Zaburi
118 Mumushukuru Yehova, kwa maana yeye ni mwema;+
Upendo wake mushikamanifu unadumu milele.
2 Israeli aseme sasa:
“Upendo wake mushikamanifu unadumu milele.”
3 Watu wa nyumba ya Haruni waseme sasa:
“Upendo wake mushikamanifu unadumu milele.”
4 Wale wenye kumuogopa Yehova waseme sasa:
“Upendo wake mushikamanifu unadumu milele.”
6 Yehova iko* upande wangu; sitaogopa.+
Mwanadamu anaweza kunifanya nini?+
7 Yehova iko* upande wangu akiwa musaidizi wangu;*+
Nitaangalia kwa furaha kushindwa kwa wale wenye kunichukia.+
8 Ni muzuri kumukimbilia Yehova
Kuliko kutegemea wanadamu.+
9 Ni muzuri kumukimbilia Yehova
Kuliko kutegemea wakubwa.+
11 Yalinizunguka, ndiyo, yalinizunguka kabisa,
Lakini katika jina la Yehova,
Niliyafukuza.
12 Yalinizunguka kama nyuki,
Lakini yalizimwa haraka kama moto kati ya miiba.
Katika jina la Yehova,
Niliyafukuza.+
13 Nilisukumwa kwa nguvu* ili nianguke,
Lakini Yehova alinisaidia.
14 Yah ni mahali pangu pa kujificha na nguvu zangu,
Na amekuwa wokovu wangu.+
15 Sauti ya shangwe na wokovu*
Iko katika mahema ya wenye haki.
Mukono wa kuume wa Yehova unaonyesha nguvu zake.+
16 Mukono wa kuume wa Yehova unajiinua;
Mukono wa kuume wa Yehova unaonyesha nguvu zake.+
17 Sitakufa, hapana, nitaishi,
Ili nitangaze kazi za Yah.+
19 Munifungulie milango mikubwa ya haki;+
Nitaingia ndani na kumusifu Yah.
20 Huu ni mulango mukubwa wa Yehova.
Wenye haki wataingia kupitia mulango huo.+
21 Nitakusifu, kwa maana ulinijibu+
Na ukakuwa wokovu wangu.
24 Hii ndiyo siku yenye Yehova amefanya;
Tutaifurahia na kuishangilia.
25 Yehova, utuokoe, tafazali, tunakulilia!
Yehova, utupatie ushindi, tafazali!
26 Amebarikiwa ule mwenye anakuja katika jina la Yehova;+
Tunakubariki kutoka katika nyumba ya Yehova.
27 Yehova ni Mungu;
Anatupatia mwangaza.+
28 Wewe ni Mungu wangu, na nitakusifu;
Mungu wangu, nitakutukuza.+