Tusiwasahau Wale Walio Katika Nyumba za Kuwatunzia Watu Waliozeeka
1. Sababu gani tunapaswa kuwahubiria wale walio katika nyumba za kuwatunzia watu waliozeeka?
1 Watu wengi wanapambana na matokeo mabaya ya kuzeeka. (Mhu. 12:1-7) Kwa kuwa watu fulani wenye kuzeeka wanaishi katika nyumba za kuwatunzia watu waliozeeka, inakuwa vigumu kuwapata tunapohubiri nyumba kwa nyumba. Hata kama pengine wanaweza kuwa na magumu ya kutembea ao kukumbuka mambo fulani, watu waliozeeka wanaweza kuwa wangali na uwezo wa kujifunza, kuelewa, na kufikia kumupenda Yehova. Namna gani tunaweza kuwapata ili kuzungumuza nao kuhusu habari njema ya “tumaini la furaha”?—Tito 2:13.
2. Namna gani tunaweza kujua hesabu ya nyumba za kuwatunzia watu waliozeeka?
2 Tutaanza Namna Gani?: Kwa kawaida tunaweza kujua hesabu ya nyumba za kuwatunzia watu waliozeeka kwa kutumia kitabu cha namba za telefone cha eneo letu. Kisha tafuta aina mbalimbali za nyumba za kuwatunzia watu waliozeeka kama vile nyumba ambamo kikundi kidogo cha watu wanaohitaji musaada wanaishi pamoja, nyumba za mashirika yanayotoa musaada wa kila siku bila kuwa na hopitali. Mwangalizi wa utumishi anaweza kufanya mipango ili wahubiri wenye uzoefu watembelee kila nyumba ya kuwatunzia watu waliozeeka. Kwa kawaida kupanga mambo vizuri na kumutegemea Yehova, kunaweza kutusaidia kuanzisha funzo la Biblia la kikundi.—Met. 21:5; 1 Yoh. 5:14, 15.
3, 4. (a) Tunapaswa kuzungumuza kwanza na nani mbele ya kuanzisha funzo la kikundi? (b) Namna gani tunaweza kupanga programu ya funzo hilo?
3 Namna ya kuanzisha funzo kutategemea aina ya nyumba ya kuwatunzia watu waliozeeka. Katika makao makubwa-makubwa yenye watu waliozeeka na wafanyakazi wengi, ni vizuri zaidi kumufikia kwanza mutu anayekaribisha wageni ili kumuomba nafasi ya kuzungumuza na musimamizi. Katika makao madogo-madogo yenye watu waliozeeka wachache, na wafanyakazi wawili ao watatu, inaweza kuwa vizuri kuzungumuza moja kwa moja na mwenye makao hayo.
4 Katika hali zote hizo, jitambulishe kwamba wewe ni mutu anayejitolea kutumia wakati wake ili kusaidia watu wanaopenda kusoma na kuzungumuzia habari za Biblia. Uliza ikiwa kuna watu waliozeeka ambao wanaweza kufurahia kushiriki katika mazungumuzo ya Biblia ya kikundi kwa dakika 30 hivi. Unaweza kutumia vitabu mbalimbali, lakini wengi wamefurahia kutumia Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia na Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Unaweza kuamua kumuonyesha musimamizi vitabu hivyo. Munaweza kuzungumuza pamoja ili kupanga siku, saa na mahali pa kujifunzia na vinaweza kuwekwa kwenye programe ya kazi ya nyumba ya kuwatunzia watu waliozeeka. Usiogope kujitambulisha kwamba wewe ni Shahidi wa Yehova. Wakati huohuo, mueleweshe musimamizi wa nyumba hiyo kwamba utafika kila mara kuwasaidia watu wajifunze Biblia wala si kufanya ibada ya dini.
