Njia Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Jinsi ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya Kwanza Katika Mwezi wa 2
“Unafikiri kwamba Mungu ana tengenezo ao anaongoza kila mutu kibinafsi? [Acha mutu ajibu.] Ona jinsi gazeti hili linasema kuhusu watu waliounda tengenezo la Mungu wakati wa zamani.” Fungua Mnara wa Mlinzi wa tarehe 1/02/2012 kwenye ukurasa wa 16, na muzungumuzie habari iliyo chini ya kichwa kidogo cha kwanza na andiko moja hivi kati ya maandiko yanayoonyeshwa. Tolea mutu gazeti na ufanye mupango wa kumurudilia ili kuzungumuzia habari inayofuata.
Mnara wa Mlinzi 01/02/12
“Katika miaka ya hivi karibuni, watu wamezungumuzia sana Har-Magedoni. Unafikiri wanadamu wana jambo lolote ambalo wanaweza kufanya ili kuzuia Har-Magedoni isitukie? [Acha mutu ajibu.] Ona mahali neno Har-Magedoni linatoka. [Soma Ufunuo 16:16. Kisha onyesha jalada la gazeti.] Gazeti hili linatoa jibu la Biblia kuhusu maulizo hayo.”
Amkeni! Mwezi wa 2
“Leo watu wengi wanafurahia kuzungumuza na wengine kupitia Internet. Unafikiri kwamba namna hiyo ya kuzungumuza ina hatari? [Acha mutu ajibu.] Biblia ina kanuni zinazoweza kutusaidia kuepuka hatari zinazotokana na Internet. [Fungua gazeti kwenye ukurasa wa 6-9, na muzungumuzie ulizo moja kati ya maulizo yanayoonyeshwa na musome andiko moja.] Gazeti hili litakusaidia utambue hatari zinazotokana na kuzungumuza na wengine kwa njia ya Internet na jinsi ya kuepuka hatari hizo.”