TAREHE 3-9/11
WIMBO WA SULEMANI 1-2
Wimbo 132 na Sala | Maneno ya Utangulizi (Dak. 1)
1. Habari Juu ya Upendo wa Kweli
(Dak. 10)
[Muangalie VIDEO Utangulizi wa Wimbo wa Sulemani.]
Sulemani alimusifu sana kijana mwanamuke Mushulami na alimuahidi kumupatia mazawadi ya mingi (Wim 1:9-11)
Mwanamuke Mushulami alikuwa napenda kwelikweli mupenzi wake mwenye alikuwa muchungaji, na ile njo ilimusaidiaka abakie mushikamanifu kwake (Wim 2:16, 17; w15 15/1 uku. 30 fu. 9-10)
SHAURI: Wakati uko nasoma kitabu ya Wimbo wa Sulemani, tumia sehemu “Habari Zenye Kuwa Ndani” yenye iko mu Tafsiri ya Ulimwengu Mupya, juu ya kuelewa nani njo iko nasema.
2. Mali ya Kiroho
(Dak. 10)
Wim 2:7—Mufano wa kijana mwanamuke Mushulami unaweza kufundisha nini Bakristo benye habayafunga ndoa? (w15 15/1 uku. 31 fu. 11)
Mu usomaji wa Biblia wa hii juma, ulipata mali gani ya kiroho yenye ungependa kuzungumuzia?
3. Usomaji wa Biblia
(Dak. 4) Wim 2:1-17 (th somo ya 12)
4. Kuanzisha Mazungumuzo
(Dak. 3) NYUMBA KWA NYUMBA. Zungumuzia kweli moya yenye kuwa mu nyongeza ya A ya broshua Penda Watu. (lmd somo ya 1 nukta ya 3)
5. Kuendelesha Mazungumuzo
(Dak. 4) NYUMBA KWA NYUMBA. Zungumuzia kweli moya yenye kuwa mu nyongeza ya A ya broshua Penda Watu. (lmd somo ya 9 nukta ya 3)
6. Kufanya Banafunzi
Wimbo 46
7. “Mutu Mukarimu Atabarikiwa”
(Dak. 15) Mazungumuzo. Itolewe na muzee.
Kama tunatumia wakati yetu, nguvu yetu na bitu byetu juu ya kusaidia bengine, tutabarikiwa sana. Ni kweli kama mutu mwenye tulisaidia atafurahi, lakini siye pia tutafurahi. (Mez 22:9) Tutafurahi juu tunajua kama tuko namuiga Yehova, na yeye atatukubali.—Mez 19:17; Yak 1:17.
Muangalie VIDEO Ukarimu Unaletaka Furaha. Kisha uliza basikilizaji:
Namna gani bandugu na badada ba mu hii video balipata furaha juu ya ukarimu wenye bandugu na badada ba mu dunia yote balibaonyesha?
Namna gani balipata pia furaha yenye inatokana na kuonyesha bengine ukarimu?
8. Funzo ya Biblia ya Kutaniko
(Dak. 30) lfb somo ya 32-33