Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w25 Mwezi wa 5 uku. 8-13
  • Yehova Atakufariji

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Yehova Atakufariji
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • YEHOVA ANATUONYESHA REHEMA KWA KUTUSAMEHE
  • YEHOVA ANATUPATIA TUMAINI
  • YEHOVA ANATUSAIDIA TUSIOGOPE
  • Yehova “Anaponyesha Wenye Kuvunjika Moyo”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Hatuko Peke Yetu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • Maamuzi Yenye Inaonyesha Kama Tunamutegemea Yehova
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2023
  • Yehova Anakupenda Sana
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
w25 Mwezi wa 5 uku. 8-13

HABARI YA KUJIFUNZA YA 20

WIMBO 7 Yehova Ni Nguvu Yangu

Yehova Atakufariji

“Asifiwe, Baba wa rehema nyingi na Mungu wa faraja yote.”—2 KO. 1:3.

WAZO KUBWA

Mambo yenye tunaweza kujifunza kupitia namna Yehova alifariji Wayahudi wenye walikuwa mu uhamisho.

1. Wayahudi wenye walikuwa mu uhamisho walikuwa mu hali gani? Fasiria.

WAZIA namna Wayahudi wenye walikuwa mu uhamisho Babiloni walijisikia. Walijionea namna inchi yao iliharibiwa. Kwa sababu ya zambi zao na zambi za baba zao, walitoshwa mu nyumba zao na kupelekwa mu inchi ingine. (2 Ny. 36:15, 16, 20, 21) Ni kweli kama mu Babiloni walikuwa na uhuru wa kufanya mambo mbalimbali ya kila siku. (Yer. 29:4-7) Lakini maisha haikukuwa mwepesi. Na haiko ile maisha njo walipenda kuwa nayo. Ile maisha ilifanya wajisikie namna gani? Muyahudi moya muaminifu mwenye alikuwa mu uhamisho alisema hivi: “Pembeni ya mito ya Babiloni, ni pale tulikaa. Tulilia wakati tulikumbuka Sayuni.” (Zb. 137:1) Wale Wayahudi wenye kuvunjika moyo wenye walikuwa mu uhamisho walikuwa na lazima ya kufarijiwa. Lakini wangepata wapi faraja?

2-3. (a) Yehova alifanya nini kwa ajili ya Wayahudi wenye walikuwa mu uhamisho? (b) Tutazungumuzia nini mu hii habari?

2 Yehova ni “Mungu wa faraja yote.” (2 Ko. 1:3) Juu ni Mungu mwenye upendo, anapenda sana kufariji wale wote wenye wanamukaribia. Yehova alijua kama Wayahudi fulani wenye walikuwa mu uhamisho, wangekubali nizamu yake na kumurudilia. (Isa. 59:20) Kwa hiyo, miaka zaidi ya 100 mbele wapelekwe mu uhamisho, Yehova aliongoza nabii Isaya kupitia roho yake ili aandike kitabu yenye kuwa na jina yake, ni kusema kitabu ya Isaya. Juu ya nini? Isaya alisema hivi: “‘Mufariji, mufariji watu wangu,’ ni vile Mungu wenu anasema.” (Isa. 40:1) Kwa kweli, kupitia mambo yenye ule nabii aliandika, Yehova alitolea Wayahudi faraja yenye wangekuwa nayo lazima.

3 Kama wale Wayahudi wenye walikuwa mu uhamisho, mara kwa mara siye pia tunakuwaka na lazima ya faraja. Mu hii habari tutazungumuzia njia tatu zenye Yehova alitumia ili kufariji wale Wayahudi: (1) Aliahidi kusamehe watenda-zambi wenye kutubu, (2) alipatia watu wake tumaini, na (3) aliwasaidia wasiogope. Wakati tutakuwa nazungumuzia ile mambo, ona namna maneno ya Yehova yenye kufariji inaweza kutusaidia.

YEHOVA ANATUONYESHA REHEMA KWA KUTUSAMEHE

4. Namna gani Yehova alionyesha kama yeye ni Mungu mwenye rehema? (Isaya 55:7)

4 Yehova ni “Baba wa rehema nyingi.” (2 Ko. 1:3) Yehova alionyesha sifa ya rehema wakati aliahidi kusamehe Wayahudi wenye kutubu. (Soma Isaya 55:7.) Alisema hivi: “Nitakuonyesha rehema kwa upendo mushikamanifu wa milele.” (Isa. 54:8) Yehova alionyesha rehema yake namna gani? Hata kama taifa ya Wayahudi ilipaswa kuendelea kuteseka kwa sababu ya matendo yao, Yehova aliahidi kama hawangebakia Babiloni milele. Wangebakia mu uhamisho kwa wakati fulani tu. (Isa. 40:2) Ile maneno ilipaswa kutia moyo na kufariji sana Wayahudi wenye walitubu!

5. Juu ya nini tuko hakika kama Yehova ni Mungu mwenye rehema?

5 Tunajifunza nini? Yehova iko tayari kusamehe watumishi wake mu njia kubwa. Leo tuko hakika zaidi kama Yehova iko tayari kusamehe watumishi wake mu njia kubwa sana. Juu ya nini? Juu tunajua mambo yenye Yehova amefanya juu zambi zetu zisamehewe. Miaka mingi kisha Isaya kutoa unabii, Yehova alituma Mwana wake mupendwa ku dunia ili atoe zabihu ya ukombozi kwa ajili ya watenda-zambi wote wenye kutubu. Ile zabihu njo inafanya zambi zetu ‘zifutwe,’ ni kusema zisamehewe kabisa-kabisa. (Mdo. 3:19; Isa. 1:18; Efe. 1:7) Kwa kweli, tunatumikia Mungu mwenye rehema!

6. Kukazia akili rehema ya Yehova kunaweza kutuletea faida gani? (Ona pia picha.)

6 Maneno yenye kuongozwa na roho ya Mungu yenye kuwa mu Isaya 55:7 inaweza kutufariji ikiwa zamiri yetu inaendelea kutuhukumu. Wamoja kati yetu wanaendelea kusumbuliwa na zamiri kwa sababu ya kosa fulani yenye walifanya zamani hata kama walishatubu, zaidi sana kama wanaendelea kupata matokeo ya mubaya ya ile kosa. Lakini kama tumetubu zambi zetu na kubadilika, tunaweza kuwa hakika kama Yehova alishatusamehe. Na wakati Yehova anasamehe anaamua kama hatakumbuka tena zambi yetu. (Linganisha na Yeremia 31:34.) Kwa hiyo, kama Yehova haendelee kukumbuka zambi zetu, juu ya nini siye tuendelee kuzikumbuka? Jambo ya maana kwa Yehova ni mambo yenye tuko nafanya sasa, hapana makosa yenye tulifanya zamani. (Eze. 33:14-16) Na hivi karibuni, Baba yetu mwenye rehema nyingi, atamaliza matokeo ya makosa yetu.

Ndugu iko natembea kwa uhakika. Picha: Picha zenye kuonyesha tofauti kati ya mambo yenye alikuwa anafanya na yenye iko nafanya sasa. Makosa yenye alifanya zamani: 1. Alicheza michezo ya video yenye jeuri. 2. Alikunywa pombe sana na kuvuta. 3. Aliangalia mambo ya mubaya ku ordinatere. Mambo yenye iko nafanya sasa: 1. Kusafisha Jumba ya Ufalme. 2. Iko nazungumuza na dada mwenye kuzeeka. 3. Iko nahubiri.

Jambo ya maana kwa Yehova ni mambo yenye tuko nafanya sasa, hapana makosa yenye tulifanya zamani (Ona fungu ya 6)


7. Nini njo inaweza kutuchochea kuzungumuza na wazee kama tuko nafichika zambi?

7 Tunapaswa kufanya nini kama zamiri yetu iko natuhukumu kwa sababu ya zambi nzito yenye tumeficha? Biblia inatutia moyo tutafute musaada wa wazee. (Yak. 5:14, 15) Inaweza kuwa nguvu kukubali makosa yetu. Lakini tutazungumuza na wale wanaume waaminifu ikiwa tunapenda kutubu na ikiwa tunakumbuka kama Yehova na wanaume wenye ameweka ili kutusaidia watatuonyesha upendo na rehema. Ona namna Yehova alifariji ndugu mwenye kuitwa Arthur.a Zamiri yake ilikuwa namusumbua sana. Arthur anasema hivi: “Kwa mwaka moya hivi, niliangalia pornografia. Lakini kisha kusikiliza hotuba yenye ilikuwa nazungumuzia zamiri, niliambia bibi yangu na wazee wa kutaniko juu ya zambi yangu. Kisha pale nilijisikia muzuri. Lakini zamiri iliendelea kunisumbua juu ya mambo yenye nilifanya. Wazee walinikumbusha kama Yehova angali ananikubali. Anatupatiaka nizamu juu anatupenda. Maneno yao yenye upendo ilinigusa sana na ilinisaidia nibadilishe namna yangu ya kuona mambo.” Leo Arthur ni painia na ni mutumishi wa huduma. Inafariji sana kujua kama Yehova iko tayari kutuonyesha rehema kama tunatubu!

