MAISHA YA MUKRISTO
Ukuwe Kama Yosefu—Kimbia Uasherati
Yosefu alituachia mufano muzuri, kama tunashawishiwa kufanya uasherati. Kila mara wakati bibi ya mukubwa wake alikuwa anamushawishi, Yosefu alikataa. (Mwa 39:7-10) Alijibu hivi: “Ninaweza namna gani kufanya ubaya huu mukubwa na kwa kweli nimutendee Mungu zambi?” Ile jibu ilionyesha kama alielewa kwamba ni jambo la maana sana kwa Yehova ngono ikuwe tu kati ya bibi na bwana. Kisha, wakati ile jaribu ilikuwa nguvu, alikimbia kuliko kubakia pale na kuruhusu ule mwanamuke aregeze azimio lake la kufanya mambo yenye kuwa sawa.—Mwa 39:12; 1Ko 6:18.
MUANGALIE VIDEO KIMBIA UASHERATI, NA KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:
Jin alijikuta katika hali gani?
Jin alijiuliza maulizo gani yenye kuonyesha utambuzi wakati Mee-Kyong alimuomba amusaidie katika somo la hesabu la kufanya ku nyumba?
Ombi la Mee-Kyong lilifanya Jin ajisikie namna gani?
Namna gani Jin alipata musaada?
Jin alifanya nini ili kukimbia uasherati?
Umejifunza mambo gani mu hii video?