5. Ni mashauri gani yenye kufaa yatakayofanya funzo liwe lenye kupendeza na lenye kujenga?
5 Namna ya Kuongoza Funzo la Kikundi: Namna ya kuongoza funzo hilo inategemea hali na makao ya watu waliozeeka; kwa hiyo, ni vizuri kuwa mwenye busara na kubadilika kulingana na hali. Kiongozi wa funzo anapaswa kuleta vichapo vingi vya kutumia na anapaswa kuvikusanya kisha funzo. Ni vizuri kuleta vitabu vilivyo na maandishi makubwa-makubwa kwa ajili ya wanafunzi fulani. Kama kawaida, mafungu yanaweza kusomwa na kuuliza maulizo, na majibu yanaweza kutolewa. Wale wanaotaka na walio na uwezo wanaweza kuombwa kusoma mafungu ao Maandiko ya Biblia. Wakati wa funzo, uwe mwenye kuchangamuka, mwenye kutia moyo, na mwenye kufanya urafiki. Ikiwa musimamizi anakubali, wakati fulani unaweza kuwaonyesha wanafunzi, moja kati ya video zetu inayochochea watu waamini Biblia ao inayotoa somo nzuri kutoka katika habari fulani ya Biblia. Unaweza kuanza na kumaliza funzo kwa kutoa sala fupi. Wahubiri fulani wamepanga hata wakati fulani wa kuimba nyimbo za Ufalme.
6. Unaweza kufanya nini ikiwa mwanafunzi mumoja anapinga jambo fulani?
6 Utafanya nini ikiwa mwanafunzi fulani anapinga jambo ambalo linasomwa ao kuzungumuziwa wakati wa funzo? Tumia utambuzi unapomujibia. (Kol. 4:6) Pengine unaweza kusoma andiko fupi la Biblia linalozungumuzia waziwazi jambo hilo. Ikiwa unaona kwamba si lazima kufanya hivyo, unaweza kumuambia kwamba umemuelewa, lakini mutazungumuzia jambo hilo ninyi wawili kisha funzo.
7. Tunaweza kufanya nini ikiwa mwanafunzi mumoja anauliza ulizo linalomuhusu peke yake ao anapendezwa sana?
7 Wakati mwengine, mwanafunzi anaweza kuuliza ulizo ao kutaka kujua mengi zaidi. Dada mumoja anazoea kusema hivi: “Hilo ni ulizo nzuri sana. Lakini kwa kuwa linakuhusu wewe tu, vumilia kidogo mupaka tumalize kwanza kujifunza. Kisha mimi na wewe tutazungumuzia ulizo hilo.” Inawezekana kupanga kuongoza funzo la Biblia na mutu mumoja-mumoja anayependezwa kwa wakati mwingine na mahali mbalimbali.
8. Namna gani mafunzo ya kikundi na funzo lolote la Biblia na mutu mumoja-mumoja yanapaswa kuripotiwa?
8 Ni vizuri zaidi Wahubiri walewale waendelee kuongoza funzo la kikundi kwenye makao hayo. Kila muhubiri anayeshiriki anaweza kuripoti wakati huo. Wakati funzo hilo linaanza kabisa, muhubiri anayesimamia funzo hilo la kikundi anaweza kuhesabu ziara moja ya kurudia kila mara funzo linapoongozwa na funzo moja la Biblia kwa mwezi. Mafunzo ya Biblia yanayoanzishwa pamoja na mutu mumoja-mumoja mwenye kuzeeka ambaye ana uwezo wa kujifunza na kuelewa yanaweza kuripotiwa kwa njia ya kawaida.
9, 10. Wale mbao wanaongoza funzo la kikundi wanapaswa kuwa na sifa gani? Eleza.
9 Endelea Kuongoza Funzo la Kikundi: Ni vizuri zaidi kupanga siku na saa ya funzo la kikundi. Watu waliozeeka na wafanyakazi watafurahi ikiwa funzo linafanyika kwa ukawaida na linaanza na kumalizika kwa wakati. (Mt. 5:37) Kwa hiyo, muhubiri anahitaji kujitolea, kuwa na bidii na kupanga mambo vizuri. Wahubiri fulani wameona kwamba ni vizuri zaidi watu wawili wenye uzoefu kutumika pamoja ili kuongoza funzo la kikundi. (Mhu. 4:9, 10) Makao makubwa-makubwa yanaweza kuhitaji wahubiri wengi.
10 Ni vizuri pia kuwa mwenye kufanya urafiki na kuwahangaikia wengine. (Flp. 2:4) Unapojifunza nao kwa mara ya kwanza, jikaze kuzungumuza na kila mutu anayeshiriki katika funzo hilo. Andika majina yao na ujikaze kuyakumbuka wakati wa funzo la kufuata. Hata hivyo, watu fulani wenye kuzeeka wanaweza kukasirika wakati mutu ambaye hawajue anawaita kwa majina yao. Ukionyesha uvumilivu na kuwahangaikia, utafanya kila mutu ajisikie vizuri na mwenye kupendwa.
