Zaburi
Muziki wa Daudi.
141 Ee Yehova, ninakuitia.+
Kuja haraka unisaidie.+
Sikiliza wakati ninakuita.+
2 Sala yangu ikuwe kama uvumba+ wenye kutayarishwa mbele yako,+
Mikono yangu yenye kuinuliwa ikuwe kama toleo la nafaka la mangaribi.+
3 Weka mulinzi kwa ajili ya kinywa changu, Ee Yehova,
Weka ulinzi kwenye mulango wa midomo yangu.+
4 Usiache moyo wangu uelekee kwenye jambo lolote la mubaya,+
Ili nisishiriki katika matendo maovu pamoja na watu waovu;
Nisikule hata kidogo vyakula vyao vitamu.
5 Kama mwenye haki ananipiga, hilo litakuwa tendo la upendo mushikamanifu;+
Kama ananikaripia, hilo litakuwa kama mafuta kwenye kichwa changu,+
Yenye kichwa changu hakitakataa hata kidogo.+
Sala yangu itaendelea hata wakati wa misiba yao.
6 Hata kama waamuzi wao wanatupwa chini kutoka kwenye muteremuko mukali,
Watu watasikiliza maneno yangu, kwa maana ni yenye kupendeza.
7 Kama vile wakati mutu analima na kuvunja-vunja udongo,
Ni vile mifupa yetu imesambazwa kwenye kinywa cha Kaburi.*
8 Lakini macho yangu yanakuangalia, Ee Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova.+
Nimekukimbilia.
Usiondoe uzima wangu.*
9 Unilinde kutokana na mataya* ya mutego wenye wamenitegea,
Kutokana na mitego ya watenda-maovu.