Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwb25 Mwezi wa 11 uku. 2-3
  • Tarehe 3-9/11

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tarehe 3-9/11
  • Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2025
Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2025
mwb25 Mwezi wa 11 uku. 2-3

TAREHE 3-9/11

WIMBO WA SULEMANI 1-2

Wimbo 132 na Sala | Maneno ya Utangulizi (Dak. 1)

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU

1. Habari Juu ya Upendo wa Kweli

(Dak. 10)

[Muangalie VIDEO Utangulizi wa Wimbo wa Sulemani.]

Sulemani alimusifu sana kijana mwanamuke Mushulami na alimuahidi kumupatia mazawadi ya mingi (Wim 1:​9-11)

Mwanamuke Mushulami alikuwa napenda kwelikweli mupenzi wake mwenye alikuwa muchungaji, na ile njo ilimusaidiaka abakie mushikamanifu kwake (Wim 2:​16, 17; w15 15/1 uku. 30 fu. 9-10)

Mufalme Sulemani iko namualika Mushulami mu hema yake. Mwanamuke Mushulami anakatala, anamugeuzia Sulemani mugongo na anakunja mikono. Batumishi tatu ya Sulemani biko mbele ya hema na banakamata essuie-mains, beseni, na jage.

SHAURI: Wakati uko nasoma kitabu ya Wimbo wa Sulemani, tumia sehemu “Habari Zenye Kuwa Ndani” yenye iko mu Tafsiri ya Ulimwengu Mupya, juu ya kuelewa nani njo iko nasema.

2. Mali ya Kiroho

(Dak. 10)

  • Wim 2:7—Mufano wa kijana mwanamuke Mushulami unaweza kufundisha nini Bakristo benye habayafunga ndoa? (w15 15/1 uku. 31 fu. 11)

  • Mu usomaji wa Biblia wa hii juma, ulipata mali gani ya kiroho yenye ungependa kuzungumuzia?

3. Usomaji wa Biblia

(Dak. 4) Wim 2:​1-17 (th somo ya 12)

TUJITOE KABISA MU KAZI YA KUHUBIRI

4. Kuanzisha Mazungumuzo

(Dak. 3) NYUMBA KWA NYUMBA. Zungumuzia kweli moya yenye kuwa mu nyongeza ya A ya broshua Penda Watu. (lmd somo ya 1 nukta ya 3)

5. Kuendelesha Mazungumuzo

(Dak. 4) NYUMBA KWA NYUMBA. Zungumuzia kweli moya yenye kuwa mu nyongeza ya A ya broshua Penda Watu. (lmd somo ya 9 nukta ya 3)

6. Kufanya Banafunzi

(Dak. 5) lff somo ya 18 utangulizi na nukta ya 1-3 (th somo ya 8)

MAISHA YA MUKRISTO

Wimbo 46

7. “Mutu Mukarimu Atabarikiwa”

(Dak. 15) Mazungumuzo. Itolewe na muzee.

Kama tunatumia wakati yetu, nguvu yetu na bitu byetu juu ya kusaidia bengine, tutabarikiwa sana. Ni kweli kama mutu mwenye tulisaidia atafurahi, lakini siye pia tutafurahi. (Mez 22:9) Tutafurahi juu tunajua kama tuko namuiga Yehova, na yeye atatukubali.—Mez 19:17; Yak 1:17.

Mutoto mwanamuke iko natia makuta mu kibweta.
Mwanaume moya iko natumia tablete yake juu ya kutuma muchango wake wa kila mwezi.

Muangalie VIDEO Ukarimu Unaletaka Furaha. Kisha uliza basikilizaji:

  • Namna gani bandugu na badada ba mu hii video balipata furaha juu ya ukarimu wenye bandugu na badada ba mu dunia yote balibaonyesha?

  • Namna gani balipata pia furaha yenye inatokana na kuonyesha bengine ukarimu?

Ujifunze Mambo Mingi Zaidi ku Enternete

Alama ya “Dons” inaonyesha mukono yenye inakamata makuta.

Namna gani unaweza kutoa michango ya kujipendea juu ya kutegemeza kazi ya Mashahidi wa Yehova? Finya pa alama ya “Dons” yenye iko chini ya ukurasa wa kwanza wa JW Library®. Mu mainchi ya mingi, kisha kufinya ile alama, utaona sehemu FAQ. Ukifinya pale, utaona dokima yenye kuitwa Michango kwa Ajili ya Mashahidi wa Yehova—Maulizo Yenye Watu Wanazoea Kuuliza.

8. Funzo ya Biblia ya Kutaniko

(Dak. 30) lfb somo ya 32-33

Maneno ya Kumalizia (Dak. 3) | Wimbo 137 na Sala

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine