Mezali
9 Hekima ya kweli imejenga nyumba yake;
Imechonga nguzo zake saba (7).
4 “Mutu yeyote mwenye hana uzoefu, aingie humu.”
Anamuambia ule mwenye hana akili ya muzuri:*
5 “Kuja, ukule mukate wangu
Na ukunywe divai yenye nilichanganya.
7 Ule mwenye kumurekebisha mutu mwenye zihaka anaalika haya,+
Na mutu yeyote mwenye kumukaripia mutu muovu ataumia.
8 Usimukaripie mutu mwenye zihaka, kwa maana atakuchukia.+
Karipia mwenye hekima, naye atakupenda.+
9 Patia mwenye hekima, na atakuwa mwenye hekima zaidi.+
Fundisha mwenye haki, na elimu yake itaongezeka.
12 Kama unakuwa mwenye hekima, unakuwa mwenye hekima kwa faida yako mwenyewe,
Lakini kama uko mwenye zihaka, utabeba zihaka hiyo peke yako.
13 Mwanamuke mujinga ni mwenye fujo.+
Yeye ni mujinga na hajue kitu.
14 Anakaa kwenye muingilio wa nyumba yake
Kwenye kiti katika mahali pa juu pa muji,+
15 Anaita kwa sauti kubwa wale wenye kupita karibu naye,
Wale wenye kuenda mbele moja kwa moja katika njia yao:
16 “Mutu yeyote mwenye hana uzoefu, aingie humu.”