Waamuzi
8 Kisha watu wa Efraimu wakamuambia: “Mbona umetutendea hivi? Sababu gani haukutuita wakati ulienda kupigana na Wamidiani?”+ Na wakamulaumu kwa ukali.+ 2 Lakini akawaambia: “Nimefanya nini nikilinganishwa na ninyi? Je, masalio ya mizabibu ya Waefraimu+ hayako ya muzuri kuliko mavuno ya mizabibu ya Abiezeri?+ 3 Mungu alitia katika mukono wenu Orebu na Zeebu,+ wakubwa wa Midiani, mimi nimefanya nini nikilinganishwa na ninyi?” Wakati Gideoni alisema vile,* kasirani yao ikapoa.*
4 Basi Gideoni akafika kwenye Muto Yordani na kuuvuka. Yeye na wale wanaume mia tatu (300) wenye walikuwa pamoja naye walikuwa wamechoka, lakini waliendelea kufuatilia maadui wao. 5 Akaambia watu wa Sukoti: “Tafazali mupatie mikate watu wenye kuwa pamoja na mimi, kwa maana wamechoka na ninafuatilia Zeba na Zalmuna, wafalme wa Midiani.” 6 Lakini wakubwa wa Sukoti wakasema: “Je, tayari viganja vya mikono ya Zeba na Zalmuna viko katika mukono wako ili tupatie jeshi lako mikate?” 7 Basi Gideoni akasema: “Kwa sababu hiyo, wakati Yehova atatia Zeba na Zalmuna katika mukono wangu, nitawapiga kwa miiba na michongoma ya jangwa.”+ 8 Na akapanda kutoka pale na kuenda Penueli na akaomba jambo lilelile, lakini watu wa Penueli wakamujibu kama vile watu wa Sukoti walimujibu. 9 Basi akaambia pia watu wa Penueli: “Wakati nitarudia kwa amani, nitabomoa munara huu.”+
10 Basi Zeba na Zalmuna walikuwa Karkori pamoja na majeshi yao, watu karibu elfu kumi na tano (15 000). Hao tu ndio wenye walibakia kati ya jeshi lote la watu wa Mashariki,+ kwa maana watu elfu mia moja makumi mbili (120 000) wenye kubeba upanga walikuwa wameuawa. 11 Gideoni akaendelea kupanda kupitia njia ya watu wenye kukaa katika mahema upande wa mashariki wa Noba na Yogbeha+ na akashambulia kambi, yenye wanajeshi wake hawakukuwa tayari kupigana. 12 Wakati Zeba na Zalmuna walikimbia, alifuatilia na kukamata hao wafalme wawili wa Midiani, Zeba na Zalmuna, na kambi yao yote ikaogopa.
13 Kisha Gideoni mwana wa Yoashi akarudia kutoka katika vita kupitia njia yenye kupanda kuenda Heresi. 14 Wakati alikuwa katika njia, alimukamata kijana mumoja mwanaume wa Sukoti na kumuuliza maulizo. Basi kijana huyo mwanaume akamuandikia majina makumi saba na saba (77) ya wakubwa na wazee wa Sukoti. 15 Basi akarudia kwa watu wa Sukoti na kusema: “Muone Zeba na Zalmuna wenye mulinichokoza juu yao, kwa kusema, ‘Je, tayari viganja vya mikono ya Zeba na Zalmuna viko katika mukono wako ili tupatie watu wako wenye kuchoka mikate?’”+ 16 Kisha akachukua wazee wa muji na kwa miiba na michongoma ya jangwa, akafundisha watu wa Sukoti somo.+ 17 Na akabomoa munara wa Penueli+ na kuua watu wa muji huo.
18 Akauliza Zeba na Zalmuna: “Watu wenye muliua kule Tabori walikuwa watu wa namna gani?” Wakasema: “Walikuwa kama wewe, kila mumoja alikuwa kama mwana wa mufalme.” 19 Basi akasema: “Walikuwa ndugu zangu, wana wa mama yangu. Kama vile hakika Yehova anaishi, ikiwa hamungewaua, mimi pia singewaua ninyi.” 20 Kisha akamuambia Yeteri muzaliwa wake wa kwanza: “Simama, uwaue.” Lakini kijana huyo mwanaume hakuchomoa upanga wake; aliogopa, kwa sababu alikuwa kijana tu. 21 Basi Zeba na Zalmuna wakamuambia: “Simama wewe mwenyewe na utuue, kwa maana mwanaume anatambuliwa kwa nguvu zake.”* Basi Gideoni akaua Zeba na Zalmuna+ na kukamata mapambo yenye umbo ya mwezi mupya yenye yalikuwa kwenye shingo za ngamia wao.
22 Kisha wakati fulani watu wa Israeli wakamuambia Gideoni: “Utawale juu yetu, wewe na mwana wako na mujukuu wako pia, kwa maana umetuokoa katika mukono wa Midiani.”+ 23 Lakini Gideoni akawaambia: “Mimi sitatawala juu yenu, wala mwana wangu hatatawala juu yenu. Yehova ndiye atatawala juu yenu.”+ 24 Pia akawaambia: “Acha niwaombe jambo moja: kila mumoja wenu anipatie pete ya pua kutoka katika vitu vyake vyenye vilichukuliwa katika vita.” (Kwa maana walikuwa na pete za pua za zahabu kwa sababu walikuwa Waishmaeli.)+ 25 Wakajibu: “Hakika tutakupatia pete hizo.” Basi wakatandika nguo ya kujifunika na kila mumoja wao akatupa juu ya nguo hiyo pete ya pua kutoka katika vitu vyake vyenye vilichukuliwa katika vita. 26 Uzito wa zile pete za pua za zahabu zenye alikuwa ameomba ulikuwa shekeli* elfu moja mia saba (1 700) za zahabu, bila kuhesabia yale mapambo yenye umbo ya mwezi mupya, mapambo ya mikufu,* nguo za manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau zenye kuvaliwa na wafalme wa Midiani, na mikufu yenye ilikuwa kwenye shingo za ngamia wao.+
27 Basi Gideoni akatumia vitu hivyo ili kutengeneza efodi+ na kuitia katika muji wake wa Ofra;+ na Israeli wote wakafanya nayo ukahaba wa kiroho kule,+ na ikakuwa mutego kwa Gideoni na kwa nyumba yake.+
28 Basi Wamidiani+ wakanyenyekezwa mbele ya Waisraeli, na hawakuwachokoza tena;* na inchi ikapata pumuziko kwa miaka makumi ine (40) katika siku za Gideoni.+
29 Basi Yerubaali+ mwana wa Yoashi akarudia kwake na kukaa kule.
30 Gideoni akakuwa na wana makumi saba (70),* kwa sababu alikuwa na bibi wengi. 31 Suria* wake mwenye alikuwa kule Shekemu akamuzalia mwana, na Gideoni akamupatia jina Abimeleki.+ 32 Na Gideoni mwana wa Yoashi akakufa katika uzee muzuri, akazikwa katika kaburi la Yoashi baba yake katika muji wa Ofra wa Waabiezeri.+
33 Kisha tu Gideoni kufa, Waisraeli wakaanza tena kufanya ukahaba wa kiroho pamoja na Mabaali,+ na wakafanya Baal-beriti kuwa mungu wao.+ 34 Waisraeli hawakumukumbuka Yehova Mungu wao,+ mwenye aliwaokoa katika mukono wa maadui wao wote wenye waliwazunguka;+ 35 na hawakuonyesha upendo mushikamanifu kwa nyumba ya Yerubaali, ni kusema, Gideoni, kwa ajili ya mambo yote ya muzuri yenye alikuwa amefanyia Israeli.+