Isaya
2 Hili ndilo jambo lenye Isaya mwana wa Amozi aliona kuhusu Yuda na Yerusalemu:+
2 Katika kipindi cha mwisho cha zile siku,
Mulima wa nyumba ya Yehova
Utawekwa imara kabisa kwenye kichwa cha milima,+
Na utainuliwa juu ya vilima,
Na mataifa yote yatamiminika kule.+
3 Na vikundi vingi vya watu vitaenda na kusema:
“Mukuje, tupande kwenye mulima wa Yehova,
Kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo.+
Atatufundisha njia zake,
Na tutatembea katika mapito yake.”+
Watafua panga zao kuwa majembe
Na mikuki yao kuwa miundu.+
Taifa halitainua upanga juu ya taifa,
Wala hawatajifunza vita tena.+
6 Kwa maana umeacha watu wako, nyumba ya Yakobo,+
Kwa sababu wamejaa vitu vya kutoka Mashariki;
Wanafanya uchawi+ kama Wafilisti,
Na wako na watoto wengi wa wageni.
7 Inchi yao imejaa feza na zahabu,
Na hazina zao hazina mwisho.
Inchi yao imejaa farasi,
Na magari yao hayana mwisho.+
8 Inchi yao imejaa miungu yenye haina mafaa yoyote.+
Wanainamia kazi ya mikono yao wenyewe,
Wanainamia kile chenye vidole vyao wenyewe vimetengeneza.
9 Basi mutu anainama, anashuka,
Na hauwezi kuwasamehe.
10 Ingia ndani ya mwamba na ujifiche katika mavumbi
Kwa sababu ya kuwapo kwa Yehova kwenye kuogopesha sana
Na utukufu wake mukubwa.+
Yehova peke yake ndiye atainuliwa siku hiyo.
12 Kwa maana hiyo ni siku ya Yehova wa majeshi.+
Inakuja juu ya kila mutu mwenye majivuno na mwenye kujipandisha,
Juu ya kila mutu, kama ni mwenye kuinuliwa ao mwenye kuwa chini,+
13 Juu ya mierezi yote ya Lebanoni yenye kuwa ya murefu na yenye kuinuliwa
Na juu ya mialoni yote ya Bashani,
14 Juu ya milima yote ya murefu
Na juu ya vilima vyote vya murefu,
15 Juu ya kila munara murefu na kila ukuta wenye ngome,
16 Juu ya mashua* zote za Tarshishi+
Na juu ya mashua zote zenye kutamanika.
17 Kiburi cha mwanadamu kitashushwa,
Na majivuno ya wanadamu yatainama.*
Yehova peke yake ndiye atainuliwa siku hiyo.
18 Miungu yenye haina mafaa yoyote haitakuwa tena.+
19 Na watu wataingia ndani ya mapango ya miamba
Na ndani ya mashimo katika udongo,+
Kwa sababu ya kuwapo kwa Yehova kwenye kuogopesha sana
Na utukufu wake mukubwa,+
Wakati anasimama ili kufanya dunia itetemeke kwa woga mukubwa.
20 Siku hiyo wanadamu watakamata miungu yao yenye haina mafaa yoyote, ya feza na zahabu
Yenye walijitengenezea ili waiinamie
Na wataitupia panya-sange* na popo,+
21 Ili kuingia katika mashimo yenye kuwa katika miamba
Na ndani ya mipasuko ya miamba,
Kwa sababu ya kuwapo kwa Yehova kwenye kuogopesha sana
Na utukufu wake mukubwa,
Wakati anasimama ili kufanya dunia itetemeke kwa woga mukubwa.
22 Kwa ajili yenu wenyewe, muache kutumainia mwanadamu bure,
Mwenye ni pumuzi tu yenye kuwa katika matundu ya pua yake.*
Sababu gani afikiriwe?