11. Namna gani wale wanaoongoza funzo la kikundi wanaweza kuonyesha heshima kwa wafanyakazi na kwa watu wa jamaa wa watu waliozeeka?
11 Ni jambo la lazima pia kuonyesha heshima na kuwahangaikia wafanyakazi wa makao hayo na watu wa jamaa wa watu waliozeeka. Ikiwa programu ya kujifunza tayari imepangwa, si vizuri kubadilisha wakati ao mahali bila kuzungumuza kwanza na musimamizi. Muulize mara kwa mara, maoni yake kuhusu matokeo ya funzo hilo. Watu wa jamaa wa watu waliozeeka wanapowatembelea wakati wa funzo, jikaze kuzungumuza nao. Waelezee sababu gani tunawafundisha watu Biblia. Wahakikishie kwamba unawahangaikia sana watu wa jamaa zao. Waalike wao pia washiriki katika funzo.
12, 13. Eleza mifano inayoonyesha faida ya kuhubiri kwenye nyumba za kuwatunzia watu waliozeeka.
12 Matokeo: Waangalizi wanaosafiri na ndugu na dada katika kutaniko wanaeleza matokeo yenye kutia moyo yanayotokana na kuongoza funzo la kikundi. Kwa mufano, watu 20 hivi wenye kuishi katika nyumba za kuwatunzia watu waliozeeka walihuzuria siku ya kwanza ya mazungumuzo. Jambo hilo lilifanya mafunzo sita mbalimbali ya Biblia yaanzishwe. Mwishowe, mumoja kati yao alibatizwa. Katika makao mengine, funzo la kikundi lilimuchochea mwanamuke mumoja wa miaka 85 aanze kukusanyika na kutaniko la eneo lake na kupenda kubatizwa. Wakati makao fulani yaliamua kuongeza kazi zake, na kuondoa programu ya funzo la kikundi lililokuwa likiongozwa na Mashahidi wa Yehova; watu waliozeeka ambao walikuwa katika makao hayo walipeleka malalamiko yao kwa musimamizi. Mwishowe, funzo lilianza tena na kisha watu kati ya 25 na 30 walikuwa wanahuzuria funzo hilo.
13 Upendo ambao tunawaonyesha wale walio katika nyumba za kuwatunzia watu waliozeeka unashangaza pia watu wengine. Kwa mufano, kwa kawaida, tunawaona wafanyakazi wa makao hayo wakihuzuria na hata kushiriki katika funzo. Bidii tunayoonyesha ili kuhangaikia sana wale walio katika nyumba za kuwatunzia watu waliozeeka inatoa pia ushuhuda muzuri kwa watu wa eneo. (1 Pet. 2:12) Kisha kumuambia sababu gani tunawafundisha watu Biblia, musimamizi mumoja alisema: “Tulikuwa na lazima yenu tangu zamani! Mutaanza siku gani?” Musimamizi mwengine aliandika hivi: “Ningependa funzo la kikundi kama hili lifanywe katika nyumba zote za kuwatunzia watu waliozeeka za eneo letu. Mashahidi wa Yehova wanafanya kazi hii bila malipo kwa kuwa wanaiona kuwa sehemu ya utumishi wao kwa watu wa eneo.” Nyumba moja ya kuwatunzia watu waliozeeka huko Hawaii ilipatia Mashahidi wa Yehova Diplome ya Kazi ya Kujitolea iliowataja kuwa “zawadi nzuri” kwa wale walio katika nyumba hiyo ya kuwatunzia watu waliozeeka.
14. Sababu gani tunapaswa kuwahubiria wale walio katika nyumba za kuwatunzia watu waliozeeka?
14 Yehova anawaalika watu waliozeeka wamusifu. (Zab. 148:12, 13) Aliko hilo linahusu pia wale walio katika nyumba za kuwatunzia watu waliozeeka. Je, kuna nyumba za kuwatunzia watu waliozeeka katika eneo lenu zenye watu waliozeeka wanaoweza kufaidika kwa kusikiliza habari njema? Kwa musaada wa wazee wa kutaniko lenu na wasimamizi wa nyumba hizo, tunaweza kupata nafasi ya kuwahubiria wale walio katika nyumba za kuwatunzia watu waliozeeka. Tunapowakumbuka wale waliozeeka, tunamuiga Yehova.—Zab. 71:9, 18.