye hakae katika kiti cha wenye kuzihaki.+
2 Lakini anapendezwa na sheria ya Yehova,+
Na anasoma sheria Yake kwa sauti ya chini* muchana na usiku.+
3 Atakuwa kama muti wenye kupandwa pembeni ya mito midogo ya maji,
Muti wenye unazaa matunda katika wakati wake,
Na majani yake hayakauke.
Na kila jambo lenye anafanya litafanikiwa.+
4 Waovu hawako vile;
Wako kama maganda ya mbegu yenye kupeperushwa mbali na upepo.