Zaburi
Kwa kiongozi; Ya Yedutuni.* Muziki wa Daudi.
62 Kwa kweli, ninamungojea* Mungu kimya-kimya.
Wokovu wangu unatoka kwake.+
2 Kwa kweli, yeye ni mwamba wangu na wokovu wangu, kimbilio langu salama;*+
Sitatikiswa sana hata kidogo.+
3 Mutaendelea mupaka wakati gani kumushambulia mutu ili kumuua?+
Ninyi wote muko hatari kama ukuta wenye kuinama, ukuta wa majiwe wenye unakaribia kuanguka.*
4 Kwa maana wanafanya shauri pamoja ili kumuangusha kutoka kwenye cheo chake cha juu;*
Wanafurahia kusema uongo.
Kwa kinywa chao wanabariki, lakini ndani yao wanalaani.+ (Sela)
6 Kwa kweli, yeye ni mwamba wangu na wokovu wangu, kimbilio langu salama;
Sitatikiswa hata kidogo.+
7 Wokovu wangu na utukufu wangu unamutegemea Mungu.
Mwamba wangu wenye nguvu, kimbilio langu, ni Mungu.+
8 Mumutegemee nyakati zote, Enyi watu.
Mumwange mioyo yenu mbele yake.+
Mungu ni kimbilio letu.+ (Sela)
9 Wana wa binadamu ni pumuzi tu,
Wana wa wanadamu ni udanganyifu.+
Wakati wanatiwa pamoja kwenye mizani,* ni wepesi kuliko pumuzi tu.+
10 Musitegemee upunjaji
Wala kuwa na matumaini ya uongo katika unyanganyi.
Kama mali zenu zinaongezeka, musiweke moyo wenu juu ya mali hizo.+
11 Mungu amezungumuza mara moja, mara mbili nimesikia jambo hili:
Kwamba nguvu ni za Mungu.+