TAREHE 18-24/8
MEZALI 27
Wimbo 102 na Sala | Maneno ya Utangulizi (Dak. 1)
1. Namna Barafiki Bazuri Banatusaidiaka
(Dak. 10)
Rafiki muzuri haogopake kutushauria wakati tuko na lazima ya mashauri (Mez 27:5, 6; w19.09 uku. 5 fu. 12)
Rafiki muzuri anaweza kutusaidia kushindia hata ndugu wa mu familia (Mez 27:10; it-2 uku. 669 fu. 7)
Rafiki muzuri anaweza kutusaidia tukuwe batu bazuri zaidi (Mez 27:17; w23.09 uku. 9 fu. 7)
2. Mali ya Kiroho
(Dak. 10)
Mez 27:21—Namna tunatenda wakati banatusifu inaweza kuonyesha kama tuko batu ba namna gani? (w06 15/9 uku. 19 fu. 12)
Mu usomaji wa Biblia wa hii juma, ulipata mali gani ya kiroho yenye ungependa kuzungumuzia?
3. Usomaji wa Biblia
(Dak. 4) Mez 27:1-17 (th somo ya 5)
4. Kuanzisha Mazungumuzo
(Dak. 3) NYUMBA KWA NYUMBA. Mwenye-nyumba haiko mu dini ya Kikristo. (lmd somo ya 6 nukta ya 5)
5. Kuendelesha Mazungumuzo
(Dak. 4) MAHUBIRI YA WAKATI WOWOTE. Tumikisha video moya ya mu Byombo bya Kufundishia. (lmd somo ya 8 nukta ya 3)
6. Hotuba
(Dak. 5) ijwyp-SW habari ya 75—Kichwa: Nifanye Nini Kama Rafiki Yangu Ananikosea? (th somo ya 14)
Wimbo 109
7. “Ndugu Mwenye Amezaliwa kwa Ajili ya Nyakati za Taabu”
(Dak. 15) Mazungumuzo.
Yehova ametupatia familia ya bandugu na badada mu dunia yote. Mu ile familia, tunaweza kupata barafiki benye kutupenda. Ni kweli kama uko na barafiki ba mingi mu kutaniko, lakini bangapi njo barafiki yako ba karibu? Juu ukuwe na burafiki ya nguvu na mutu fulani, munapaswa kujuana muzuri, kutumainiana, kukuwa naambiana mambo yenye iko mu moyo, kufanya mambo fulani pamoya, na kusaidiana. Njo maana kuanzisha na kuendelesha burafiki inaombaka wakati na kujikaza.
Musome Mezali 17:17. Kisha uliza basikilizaji:
Juu ya nini ni muzuri tujikaze kukuwa na barafiki ba karibu kuanzia sasa mbele taabu kubwa ianze?
Musome 2 Wakorinto 6:12, 13. Kisha uliza basikilizaji:
Namna gani hii andiko inaweza kutusaidia tupate barafiki?
Muangalie VIDEO “Kila Kitu Kiko na Wakati Wake Wenye Uliwekwa”—Inaomba Wakati Juu ya Kukomalisha Urafiki. Kisha uliza basikilizaji:
Hii video inakufundisha nini kuhusu burafiki?
Kukomalisha burafiki iko sawa vile kukomalisha mumea. Kuonyesha mutu sura ya kicheko ao kumusalimia kwa uchangamufu iko sawa vile kupanda mbegu. Na kumuhangaikia kabisa iko sawa vile kumwangilia mayi. Vile tu kukomalisha mumea inaombaka wakati ni vile kuanzisha burafiki inaombaka pia wakati. Njo maana, mukuwe bavumilivu na muache burafiki yenu ikomale vile muko napitisha wakati pamoya. Mukifanya vile, burafiki yenu inaweza kuendelea milele.
8. Funzo ya Biblia ya Kutaniko
(Dak. 30) lfb somo ya 10-11