Waamuzi
15 Kisha wakati fulani, katika siku za mavuno ya ngano, Samsoni akaenda kumutembelea bibi yake na akapeleka mwana-mbuzi. Akasema: “Ninataka kuingia kwa bibi yangu katika chumba cha kulala.”* Lakini baba ya mwanamuke huyo hakumuruhusu kuingia. 2 Baba ya mwanamuke huyo akasema: “Niliwaza, ‘Unamuchukia kabisa.’+ Kwa hiyo nikamupatia mumoja wa marafiki wako mwanamuke huyo.+ Je, dada yake mudogo haiko mwenye sura na umbo ya muzuri kuliko yeye? Tafazali, umuchukue huyo pa nafasi yake.” 3 Lakini, Samsoni akawaambia: “Wakati huu Wafilisti hawatanilaumu ikiwa ninawaumiza.”
4 Basi Samsoni akaenda na kukamata mbweha mia tatu (300). Kisha akakamata mienge, akafunga mikia ya mbweha wawili-wawili na kuweka mwenge mumoja katikati ya kila mikia mbili. 5 Kisha akawasha moto ile mienge na kupeleka mbweha hao katika mashamba ya Wafilisti ya nafaka yenye kusimama. Basi akateketeza kila kitu kuanzia fungu la nafaka mupaka mashamba ya nafaka, na pia mashamba ya mizabibu na ya mizeituni.
6 Wafilisti wakauliza: “Ni nani alifanya hivi?” Wakaambiwa: “Ni Samsoni, mwana-mukwe wa ule Mutimna, kwa sababu alichukua bibi ya Samsoni na kumupatia mumoja wa marafiki wake.”+ Kwa hiyo Wafilisti wakaenda kuteketeza mwanamuke huyo na baba yake kwa moto.+ 7 Kisha Samsoni akawaambia: “Kama ni hivi munazoea kufanya, sitaondoka mupaka nilipize kisasi juu yenu.”+ 8 Basi akapiga na kuua Wafilisti wengi sana, mumoja kisha mwingine,* kisha akashuka na kukaa katika pango* ndani ya mwamba wa Etamu.
9 Kisha wakati fulani Wafilisti wakapanda na kupiga kambi katika Yuda na walikuwa wanatembea-tembea katika Lehi.+ 10 Basi watu wa Yuda wakauliza: “Sababu gani mumepanda ili kutushambulia?” wakajibu: “Tumepanda ili kumukamata* Samsoni, na kumutendea kama vile alitutendea.” 11 Kwa hiyo watu elfu tatu (3 000) wa Yuda wakaenda kwenye pango la* mwamba wa Etamu, wakamuuliza Samsoni: “Je, haujue kwamba Wafilisti wanatutawala?+ Sasa sababu gani umetutendea hivi?” Akawajibu: “Nimewatendea wao kama vile walinitendea.” 12 Lakini wakamuambia: “Tumekuja kukukamata* ili tukutie katika mukono wa Wafilisti.” Samsoni akawaambia: “Muniapie kwamba ninyi wenyewe hamutanishambulia.” 13 Wakamuambia: “Hapana, tutakufunga tu na kukutia katika mukono wao, lakini hatutakuua.”
Basi wakamufunga kwa kamba mbili za mupya na kumupeleka inje ya ule mwamba. 14 Wakati alifika Lehi, Wafilisti wakafanya makelele ya ushindi kwa kumuona. Kisha roho ya Yehova ikamutia nguvu,+ na kamba zenye zilifungwa kwenye mikono yake zikakuwa kama nyuzi za kitani zenye kuunguzwa kwa moto, na pingu zake zikayeyuka kutoka kwenye mikono yake.+ 15 Akaona mufupa wa mubichi wa taya* ya punda-dume; akaukaribia na kuukamata na akautumia kupiga na kuua watu elfu moja (1 000).+ 16 Kisha Samsoni akasema:
“Kwa mufupa wa taya* ya punda—rundo moja, marundo mbili!
Kwa mufupa wa taya ya punda nimepiga na kuua watu elfu moja (1 000).”+
17 Wakati alimaliza kusema, akatupa ule mufupa wa taya* na kuita mahali pale Ramat-lehi.*+ 18 Kisha akasikia kiu sana, na akamuitia Yehova na kusema: “Ni wewe ulitia wokovu huu mukubwa katika mukono wa mutumishi wako. Lakini sasa, je, nikufe na kiu na je, nianguke katika mikono ya watu wenye hawatahiriwe?” 19 Basi Mungu akapasua shimo lenye lilikuwa katika Lehi, na maji yakatoka.+ Wakati alikunywa, roho* yake ikamurudia na akakuwa tena na nguvu. Ndiyo sababu aliita mahali pale En-hakore,* na mahali pale panapatikana Lehi mupaka leo.
20 Na alihukumu Israeli katika siku za Wafilisti kwa miaka makumi mbili (20).+