YEHOVA ANATUPATIA TUMAINI

8. (a) Yehova alipatia Wayahudi tumaini gani? (b) Kulingana na Isaya 40:29-31, namna gani ile tumaini ingesaidia Wayahudi wenye walitubu?

8 Kwa wanadamu, Wayahudi wenye walikuwa mu uhamisho Babiloni, hawakukuwa na tumaini yoyote. Babiloni njo ilikuwa serikali kubwa zaidi ya ulimwengu ile wakati na ilijulikana kuwa haiachiliake watu wenye ilikamata. (Isa. 14:17) Lakini Yehova alipatia watu wake tumaini. Aliahidi kama atafanya watu wake waachiliwe na hakuna kitu yenye ingemuzuia. (Isa. 44:26; 55:12) Kwa Yehova, Babiloni ilikuwa tu sawa vile vumbi. (Isa. 40:15) Angeweza tu kuipuliza kidogo na inapotea. Tumaini yenye Yehova alipatia watu wake ingewasaidia namna gani? Ingewafariji. Lakini haiko ile tu. Isaya aliandika hivi: “Wale wenye kumutumainia Yehova watapata nguvu tena.” (Soma Isaya 40:29-31.) Kwa kweli, ile tumaini ingewapatia tena nguvu; ‘wangeruka juu kwa mabawa kama tai.’

9. Ni mambo gani ingesaidia Wayahudi wenye walikuwa mu uhamisho wakuwe hakika kama ahadi za Yehova zitatimia?

9 Yehova alipatia pia Wayahudi sababu zenye zingewasaidia wakuwe hakika kama ahadi zake zingetimia. Alifanya vile namna gani? Fikiria maunabii yenye ilikuwa ilishatimia. Walijua kama Waashuru walishinda ufalme wa kaskazini wa Israeli na kupeleka watu mu uhamisho. (Isa. 8:4) Walijionea namna Wababiloni waliharibu Yerusalemu na kupeleka wakaaji wa Yerusalemu mu uhamisho. (Isa. 39:5-7) Waliona namna Mufalme Sedekia alifanywa kuwa kipofu na kupelekwa Babiloni. (Yer. 39:7; Eze. 12:12, 13) Mambo yote yenye Yehova alitabiri ilitimia. (Isa. 42:9; 46:10) Bila shaka ile mambo yote iliwasaidia wakuwe hakika kabisa kama ahadi ya Yehova yenye ilionyesha kama wataachiliwa huru ingetimia pia!

10. Ni nini ingine inaweza kutusaidia tuendelee kuwa na tumaini?

10 Tunajifunza nini? Wakati tunavunjika moyo, tumaini inaweza kutufariji na kutusaidia tukuwe tena na nguvu. Tunaishi mu wakati wa nguvu sana na tunapambana na maadui wenye nguvu sana. Lakini ile haipaswe kutuvunja moyo. Yehova ametupatia tumaini ya muzuri sana, tumaini ya kuishi milele mu amani na usalama wa kweli. Tunapaswa kuendelea kuweka mu akili yetu na mu moyo wetu ile tumaini. Kama hatufanye vile, tunaweza kuwa sawa vile tuko naangalia fasi ya muzuri yenye kupendeza, lakini kupitia kioo ya buchafu ya dirisha. Namna gani tunaweza kusafisha “kioo ya dirisha yetu” ya mufano, ni kusema kuendelea kuweka katika akili tumaini yetu? Tunaweza kufanya vile kwa kuwazia mara kwa mara namna maisha yetu itakuwa mu dunia mupya. Tunaweza kusoma habari, kuangalia video, na kusikiliza nyimbo zenye zinazungumuzia tumaini yetu. Na tunaweza kuzungumuza na Yehova katika sala juu ya ahadi zenye tuko nangoya kwa hamu zitimie.

11. Ni nini ilisaidia dada fulani mwenye iko na ugonjwa wenye hauwezi kupona apate tena nguvu?

11 Ona namna tumaini ilifariji na kutia nguvu dada Joy, mwenye kuwa na ugonjwa wenye hauwezi kupona. Anasema hivi: “Wakati niko na mahangaiko ya mingi, ninaambiaka Yehova namna niko najisikia kabisa, juu ninajua kama ananielewa. Na Yehova ananijibiaka kwa kunipatia ‘nguvu zenye kupita zile za kawaida.’” (2 Ko. 4:7) Pia, Joy anawaziaka namna maisha yake itakuwa mu dunia mupya, kwenye “hakuna mukaaji mwenye atasema: ‘Niko mugonjwa.’” (Isa. 33:24) Kama na weye unafungulia Yehova moyo wako na kukazia akili tumaini yako, unaweza kupata tena nguvu.

12. Tuko na sababu gani za kuwa hakika kama ahadi za Yehova zitatimia? (Ona pia picha.)

12 Siye pia Yehova anatupatia sababu zenye zinatusaidia tukuwe hakika kama atatimiza ahadi zake, sawa tu vile alifanyia Wayahudi. Fikiria maunabii yenye iko natimia leo. Kwa mufano tuko naona namna serikali kubwa ya ulimwengu iko ‘nguvu sehemu moja na zaifu sehemu ingine.’ (Da. 2:42, 43) Pia tunasikia juu ya “matetemeko ya inchi mahali pamoja kisha pengine,” na tuko nahubiri mu “mataifa yote.” (Mt. 24:7, 14) Ile maunabii na maunabii ingine ya mingi inatusaidia tukuwe hakika zaidi kama ahadi za Yehova zenye haziyatimia zitatimia pia.

Dada iko nasoma na kufikiri sana juu ya unabii wa Biblia. Picha: 1. Bibia na bwana wanasimama pembeni ya prezantware na wako nazungumuza na mwanaume fulani. 2. Baba na mutoto wake wako naangalia vile vitu vimeharibika kisha musiba wa asili. 3. Jiwe inapiga ku miguu ya sanamu yenye Nebukadneza aliona mu ndoto yenye kuzungumuziwa mu Danieli sura ya 2. 4. Watu wako nafurahia maisha mu dunia paradiso.

Maunabii yenye iko natimia leo inatusaidia tukuwe hakika kama ahadi za Yehova zitatimia (Ona fungu ya 12)


YEHOVA ANATUSAIDIA TUSIOGOPE

13. (a) Wayahudi wangepambana na magumu gani mbele waachiliwe? (b) Sawa vile Isaya 41:10-13 inaonyesha, namna gani Yehova alifariji Wayahudi wenye walikuwa mu uhamisho?

13 Yehova alifariji Wayahudi wenye walikuwa mu uhamisho Babiloni kwa kuwapatia tumaini ya muzuri, aliwaahidi kama wataachiliwa. Lakini alijua kama wangepambana na magumu fulani wakati walikuwa karibu kuachiliwa. Yehova alitabiri kama ku mwisho-mwisho wa uhamisho wa Wayahudi katika Babiloni, mufalme fulani mwenye nguvu angeshinda mataifa ya mingi na kushambulia Babiloni. (Isa. 41:2-5) Ile ingeogopesha Wayahudi? Yehova alifariji watu wake mbele ya wakati. Aliwaambia hivi: “Usiogope, kwa maana niko pamoja na wewe. Usihangaike, kwa maana niko Mungu wako.” (Soma Isaya 41:10-13.) Alimaanisha nini wakati alisema “niko Mungu wako”? Hakukuwa nakumbusha Wayahudi kama walipaswa kumuabudu, juu ile ni jambo yenye walipaswa tu kufanya. Lakini alikuwa nawakumbusha kama alikuwa angali upande wao.—Zb. 118:6.

14. Yehova alifanya nini ingine ili kusaidia Wayahudi wasiogope?

14 Pia Yehova alisaidia Wayahudi wasiogope kwa kuwakumbusha kama iko na nguvu mingi sana na anajua mambo mingi sana. Aliwaomba waangalie nyota za mbinguni. Aliwaambia kama ni yeye aliumba zile nyota zote, lakini pia anajua jina ya kila nyota. (Isa. 40:25-28) Sasa kama Yehova anajua jina ya kila nyota, atashindwa kabisa kujua jina ya kila mutumishi wake? Na kama Yehova iko na nguvu ya kuumba nyota, bila shaka iko na nguvu ya kusaidia watu wake. Kwa kweli, Wayahudi wenye walikuwa mu uhamisho hawakukuwa na sababu yoyote ya kuhangaika ao ya kuogopa.

15. Namna gani Mungu alitayarisha Wayahudi wenye walikuwa mu uhamisho juu ya mambo yenye ingetokea?

15 Pia Yehova alitayarisha watu wake mbele ya wakati juu ya mambo yenye itatokea. Mu sehemu ya kwanza ya kitabu ya Isaya, Mungu aliambia hivi taifa ya Israeli: “Muende, watu wangu, muingie katika vyumba vyenu vya ndani, na mufunge milango nyuma yenu. Mujifiche kwa wakati mufupi mupaka kasirani kali ipite.” (Isa. 26:20) Inawezekana ile andiko ilitimia kwa mara ya kwanza wakati Mufalme Koreshi alishinda Wababiloni. Mwanahistoria fulani Mugiriki wa zamani anasema kama wakati Koreshi aliingia Babiloni, “alipatia [maaskari wake] amri ya kuua watu wote wenye wangekuta inje.” Ile ilipaswa kuogopesha sana Wababiloni. Lakini inawezekana Wayahudi wenye walikuwa mu uhamisho waliokoka juu walitii maagizo ya Yehova.

16. Juu ya nini hatupaswe kuhangaika sana juu ya wakati wetu wenye kuya? (Ona pia picha.)

16 Tunajifunza nini? Karibuni tutapambana na taabu kubwa zaidi yenye haiyatokeaka. Wakati itaanza, watu wote kwa ujumla watavurugika na kuogopa. Lakini hapana watu wa Yehova. Tunajua kama Yehova ni Mungu wetu. Tutasimama wima juu tunajua kama “ukombozi [wetu] unakaribia.” (Lu. 21:28) Hata wakati muungano wa mataifa utatushambulia, tutaendelea kumutumainia Yehova. Yehova atatulinda kwa kutumia malaika wake, na atatupatia maagizo yenye itatusaidia tuokoke. Ile maagizo itatufikia namna gani? Tungoye tuone. Lakini inawezekana tutapata ile maagizo kupitia makutaniko yetu. Ni mu ile njia njo makutaniko yetu itakuwa sawa “vyumba vya ndani,” kwenye tutapata ulinzi. Namna gani tunaweza kujitayarisha kwa ajili ya mambo yenye itatokea karibuni? Tunapaswa kuendelea kuwa karibu na ndugu na dada zetu, kuwa tayari kutii muongozo wa kiteokrasi, na kuwa hakika kama Yehova iko naongoza tengenezo yetu.—Ebr. 10:24, 25; 13:17.

Ndugu na dada wako nasoma Biblia mu chumba fulani wakati wa taabu kubwa. Wako naangalia inje ku dirisha wakati ndugu moya anashota kidole mawingu.

Kufikiria namna Yehova iko na nguvu mingi sana na iko na uwezo wa kutuokoa, kutatusaidia tusihangaike kupita kiasi wakati wa taabu kubwa (Ona fungu ya 16)b


17. Namna gani unaweza kuacha Yehova akufariji?

17 Hata kama maisha haikukuwa mwepesi kwa Wayahudi wenye walikuwa mu uhamisho, Yehova aliwapatia faraja yenye walikuwa nayo lazima. Atafanya vile kwa ajili yetu pia. Hata kutokee nini, ukuwe hakika kama Yehova atakufariji. Ukuwe hakika kama atakuonyesha rehema kwa kukusamehe. Endelea basi kukazia akili tumaini yako, na uendelee kukumbuka kama juu Yehova ni Mungu wako, hauna sababu ya kuogopa.

NAMNA GANI MAANDIKO YENYE KUFUATA INAKUFARIJI?

  • Isaya 55:7

  • Isaya 40:29-31

  • Isaya 41:10-13

WIMBO 3 Nguvu Yangu, Tumaini Yangu, Ninakutegemea

a Majina fulani imebadilishwa.

b MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu na dada wanakutana pamoya mu kikundi kidogo. Wako hakika kama Yehova iko na nguvu na uwezo wa kulinda watu wake hata wakuwe wapi ku dunia.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine