MAISHA YA MUKRISTO
Namna ya Kutoa Majibu Mazuri
Majibu mazuri yanajenga kutaniko. (Rom 14:19) Yanaletea pia furaha wale wenye kuyatoa. (Met 15:23, 28) Kwa hiyo, tunapaswa kujikaza kutoa hata jibu moja kwenye kila mukutano. Lakini, haiwezekane tuchaguliwe kila mara tunaonyesha mukono. Ndiyo sababu ni muzuri kutayarisha majibu mengi.
Jibu la muzuri . . .
ni lenye kuwa wazi, mwepesi kuelewa na fupi. Mara nyingi halipite segonde 30
ni lenye kusemwa katika maneno yetu
ni lenye halirudilie majibu ya wengine
Kama wewe ndiye wa kwanza kujibia, . . .
jibia ulizo moja kwa moja na waziwazi
Kama jibu la ulizo limekwisha kutolewa, unaweza . . .
kuonyesha namna andiko fulani lenye kutajwa linaunga mukono habari yenye munazungumuzia
kuonyesha namna habari yenye kuzungumuziwa inatuhusu
kueleza namna tunaweza kutumikisha habari yenye kuzungumuziwa
kueleza kwa kifupi mufano wenye kukazia wazo kubwa