HABARI YA KUJIFUNZA YA 20
WIMBO 67 “Hubiri Neno”
Upendo Ukuchochee Kuendelea Kuhubiri!
“Katika mataifa yote, lazima habari njema ihubiriwe kwanza.”—MK. 13:10.
WAZO KUBWA
Namna upendo unatuchochea tuhubiri kwa bidii na kwa moyo wote.
1. Tulijifunza nini ku mukutano wa kila mwaka wa 2023?
KU MUKUTANO wa kila mwaka wa 2023a tulisikia mafasirio ya mupya kuhusu mambo fulani yenye tunaamini na tulisikia tangazo yenye kufurahisha kuhusu kazi ya kuhubiri. Kwa mufano, tulijifunza kama watu fulani wanaweza kupata nafasi ya kujiunga na watu wa Yehova hata kisha Babiloni Mukubwa kuharibiwa. Tulijifunza pia kama kuanzia Mwezi wa 11, 2023, wahubiri hawangeombwa tena kuripoti mambo fulani kuhusu kazi ya kuhubiri. Ile mabadiliko inaonyesha kama kazi yetu ya mahubiri haiko ya maana ao ya haraka sawa zamani? Hapana, haionyeshe vile.
2. Juu ya nini kila siku yenye inapita inafanya kazi yetu ya kuhubiri ikuwe ya haraka sana? (Marko 13:10)
2 Kila siku yenye inapita, inafanya kazi yetu ya kuhubiri ikuwe ya haraka sana. Juu ya nini? Juu kunabakia wakati kidogo sana mbele mwisho ufike. Ona mambo yenye Yesu alitabiri kuhusu kazi ya kuhubiri mu siku za mwisho. (Soma Marko 13:10.) Mu habari yenye kuwa mu Injili ya Matayo, Yesu alisema kama habari njema ingehubiriwa mu dunia yote yenye kuikaliwa na watu mbele “ule mwisho” ufike. (Mt. 24:14) Maneno “ule mwisho,” inazungumuzia mwisho wa ulimwengu mubaya wa Shetani. Yehova ameweka “siku na saa” ya matukio yenye itatokea karibuni. (Mt. 24:36; 25:13; Mdo. 1:7) Kila siku yenye inapita inafanya tukaribie zaidi ile wakati. (Ro. 13:11) Kwa hiyo, tunapaswa kuendelea kuhubiri mupaka mwisho ufike.
3. Nini njo inatuchochea kuhubiri?
3 Kuhusu kazi ya kuhubiri, ni muzuri tufikirie hii ulizo ya maana sana: Juu ya nini tunahubiri habari njema? Kwa kifupi, ni upendo njo unatuchochea kuhubiri. Mambo yenye tunafanya mu kazi ya kuhubiri inaonyesha kama, tunapenda habari njema, tunapenda watu, na zaidi sana, tunamupenda Yehova na jina yake. Tuzungumuzie basi ile mambo.
TUNAHUBIRI JUU TUNAPENDA HABARI NJEMA
4. Tunafanyaka namna gani wakati tunapata habari ya muzuri?
4 Unaweza kukumbuka namna ulijisikia wakati ulipata habari fulani ya muzuri? Pengine ulipata habari kama mutoto amezaliwa mu familia yenu ao kama umepata kazi yenye ulikuwa nayo lazima kabisa. Bila shaka ulipenda sana kuelezea watu wa familia na marafiki ile habari ya muzuri. Ni vile ulijisikia wakati ulipata habari njema ya Ufalme wa Mungu, habari ya muzuri zaidi?
5. Ulijisikia namna gani wakati ulijifunza kwa mara ya kwanza kweli za Biblia? (Ona pia picha.)
5 Kumbuka namna ulijisikia wakati ulijifunza kwa mara ya kwanza kweli za Biblia. Ulijifunza kama Baba yako wa mbinguni anakupenda, anapenda ukuwe mu familia ya waabudu wake, anaahidi kumaliza maumivu na mateso, na kama anakupatia tumaini ya kuonana tena na wapendwa wako wenye wamekufa; na ulijifunza mambo ingine ya mingi. (Mk. 10:29, 30; Yoh. 5:28, 29; Ro. 8:38, 39; Ufu. 21:3, 4) Ile mafundisho ya Biblia ilikufurahisha sana. (Lu. 24:32) Ulipenda sana mambo yenye ulikuwa najifunza, na ulipenda kabisa kuielezea wengine!—Linganisha na Yeremia 20:9.
Wakati tulisikia habari njema kwa mara ya kwanza, tulipenda kabisa kuielezea wengine! (Ona fungu ya 5)
6. Mufano wa Ernest na Rose, unakufundisha nini?
6 Fikiria hii mufano. Ndugu Ernestb alikuwa na miaka karibu kumi wakati baba yake alikufa. Anakumbuka hivi: “Nilijiuliza: ‘Ameenda mbinguni? Amekufa milele?’ Nilitamani watoto wenye baba zao walikuwa wangali wazima.” Ernest alizoea kuenda ku makaburi, alikuwa napiga magoti ku kaburi ya baba yake, na kusali hivi: “Tafazali Mungu, napenda kujua kwenye baba yangu iko.” Miaka 17 kisha kifo ya baba ya Ernest, Mashahidi wa Yehova walimuomba aanze kujifunza Biblia, na alikubali kabisa kufanya vile. Alifurahi sana kujua kama mutu mwenye amekufa hajue kitu, ni sawa vile iko mu usingizi muzito sana, na kama Biblia inaahidi kuwa kutakuwa ufufuo. (Muh. 9:5, 10; Mdo. 24:15) Ku mwisho, alipata majibu ya maulizo yenye ilikuwa imemuhangaisha kwa wakati murefu! Ernest alifurahia sana kweli za Biblia zenye alikuwa najifunza. Bibi yake, Rose, naye alianza kujifunza Biblia na alipenda pia ujumbe wa Ufalme. Mu 1978 Ernest na bibi yake walibatizwa. Walifurahia sana kuelezea watu wa familia yao, marafiki, na watu wengine wenye waliwasikiliza, mambo yenye waliamini. Ernest na Rose wamepata matokeo gani? Wamesaidia watu zaidi ya 70 kufanya maendeleo na kufikia ubatizo.
7. Wakati tunapenda sana kweli za Biblia na zinatia mizizi mu moyo wetu, ile inatuchochea kufanya nini? (Luka 6:45)
7 Ni wazi kama, wakati tunapenda sana kweli za Biblia na zinatia mizizi mu moyo wetu, hatuwezi kujizuia kuzielezea wengine. (Soma Luka 6:45.) Tunajisikia sawa wanafunzi wa Yesu wa karne ya kwanza wenye walisema: “Hatuwezi kuacha kusema juu ya mambo yenye tumeona na kusikia.” (Mdo. 4:20) Tunapenda sana kweli ya Biblia, njo maana tunapenda kuielezea watu wengi kadiri inawezekana.
TUNAHUBIRI JUU TUNAPENDA WATU
8. Ni nini inatuchochea kutangazia wengine habari njema? (Ona kisanduku “Penda Watu—Juu Ufanye Wanafunzi.”) (Ona pia picha.)
8 Kama Yehova na Mwana wake, tunapenda watu. (Mez. 8:31; Yoh. 3:16) Tunasikilia huruma wale wenye wako “bila Mungu” na wenye “hawana tumaini.” (Efe. 2:12) Wako nahangaika sana kwa sababu ya magumu ya maisha, lakini tuko na jambo yenye wako nayo lazima kabisa, ni kusema habari njema ya Ufalme wa Mungu. Upendo na huruma inatusaidia kufanya yote yenye tunaweza ili kuwatangazia habari njema. Ile habari ya maana sana inaweza kuwapatia tumaini, kuwasaidia wakuwe na maisha ya muzuri leo kadiri inawezekana, na kuwapatia tumaini ya kuwa na “uzima wa kwelikweli,” ni kusema uzima wa milele mu ulimwengu mupya wa Mungu.—1 Ti. 6:19.
Upendo na huruma inatusaidia kufanya yote yenye tunaweza ili kutangazia watu habari njema (Ona fungu ya 8)
9. Tunatoa onyo gani kuhusu wakati wenye kuya, na juu ya nini? (Ezekieli 33:7, 8)
9 Kupenda watu kunatuchochea pia tuwaonye kuhusu mwisho wa huu ulimwengu wenye unakaribia. (Soma Ezekieli 33:7, 8.) Tunasikilia huruma majirani wetu na watu wa familia yetu. Wengi wanaendelea na maisha yao ya kila siku bila kujua mambo yenye itatokea karibuni, ni kusema “taabu kubwa yenye haijatokea tangu mwanzo wa ulimwengu mupaka sasa, hapana, na haitatokea tena.” (Mt. 24:21) Tunapenda wajue mambo yenye itatokea mu ile wakati wa hukumu: Dini ya uongo itaharibiwa na mupangilio wote wa mambo wa Shetani utaharibiwa ku Armagedoni. (Ufu. 16:14, 16; 17:16, 17; 19:11, 19, 20) Tunasali ili watu wengi kadiri inawezekana, wasikilize onyo yenye tunawatolea na wajiunge na siye mu ibada safi. Lakini itakuwa namna gani juu ya wale wenye hawasikie onyo yenye tunawatolea leo, kutia ndani watu wa familia yetu wenye tunapenda?
10. Juu ya nini ni jambo ya haraka sana kuendelea kuonya watu?
10 Sawa vile tuliona mu habari yenye kutangulia, inaweza kuwa mapenzi ya Yehova kuokoa watu wenye watabadilika na kuamua kuwa upande wake wakati wataona uharibifu wa Babiloni Mukubwa. Kama ni vile, ni jambo ya haraka sana tuendelee kuonya watu. Fikiria hii jambo: Pengine watakumbuka mambo yenye tuko nawaambia leo. (Linganisha na Ezekieli 33:33.) Pengine watakumbuka onyo yenye tuliwatolea, na ile itawachochea wajiunge na siye mu ibada safi mbele ikuwe nyuma kufanya vile. Kama ule mulinzi wa gereza katika Filipi mwenye alibadilika kisha tu “tetemeko kubwa la inchi” kutokea, pengine wamoja kati ya watu wenye hawasikilize habari njema leo, watabadilika kisha kuona uharibifu wa Babiloni Mukubwa, wenye utashangaza sana watu.—Mdo. 16:25-34.
TUNAHUBIRI JUU TUNAMUPENDA YEHOVA NA JINA YAKE
11. Namna gani tunamupatia Yehova utukufu, heshima, na nguvu? (Ufunuo 4:11) (Ona pia picha.)
11 Sababu ya maana zaidi yenye inatuchochea kuhubiri habari njema ni juu tunamupenda Mungu na jina yake takatifu. Tunaona kuwa, kazi yetu ya kuhubiri ni nafasi ya kumusifu Mungu mwenye tunapenda. (Soma Ufunuo 4:11.) Tunakubaliana kama Yehova Mungu anastahili kupokea utukufu, heshima, na nguvu, kutoka kwa waabudu wake washikamanifu. Tunamutolea Yehova utukufu na heshima wakati tunaonyesha wengine ushuhuda wenye kuonyesha kama ‘aliumba vitu vyote’ na kama ni yeye njo alitupatia uzima. Tunamutolea nguvu yetu wakati tunatumia uwezo wetu, wakati wetu, na vitu vyetu ili kutegemeza kazi ya kuhubiri kadiri hali yetu inaruhusu. (Mt. 6:33; Lu. 13:24; Kol. 3:23) Mu maneno ingine, tunapenda kuzungumuza juu ya Mungu mwenye tunapenda. Tunachochewa pia kuambia wengine kuhusu jina yake na maana ya jina yake. Juu ya nini?
Tunamutolea Yehova nguvu yetu wakati tunatumia uwezo wetu, wakati wetu, na vitu vyetu ili kutegemeza kazi ya kuhubiri kadiri hali yetu inaruhusu (Ona fungu ya 11)
12. Namna gani tunatakasa jina ya Yehova mu mahubiri?
12 Upendo wetu kwa Yehova unatuchochea tutakase jina yake. (Mt. 6:9) Tunapenda kuchangia kutakasa jina ya Mungu, kwa kuambia wengine kama mambo yenye Shetani anasema juu ya Mungu ni ya uongo kabisa. (Mwa. 3:1-5; Yob. 2:4; Yoh. 8:44) Mu mahubiri tuko tayari kutetea Mungu wetu na kuambia wenye wanapenda kutusikiliza mambo ya kweli kumuhusu. Tunapenda watu wote wajue kama sifa yake kubwa zaidi ni upendo, kama namna yake ya kutawala njo ya muzuri zaidi na yenye haki, na kama karibuni Ufalme wake utamaliza mateso yote na kuletea wanadamu wote amani na furaha. (Zb. 37:10, 11, 29; 1 Yo. 4:8) Wakati tunamutetea Yehova mu mahubiri tunatakasa jina yake. Tunafurahi pia juu tuko natimiza daraka yetu ya kuwa Mashahidi wake. Juu ya nini tunasema vile?
13. Juu ya nini tunaona kama ni pendeleo kubwa sana kuitwa Mashahidi wa Yehova? (Isaya 43:10-12)
13 Yehova ametuita ili tukuwe “mashahidi.” (Soma Isaya 43:10-12.) Miaka fulani yenye imepita, barua fulani yenye ilitoka ku Baraza Yenye Kuongoza ilisema hivi: “Pendeleo kubwa zaidi yenye kila mumoja wetu iko nayo, ni kuitwa Shahidi wa Yehova.”c Juu ya nini? Fikiria hii mufano: Kama unapenda mutu fulani akuwe shahidi wako ku tribinali, utachagua mutu mwenye unajua na mwenye unatumainia, mwenye namna yake ya kuwa itafanya wengine watumainie ushahidi wenye atatoa. Juu Yehova ametuchagua kuwa Mashahidi wake, ile inaonyesha kama anatujua muzuri na kama anatumainia kuwa tutaambia wengine kama yeye njo Mungu wa kweli. Tunaona kuwa ni pendeleo kubwa sana kuwa Mashahidi wake, njo maana tunatumia kila nafasi yenye tunapata ili kuambia wengine kuhusu jina yake na kuwasaidia waelewe kama mambo mingi yenye imesemwa juu yake ni ya uongo. Wakati tunafanya vile, tunaonyesha kama tunaishi kulingana na jina yetu yenye tunajivunia sana, Mashahidi wa Yehova!—Zb. 83:18; Ro. 10:13-15.
TUTAENDELEA KUHUBIRI MUPAKA MWISHO
14. Ni mambo gani itatokea hivi karibuni?
14 Tunangoya kwa hamu sana mambo yenye itatokea karibuni. Kwa musaada wa Yehova tunatumaini kama watu wengi zaidi watakubali kweli mbele taabu kubwa ianze. Pia tunafurahi kujua kama hata mu kipindi ya nguvu zaidi mu historia ya wanadamu, ni kusema wakati wa taabu kubwa, inawezekana watu fulani wataachana na ulimwengu wa Shetani na kujiunga na siye ili kumusifu Yehova!—Mdo. 13:48.
15-16. Tutaendelea kufanya kazi gani, na tutaendelea nayo mupaka wakati gani?
15 Lakini mbele ile wakati ifike, kwa sasa tuko na kazi ya kufanya. Tuko na pendeleo ya kutangaza ujumbe wenye hautatangaziwa tena, ni kusema kutangaza habari njema ya Ufalme wa Mungu mu dunia yote. Wakati uleule, tunapaswa kuendelea kuonya watu. Watu wanapaswa kujua kama mwisho wa huu ulimwengu mubaya, uko nakaribia sana. Kisha, wakati kipindi ya hukumu itafika watajua kama ujumbe wenye tulikuwa nahubiri ulitoka kwa Yehova Mungu.—Eze. 38:23.
16 Tuazimie basi kufanya nini? Kupenda habari njema, kupenda watu, na zaidi ya yote kumupenda Yehova na jina yake. Ile mambo ituchochee basi kuendelea kuhubiri kwa bidii na kuona kama hii kazi ni ya haraka sana. Tufanye vile mupaka wakati Yehova atasema, “Basi, muache sasa!”
WIMBO 54 “Hii Ndiyo Njia”
a Mukutano wa kila mwaka ulifanywa tarehe 7, Mwezi wa 10, 2023, ku Jumba ya Mukusanyiko ya Newburgh ya Mashahidi wa Yehova, katika New York, Amerika. Programu yote ya ile mukutano, ilitolewa ku programu ya Télédiffusion; Sehemu ya 1 ilitolewa Mwezi wa 11, 2023 na Sehemu ya 2 ilitolewa Mwezi wa 1, 2024.
b Ona habari “Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu ‘Nilifurahia Majibu ya Biblia Yenye Kuwa Wazi na Yenye Kueleweka’” yenye ilitolewa mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 1, Mwezi wa 2, 2015.