TAREHE 22-28/9
MUHUBIRI 1-2
Wimbo 103 na Sala | Maneno ya Utangulizi (Dak. 1)
1. Endelea Kuzoeza Kizazi ya Kufuata
(Dak. 10)
[Muangalie VIDEO Utangulizi wa Kitabu cha Mhubiri.]
Kila kizazi iko na daraka ya kuzoeza kizazi ya kufuata (Muh 1:4; w17.01 uku. 27-28 fu. 3-4)
Wakati tunazoeza bengine na kubapatia kazi ya kufanya, tunabaachia pia nafasi ya kupata furaha ya kumutumikia Yehova kwa bidii (Muh 2:24)
Usisite kuzoeza bengine juu tu uko nawaza kama ukibazoeza batafikia kukamata madaraka yenye uko nayo
2. Mali ya Kiroho
(Dak. 10)
Muh 1:1—Biblia inamaanisha nini wakati inasema kama Sulemani alikuwa “mukutanishaji”? (it-F “Ecclésiaste” fu. 1)
Mu usomaji wa Biblia wa hii juma, ulipata mali gani ya kiroho yenye ungependa kuzungumuzia?
3. Usomaji wa Biblia
(Dak. 4) Muh 1:1-18 (th somo ya 11)
4. Kuanzisha Mazungumuzo
(Dak. 2) MAHUBIRI YA WAKATI WOWOTE. Ujikaze kujua habari yenye inamufurahisha mutu. Mupange juu ya kuongea tena siku ingine. (lmd somo ya 3 nukta ya 5)
5. Kuanzisha Mazungumuzo
(Dak. 2) MAHUBIRI YA MAHALI PA WATU WENGI. Zungumuzia kweli moya kati ya “Kweli Zenye Tunapendaka Kufundisha,” kwa kufuata pendekezo yenye kuwa mu fungu ya kwanza ya nyongeza ya A ya broshua Penda Watu. (lmd somo ya 2 nukta ya 3)
6. Kuendelesha Mazungumuzo
(Dak. 2) MAHUBIRI YA WAKATI WOWOTE. Jibia ulizo yenye mutu alikuulizaka mu mazungumuzo ya mbele. (lmd somo ya 9 nukta ya 5)
7. Kufanya Banafunzi
(Dak. 5) MAHUBIRI YA MAHALI PA WATU WENGI. Onyesha mutu namna tunajifunzaka Biblia na batu, na mupange juu ya kuendelesha funzo. (lmd somo ya 10 nukta ya 3)
Wimbo 84
8. Mambo Tatu ya Maana Kuhusu Kuzoeza Bengine
(Dak. 15) Mazungumuzo.
Upendo njo unatuchocheaka kuzoeza bengine juu bafikie kutimiza kazi yenye Yehova alituomba tufanye
Mu Biblia, muko mifano mingi ya muzuri sana yenye inatufundisha namna ya kuzoeza bengine. Kwa mufano, tunaweza kujifunza mambo mingi kupitia namna Samweli alizoeza Sauli, namna Eliya alizoeza Elisha, namna Yesu alizoeza banafunzi yake, na namna Paulo alizoeza Timoteo. Hatuwezi kusahau kutaya Yehova mwenye anajuaka kuzoeza muzuri zaidi. Mufano wake unaweza kutufundisha nini?
Muangalie VIDEO Uzoeze Bengine Sawa Yehova—Sehemu. Kisha uliza basikilizaji:
Namna Yehova anakuwaka nazoeza bengine inatufundisha mambo gani tatu?
9. Funzo ya Biblia ya Kutaniko
(Dak. 30) lfb somo ya 20-21