Zaburi
97 Yehova amekuwa Mufalme!+
Dunia ifurahi.+
Visiwa vingi vishangilie.+
2 Mawingu na giza nzito vinamuzunguka pande zote;+
4 Umeme wake wa radi unaangazia inchi;
Dunia inauona na kutetemeka.+
6 Mbingu zinatangaza haki yake,
Na vikundi vyote vya watu vinaona utukufu wake.+
7 Acha wale wote wenye kutumikia sanamu yoyote ya kuchongwa wapatishwe haya,+
Wale wenye kujisifu kuhusu miungu yao yenye haina mafaa yoyote.+
Mumuinamie,* ninyi miungu yote.+
9 Kwa maana wewe, Ee Yehova, ndiye Mwenye Kuwa Juu Zaidi, juu ya dunia yote;
Umeinuliwa juu zaidi kuliko miungu mingine yote.+
10 Enyi wenye kumupenda Yehova, muchukie mambo ya mubaya.+
11 Mwangaza umeangazia wenye haki+
Na shangwe imeangazia wale wenye kuwa wanyoofu katika moyo.
12 Mushangilie katika Yehova, ninyi wenye haki,
Na mushukuru jina lake takatifu.*