Kwa kiongozi; iimbwe kwa
vyombo vya kamba. Ya Daudi.
61 Ee Mungu, sikia kilio changu cha kuomba musaada.
Sikiliza sala yangu.+
2 Nitakulilia kwa sauti kutoka kwenye miisho ya dunia
Wakati moyo wangu umepoteza tumaini.+
Uniongoze kwenye mwamba wenye kuwa juu kuliko mimi.+
3 Kwa maana wewe ni kimbilio langu,
Munara wenye nguvu wenye unanilinda na adui.+
4 Nitakuwa mugeni katika hema yako milele;+
Nitakimbilia katika kivuli cha mabawa yako.+ (Sela)
5 Kwa maana wewe, Ee Mungu, umesikia naziri zangu.
Umenipatia uriti wa wale wenye kuogopa jina lako.+
6 Utaongeza siku kwenye maisha ya mufalme,+
Na miaka yake itakuwa kuanzia kizazi mupaka kizazi.
7 Atakaa akiwa mufalme milele mbele ya Mungu;+
Umupatie upendo wako mushikamanifu na uaminifu, ili vimulinde.+
8 Kisha nitaimbia jina lako sifa milele,+
Wakati nitakuwa ninatimiza naziri zangu siku kwa siku.+