Zaburi
89 Nitaimba kuhusu maonyesho ya Yehova ya upendo mushikamanifu milele.
Kwa kinywa changu nitajulisha vizazi vyote uaminifu wako.
2 Kwa maana nimesema: “Upendo mushikamanifu utajengwa* milele,+
Na umefanya uaminifu wako ukuwe imara kabisa kule mbinguni.”
4 ‘Nitafanya uzao wako ukuwe* imara kabisa+ milele,
Na nitajenga kiti chako cha ufalme kwa vizazi vyote.’”+ (Sela)
5 Mbingu zinasifu mambo yako ya ajabu, Ee Yehova,
Ndiyo, uaminifu wako katika kutaniko la watakatifu.
6 Kwa maana ni nani mbinguni mwenye anaweza kulinganishwa na Yehova?+
Ni nani kati ya wana wa Mungu+ mwenye kuwa kama Yehova?
7 Mungu ni mwenye kuogopwa sana katika baraza la* watakatifu;+
Yeye ni mukubwa na mwenye kuogopesha sana kwa wote wenye kumuzunguka.+
8 Ee Yehova Mungu wa majeshi,
Ni nani mwenye kuwa na nguvu kama wewe, Ee Yah?+
Uaminifu wako unakuzunguka.+
10 Umemuponda Rahabu+ kama mutu mwenye aliuawa.+
Kwa mukono wako wenye nguvu umesambaza maadui wako.+
14 Uadilifu* na haki ndio musingi wa kiti chako cha ufalme;+
Upendo mushikamanifu na uaminifu vinasimama mbele yako.+
15 Wenye furaha ni watu wenye wanajua vigelegele vya shangwe.+
Ee Yehova, wanatembea katika mwangaza wa uso wako.
16 Wanashangilia katika jina lako muchana wote,
Na katika haki yako wanainuliwa.
18 Kwa maana ngao yetu ni ya Yehova,
Mufalme wetu ni wa Mutakatifu wa Israeli.+
19 Wakati huo uliambia washikamanifu wako katika maono na kusema:
21 Mukono wangu utamutegemeza,+
Na mukono wangu utamutia nguvu.
22 Hakuna adui mwenye atamulipisha ushuru,
Na hakuna mwenye haiko mwenye haki mwenye atamukandamiza.+
23 Nitavunja maadui wake vipande-vipande ili wasikuwe tena mbele yake+
Na nitapiga na kuua wale wenye kumuchukia.+
24 Uaminifu wangu na upendo wangu mushikamanifu viko pamoja naye,+
Na katika jina langu nguvu zake zitainuliwa.*
26 Ataniambia kwa sauti: ‘Wewe ni Baba yangu,
Mungu wangu na Mwamba wa wokovu wangu.’+
28 Nitadumisha upendo wangu mushikamanifu kwa ajili yake milele,+
Na agano langu lenye nilifanya pamoja naye halitavunjika hata siku moja.+
30 Kama wana wake wanaacha sheria yangu
Na hawatembee kulingana na maagizo yangu,*
31 Kama wanavunja sheria zangu
Na hawashike amri zangu,
32 Basi nitapatia azabu kukosa kutii kwao* kwa kutumia fimbo+
Na kosa lao kwa kutumia viboko.
33 Lakini sitaacha hata kidogo kumutendea kwa upendo wangu mushikamanifu+
Wala sitakosa kutimiza ahadi yangu.*
35 Nimeapa katika utakatifu wangu, mara moja kwa wakati wote;
Sitamuambia Daudi uongo.+
37 Kama mwezi, kitafanywa kuwa imara kabisa milele
Kama shahidi muaminifu katika anga.” (Sela)
38 Lakini wewe mwenyewe umemutupa mbali na kumukataa;+
Umemukasirikia sana mutiwa-mafuta wako.
39 Umekataa kwa zarau agano lenye ulifanya na mutumishi wako;
Umechafua taji lake kwa kulitupa chini.
40 Umebomoa kuta zake zote za majiwe;*
Umefanya ngome yake kuwa mabomoko.
41 Wote wenye kupita karibu naye wamenyanganya vitu vyake;
Yeye ni kitu cha haya kwa majirani wake.+
43 Pia umesukumia upanga wake nyuma,
Na umemufanya asishinde katika vita.
44 Umekomesha utukufu wake
Na umetupa chini kiti chake cha ufalme.
45 Umefupisha siku za ujana wake;
Umemuvalisha haya. (Sela)
46 Ee Yehova, utaendelea kujificha mupaka wakati gani? Utajificha milele?+
Je, kasirani yako kali itaendelea kuwaka kama moto?
47 Kumbuka namna maisha yangu ni mafupi sana!+
Je, uliumba wanadamu wote bila kusudi?
48 Ni mwanadamu gani anaweza kuishi na asikufe hata siku moja?+
Je, anaweza kujiokoa* katika nguvu za Kaburi?* (Sela)
49 Yako wapi matendo yako ya zamani ya upendo mushikamanifu, Ee Yehova,
Yenye ulimuapia Daudi katika uaminifu wako?+
50 Kumbuka, Ee Yehova, zihaka zenye zilitupwa juu ya watumishi wako;
Namna ninalazimika kuvumilia* zihaka za vikundi vyote vya watu;
51 Namna maadui wako wametupa matusi, Ee Yehova;
Namna wametukana kila hatua ya mutiwa-mafuta wako.
52 Yehova asifiwe milele. Amina na Amina.+