PENDEKEZO JUU YA MAMBO YA KUJIFUNZA
Namna ya Kuwa Hakika Kama Yehova Anaweza Kukuokoa
Soma Hesabu 13:25–14:4 juu uone namna Baisraeli balionyesha kama habamutumainie Yehova.
Chunguza habari yote. Juu ya nini Baisraeli balipaswa kuwa hakika kama Yehova iko na uwezo wa kubaokoa wakati balitoka Misri? (Zb. 78:12-16, 43-53) Nini njo ilifanya baache kumutumainia Yehova? (Kum. 1:26-28) Namna gani Yoshua na Kalebu balionyesha kama banamutumainia Yehova?—Hes. 14:6-9.
Ujifunze mambo mingi zaidi. Baisraeli bangefanya nini juu batumainie Yehova zaidi? (Zb. 9:10; 22:4; 78:11) Juu ya nini inaomba tumuheshimie kwanza Yehova juu tuweze kumutumainia?—Hes. 14:11.
Unajifunza nini? Ujiulize hivi:
- ‘Inaweza kuwa nguvu kwangu kumutumainia kabisa Yehova mu hali gani?’ 
- ‘Ninaweza kufanya nini juu nimutumainie Yehova zaidi leo na mu siku zenye kuya?’ 
- ‘Wakati taabu kubwa itaanza ninaweza kuwa hakika na jambo gani?’—Lu. 21:25-28.