Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w17 Mwezi wa 9 uku. 23-27
  • ‘Neno la Mungu . . . Liko na Nguvu’

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • ‘Neno la Mungu . . . Liko na Nguvu’
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2017
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • KATIKA MAISHA YETU
  • KATIKA KAZI YA KUHUBIRI
  • WAKATI UNAFUNDISHA KWENYE JUKWAA
  • Mambo ya Kufanya juu Ufaidike na Usomaji Wako wa Biblia
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
  • Namna ya Kufaidika Kabisa na Usomaji wa Biblia
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Tumia Nguvu za Neno la Mungu Katika Mahubiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2015
  • Uwe Mwenye Kusadikisha Unapofundisha
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2017
w17 Mwezi wa 9 uku. 23-27
Mwanaume mumoja anakaa yeye mwenyewe na anakunywa pombe; Mashahidi wa Yehova wanafika kwenye mulango wake na kumuhubiria; mwanaume huyo anakuja kwenye mikutano

‘Neno la Mungu . . . Liko na Nguvu’

‘Neno la Mungu liko hai nalo liko na nguvu.’​—EBR. 4:12.

NYIMBO: 114, 113

NAMNA GANI UNAWEZA KUACHA NGUVU YA NENO LA MUNGU IFANYE KAZI . . .

  • katika maisha yako?

  • katika kazi ya kuhubiri?

  • wakati unafundisha kwenye jukwaa?

1. Sababu gani unaweza kuwa hakika kuwa Neno la Mungu liko na nguvu? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

SISI watu wa Yehova, tuko hakika kuwa Neno la Mungu, ujumbe wake kwa wanadamu, ‘liko hai nalo liko na nguvu.’ (Ebr. 4:12) Wengi wetu wamejionea katika maisha yao namna Biblia iko na uwezo wa kubadilisha maisha. Zamani, ndugu na dada fulani walikuwa wezi, watumwa wa dawa za kulewesha, ao waasherati. Kwa kadiri fulani wengine walikuwa na maisha mazuri katika ulimwengu huu lakini walijisikia kuwa walikuwa wanakosa kitu fulani katika maisha yao. (Mhu. 2:3-11) Mara kwa mara, watu wenye walionekana kuwa hawana tumaini wamepata njia ya uzima kwa musaada wa nguvu ya Biblia yenye kubadilisha maisha. Pengine umesoma na kufurahia sana mifano mingi kama hiyo yenye kuchapishwa katika Munara wa Mulinzi katika habari zenye kichwa “Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu.” Na umeona kuwa hata kisha kukubali kweli, Maandiko yanaendelea kusaidia Wakristo kufanya maendeleo ya kiroho.

2. Nguvu ya Neno la Mungu ilionekana namna gani wakati wa mitume?

2 Tunapaswa kushangaa kuwa wengi katika siku zetu wamefanya mabadiliko makubwa kwa sababu walijifunza Neno la Mungu? Hapana kabisa! Mifano hiyo inatukumbusha ndugu na dada zetu wa wakati wa mitume wenye walikuwa na tumaini la kuishi mbinguni. (Soma 1 Wakorintho 6:9-11.) Kisha kutaja aina ya watu wenye hawatariti Ufalme wa Mungu, mutume Paulo aliongezea hivi: ‘Wengine wenu mulikuwa hivyo.’ Lakini walikuwa wamefanya mabadiliko kwa musaada wa Maandiko na roho takatifu ya Mungu. Hata kisha kukubali kweli, wamoja walipaswa kuachana na matendo fulani ya mubaya yenye haipatane na Maandiko. Biblia inazungumuzia Mukristo mumoja mutiwa-mafuta wa wakati wa mitume mwenye alipaswa kutengwa na kutaniko; na kisha alirudishwa. (1 Kor. 5:1-5; 2 Kor. 2:5-8) Kwa kweli, tunatiwa moyo wakati tunafikiria magumu yenye Wakristo wenzetu wamepambana nayo na yenye wameshinda kwa musaada wa Neno la Mungu.

3. Tutazungumuzia nini katika habari hii?

3 Kwa sababu Neno la Mungu ni chombo chenye nguvu na tuko na chombo hicho, tunapenda kuhakikisha kuwa tunalitumia muzuri zaidi. (2 Tim. 2:15) Kwa hiyo, katika habari hii, tutazungumuzia namna gani tunaweza kuacha nguvu ya Neno la Mungu ifanye kazi kabisa (1) katika maisha yetu, (2) katika kazi yetu ya kuhubiri, na (3) wakati tunafundisha kwenye jukwaa. Vikumbusho hivyo vitatusaidia tuonyeshe upendo na shukrani yetu kwa Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo, mwenye kutufundisha kwa faida yetu.​—Isa. 48:17.

KATIKA MAISHA YETU

4. (a) Tunapaswa kufanya nini ili Neno la Mungu litende katika maisha yetu? (b) Namna gani unapata wakati wa kusoma Biblia?

4 Ili Neno la Mungu litende katika maisha yetu, tunapaswa kulisoma kwa ukawaida; na ikiwa inawezekana tulisome kila siku. (Yos. 1:8) Kwa kweli, wengi kati yetu wako na mambo mengi ya kufanya katika maisha. Hata hivyo, hatupaswe kuruhusu jambo lolote, hata madaraka yetu ya lazima, yatufanye tusiheshimie programu yetu ya kusoma Biblia. (Soma Waefeso 5:15, 16.) Wengi kati ya watu wa Yehova wanajikaza kupata wakati wa kusoma Biblia kila siku, iwe asubuhi ao mangaribi ao wakati mwingine. Wanajisikia kama muandikaji mumoja wa zaburi mwenye aliandika hivi: ‘Jinsi ninavyoipenda sheria yako! Ndiyo ninaihangaikia muchana kutwa.’​—Zab. 119:97.

5, 6. (a) Sababu gani ni jambo la maana kutafakari? (b) Namna gani tunaweza kutafakari kwa njia yenye kuleta matokeo? (c) Kusoma na kutafakari juu ya Neno la Mungu kumekuletea faida gani?

5 Zaidi ya kusoma Biblia, ni jambo la maana tutafakari ao kufikiri sana juu ya mambo yenye tunasoma. (Zab. 1:1-3) Ikiwa tunafanya hivyo, tutaweza kutumikisha muzuri zaidi katika maisha yetu hekima yake yenye faida sikuzote. Iwe tunasoma Neno la Mungu lenye kuchapishwa ao kwenye vyombo vya kielektronike, kusudi letu linapaswa kuwa kuchukua maandiko ya Biblia na kuyaweka katika moyo wetu.

Shahidi mumoja wa Yehova anasoma Biblia

6 Namna gani tunaweza kutafakari kwa njia yenye kuleta matokeo? Wengi wameona kuwa wakati wanamaliza kusoma sehemu fulani ya Maandiko ni muzuri kujiuliza maulizo kama haya: ‘Habari hii inanifundisha nini juu ya Yehova? Ni katika njia gani nimeanza kutumia katika maisha yangu kanuni hii yenye kupatikana katika sehemu hii ya Neno la Mungu? Ni mambo gani ninaweza kufanyia maendeleo?’ Wakati tunatafakari juu ya Neno la Mungu na kusali, tutachochewa hata zaidi kutumia mashauri yake. Kwa hiyo, nguvu ya Neno la Mungu itatenda zaidi katika maisha yetu.​—2 Kor. 10:4, 5.

KATIKA KAZI YA KUHUBIRI

7. Namna gani tunaweza kutumia muzuri Neno la Mungu katika kazi yetu ya kuhubiri?

7 Ni nini inaweza kutusaidia tutumie muzuri Neno la Mungu katika kazi yetu ya kuhubiri? Hatua ya kwanza ni kulitumia mara kwa mara wakati tunahubiri na kufundisha. Ndugu mumoja alisema hivi juu ya jambo hilo: “Ikiwa ungehubiri nyumba kwa nyumba pamoja na Yehova, ungezungumuza wewe mwenyewe ao ungemuacha azungumuze?” Alipenda kusema kuwa: Wakati tunasoma moja kwa moja Neno la Mungu katika kazi ya kuhubiri, tunamuacha Yehova azungumuze na mwenye nyumba. Andiko lenye kuchaguliwa muzuri, linaweza kuwa na nguvu zaidi kuliko jambo lolote lenye tunaweza kusema. (1 Tes. 2:13) Ujiulize hivi: ‘Ninajikaza kabisa kutumia kila nafasi yenye kujitokeza ili kusomea Neno la Mungu watu wenye ninahubiria habari njema?’

8. Wakati tunahubiri, sababu gani haitoshe kusoma tu andiko?

8 Kwa kweli, zaidi ya kusomea tu Biblia wale wenye tunazungumuza nao, tunapaswa kufanya mambo mengine. Sababu gani? Kwa sababu wengi hawajue mambo mengi ao hawajue kitu juu ya Biblia. Ilikuwa hivyo wakati wa mitume, na ni hivyo leo pia. (Rom. 10:2) Kwa hiyo, hatupaswe kufikiri kuwa mutu ataelewa wazo kubwa la andiko kwa sababu tu tunalisoma. Tunapaswa kukazia sehemu fulani za andiko, pengine kwa kurudilia maneno yenye kukazia wazo kubwa, na kufasiria maana ya maneno hayo. Ikiwa tunafanya hivyo, hilo linaweza kufanya ujumbe wa Neno la Mungu uguse akili na mioyo ya wasikilizaji wetu.​—Soma Luka 24:32.

9. Namna gani tunaweza kutanguliza maandiko katika njia yenye kufanya watu waheshimie Biblia? Toa mufano.

9 Ni muzuri pia kutanguliza maandiko katika njia yenye kufanya watu waheshimie Biblia. Kwa mufano, tunaweza kusema hivi: “Tuone Muumbaji wetu anasema nini juu ya habari hii.” Wakati tunazungumuza na mutu mwenye hajue mafundisho ya Kikristo, tunaweza kusema hivi: “Ona mambo yenye Maandishi Matakatifu yanasema.” Ao ikiwa tunahubiria mutu fulani mwenye hapendezwe na mambo ya dini, tunaweza kumuuliza hivi: “Umekwisha kusikia mezali hii ya zamani?” Kwa kweli, tunapaswa kufikiria hali ya kila mutu na kupatanisha utangulizi wetu na hali yake.​—1 Kor. 9:22, 23.

Mashahidi wa Yehova wanatumia Biblia katika kazi ya kuhubiri

10. (a) Ndugu mumoja alijionea jambo gani? Eleza. (b) Namna gani umejionea nguvu ya Neno la Mungu katika kazi yako ya kuhubiri?

10 Wengi wametambua kuwa kutumia Neno la Mungu katika kazi ya kuhubiri kunaweza kugusa sana moyo watu wenye wanahubiria. Fikiria mufano huu. Ndugu mumoja alirudilia mwanaume mumoja mwenye kuzeeka mwenye alikuwa amesoma magazeti yetu kwa miaka mingi. Kuliko kumutolea tu gazeti la Munara wa Mulinzi la hivi karibuni, ndugu huyo aliamua kusoma andiko fulani lenye lilikuwa katika gazeti hilo. Alisoma 2 Wakorintho 1:3, 4, lenye kusema hivi: ‘Baba ya rehema nyororo na Mungu wa faraja yote . . . anatufariji katika ziki yetu yote.’ Maneno hayo yaligusa sana moyo wa mwenye nyumba huyo na akaambia ndugu asome tena andiko hilo mara ya pili. Mwanaume huyo alieleza namna yeye na bibi yake walikuwa na lazima ya faraja, na sasa anapendezwa na ujumbe wa Biblia. Kwa kweli, Neno la Mungu liko na nguvu katika kazi yetu ya kuhubiri.​—Mdo. 19:20.

WAKATI UNAFUNDISHA KWENYE JUKWAA

11. Ndugu wenye kufundisha kwenye jukwaa wako na daraka gani?

11 Sisi wote tunafurahia kuhuzuria mikutano yetu ya Kikristo na mikusanyiko yetu. Kwanza, tunahuzuria ili kumuabudu Yehova. Pia tunapata faida kubwa katika mafundisho ya kiroho yenye tunapata. Ndugu wenye kufundisha kwenye jukwaa wakati wa matukio hayo wako na pendeleo kubwa. Lakini, wanapaswa pia kuelewa kuwa wako na daraka kubwa. (Yak. 3:1) Sikuzote wanapaswa kuhakikisha kuwa mafundisho yao yanategemea kabisa Neno la Mungu. Ikiwa unapewa mugawo wa kufundisha kwenye jukwaa, namna gani unaweza kuacha nguvu ya Neno la Mungu ifanye kazi wakati unafundisha?

Ndugu anatumia Biblia ili kufundisha kwenye jukwaa

12. Namna gani musemaji anaweza kuhakikisha kuwa hotuba yake inategemea kabisa Maandiko?

12 Uhakikishe kuwa hotuba yako inategemea kabisa Maandiko. (Yoh. 7:16) Hilo linatia ndani nini? Kwanza, ukuwe mwangalifu ili mifano ao hata namna yako ya kufundisha isifanye watu wakose kukazia Maandiko ya Biblia yenye unatumia. Pia kumbuka kuwa kusoma tu Maandiko mengi, hakuonyeshe kuwa unafundisha kwa kutumia Biblia. Kwa kweli, ikiwa unasoma maandiko mengi, hilo linaweza kufanya wasikilizaji wasikumbuke hata andiko moja. Kwa hiyo, uchague kwa uangalifu maandiko ya musingi, na uchukue wakati wa kuyasoma, kuyafasiria, kutoa mufano, na kuonyesha namna ya kuyatumikisha. (Neh. 8:8) Ikiwa hotuba yako inategemea plan yenye kutolewa na tengenezo la Yehova, ujifunze plan na maandiko yenye kutolewa. Ujikaze kuelewa upatano wenye kuwa kati ya maelezo yenye kupatikana kwenye plan ya hotuba na maandiko yenye kutajwa. Tumia maandiko yenye yamechaguliwa ili kufundisha mawazo makubwa yenye kupatikana kwenye plan ya hotuba. (Unaweza kupata mashauri yenye kufaa katika somo la 21 mupaka la 23 la kitabu Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi.) Zaidi ya yote, umuombe Yehova musaada katika sala ili ufundishe mawazo ya maana yenye kupatikana katika Neno lake.​—Soma Ezra 7:10; Methali 3:13, 14.

13. (a) Namna gani dada mumoja aliguswa moyo na Maandiko kwenye mikutano ya Kikristo? (b) Namna Maandiko yanatumiwa kwenye mikutano yetu imekuletea faida gani?

13 Dada mumoja katika Australia aliguswa moyo sana juu ya namna maandiko yalitumiwa kwenye mikutano ya Kikristo. Hata kama aliteseka sana wakati alikuwa anakomaa, alikubali ujumbe wa Biblia na kutoa maisha yake kwa Yehova. Hata hivyo, alikuwa na magumu ya kukubali kuwa Yehova alikuwa anamupenda. Lakini, kisha wakati fulani, alifikia kuwa hakika kuwa Mungu anamupenda. Ni nini ilimusaidia akuwe na uhakika huo? Mabadiliko yalitokea wakati alitafakari juu ya andiko moja lenye lilitumiwa kwenye mikutano yetu na alilinganisha andiko hilo na maandiko mengine ya Biblia.a Umekwisha kuguswa pia na namna Neno la Mungu linatumiwa kwenye mikutano na mikusanyiko yetu?​—Neh. 8:12.

14. Namna gani tunaweza kuonyesha shukrani yetu juu ya Neno la Yehova?

14 Kwa kweli, tuko wenye shukrani sana kwa Neno la Yehova lenye kuandikwa, Biblia. Zaidi ya kulitolea wanadamu kwa upendo, alitimiza pia ahadi yake kwamba litadumu. (1 Pet. 1:24, 25) Kwa kweli, ni muzuri tusome Neno la Mungu kwa ukawaida, tulitumikishe katika maisha yetu, na kulitumikisha wakati tunasaidia wengine. Kwa kufanya hivyo tunaonyesha upendo wetu na shukrani kwa hazina hiyo yenye kutoka kwa Mungu, lakini zaidi sana kwa ule mwenye aliiandikisha, ni kusema, Yehova Mungu.

a Ona kisanduku “Mabadiliko Makubwa.”

UTUMIE NGUVU YA NENO LA MUNGU

katika maisha yako:

  • Ulisome kwa ukawaida

  • Utafakari juu ya mambo yenye unasoma

  • Utumikishe mambo yenye unajifunza

katika kazi ya kuhubiri:

  • Utumikishe Maandiko mara kwa mara

  • Kazia na kufasiria sehemu zenye kuonyesha mawazo makubwa ya andiko

  • Tanguliza maandiko katika njia yenye kuchochea watu waheshimie Neno la Mungu

wakati unafundisha kwenye jukwaa:

  • Ufanye hotuba yako itegemee kabisa Maandiko

  • Usiache mifano, ao namna yako ya kufundisha ifanye watu wakose kukazia Biblia

  • Uchukue wakati wa kufasiria, kutoa mufano, na kuonyesha namna ya kutumikisha maandiko yenye unasoma

“Mabadiliko Makubwa”

Kwa miaka mingi kisha kujifunza kweli, ilikuwa vigumu kwa Victoria kukubali kuwa Mungu angeweza kumupenda. Ni nini ilifikia kumusaidia aanze kuona kuwa Mungu anamupenda kabisa? Victoria anaeleza hivi:

“Mabadiliko makubwa yalitokea miaka 15 hivi kisha kubatizwa kwangu. Wakati hotuba ilikuwa inatolewa kwenye Jumba la Ufalme  . . . , musemaji alizungumuzia andiko la Yakobo 1:23, 24. Andiko hilo linafananisha Neno la Mungu na kioo yenye tunaweza kutumia ili kujiona namna Yehova anatuona. Nilianza kujiuliza ikiwa namna nilijiona ilitofautiana na namna Yehova aliniona. Mwanzoni, nilipinga mawazo hayo ya mupya. Niliendelea kujisikia kuwa sistahili kutumaini kuwa Yehova anaweza kunipenda.

“Kisha siku kidogo, nilisoma andiko lenye lilibadilisha maisha yangu. Andiko hilo ni Isaya 1:18, lenye kutaja maneno ya Yehova wakati anasema hivi: ‘Sasa, mukuje, nasi tunyooshe mambo kati yetu. . . . Hata zambi zenu zikiwa nyekundu, zitafanywa kuwa nyeupe kama teluji.’ Nilijisikia kuwa Yehova alikuwa ananiambia: ‘Kuja Vicky, tunyooshe mambo kati yetu. Ninakujua, ninajua zambi zako, ninajua moyo wako, na ninakupenda.’

“Sikuweza kulala usiku huo. Bado nilikuwa na mashaka ikiwa Yehova anaweza kunipenda, lakini nilianza kufikiria zabihu ya ukombozi ya Yesu. Mara moja nikakumbuka kwamba Yehova amekuwa akinivumilia kwa muda murefu na kunionyesha kwa njia nyingi sana kwamba ananipenda. Hata hivyo, ni kama vile nilikuwa ninamuambia hivi: ‘Upendo wako hautoshe ili kunifikia. Zabihu ya mwana wako haiwezi kufunika zambi zangu.’ Ni kama vile nilikuwa ninaikataa zabihu yenye Yehova ametoa. Lakini sasa, kisha kutafakari kuhusu zawadi hiyo ya zabihu ya ukombozi, nilianza kujisikia kuwa Yehova ananipenda.”

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine