Kumbukumbu la Torati
18 “Makuhani Walawi, na kwa kweli kabila lote la Lawi, hawatapewa fungu wala uriti pamoja na Israeli. Watakula matoleo yenye yanatolewa kwa Yehova kwa njia ya moto, yenye ni uriti wake.+ 2 Kwa hiyo hawatakuwa na uriti katikati ya ndugu zao. Yehova ndiye uriti wao, kama vile amewaambia.
3 “Sasa hii ndiyo itakuwa haki ya makuhani kutoka kwa watu: Kila mutu mwenye anatoa zabihu, kama ni ngombe-dume ao kondoo, anapaswa kumupatia kuhani bega, mataya,* na tumbo. 4 Utamupatia matunda ya kwanza ya nafaka yako, divai yako mupya, mafuta yako, na manyoya ya kwanza ya kondoo yenye yalikatwa kwenye kundi lako.+ 5 Yehova Mungu wako amemuchagua yeye na wana wake katikati ya makabila yako yote ili kufanya utumishi katika jina la Yehova sikuzote.+
6 “Lakini kama Mulawi anatoka katika muji mumoja kati ya miji yako katika Israeli kwenye alikuwa anaishi+ na anatamani* kuenda mahali kwenye Yehova anachagua,*+ 7 anaweza kutumikia kule katika jina la Yehova Mungu wake sawasawa na ndugu zake wote, Walawi, wenye kusimama kule mbele ya Yehova.+ 8 Atapokea fungu lilelile la chakula pamoja nao,+ zaidi ya malipo yenye anapata kisha kuuzisha vitu vya mababu zake.
9 “Wakati utakuwa umeingia katika inchi yenye Yehova Mungu wako anakupatia, haupaswe kujifunza kuiga mazoea yenye kuchukiza ya mataifa hayo.+ 10 Asipatikane katikati yako mutu yeyote mwenye kupitisha mutoto wake mwanaume ao mutoto wake mwanamuke katika moto,+ mutu yeyote mwenye kufanya uaguzi,+ mutu yeyote mwenye kufanya uchawi,+ mutu yeyote mwenye kutafuta alama za mambo yenye yatatokea,+ mulozi,+ 11 mutu yeyote mwenye anafunga wengine kwa uchawi, mutu yeyote mwenye anatafuta shauri kwa mutu mwenye kupashana habari na pepo wachafu+ ao mutu mwenye kutabiri matukio,+ ao mutu yeyote mwenye kuuliza habari kwa wafu.+ 12 Kwa maana kila mutu mwenye kufanya mambo hayo ni chukizo kwa Yehova, na kwa sababu ya mazoea hayo yenye kuchukiza, Yehova Mungu wako anafukuza mataifa hayo mbele yako. 13 Utajionyesha kuwa bila lawama mbele ya Yehova Mungu wako.+
14 “Kwa maana mataifa haya yenye unakamata inchi yao yalizoea kusikiliza wale wenye kufanya uchawi+ na uaguzi,+ lakini Yehova Mungu wako hakukuruhusu kufanya jambo lolote kama hilo. 15 Yehova Mungu wako atakuinulia nabii kama mimi kati ya ndugu zako. Unapaswa kumusikiliza. + 16 Hilo ndilo jibu kwa mambo yenye ulimuomba Yehova Mungu wako kule Horebu katika siku ya mukusanyiko,*+ wakati ulisema, ‘Usiache nisikie sauti ya Yehova Mungu wangu ao kuona tena moto huu mukubwa, ili nisikufe.’+ 17 Kisha Yehova akaniambia, ‘Jambo lenye wamesema ni sawa. 18 Nitawainulia nabii kama wewe+ katikati ya ndugu zao, na nitatia maneno yangu katika kinywa chake,+ na atawaambia mambo yote yenye nitamuamuru.+ 19 Kwa kweli, nitamuomba hesabu kila mutu mwenye hatasikiliza maneno yangu yenye nabii huyo atasema katika jina langu.+
20 “Kama nabii yeyote anasema kwa kimbelembele katika jina langu neno lenye sikumuamuru aseme ao anasema katika jina la miungu mingine, nabii huyo anapaswa kufa.+ 21 Lakini, unaweza kusema katika moyo wako: “Namna gani tutajua kama Yehova hakusema neno hilo?” 22 Wakati nabii anasema neno katika jina la Yehova na neno hilo halitimie ao halifanyike, basi Yehova hakusema neno hilo. Nabii huyo alilisema kwa kimbelembele. Haupaswe kumuogopa.’